Wazo langu linafaa?

Kefaville

Member
Joined
Mar 21, 2013
Posts
92
Reaction score
10
Mpaka sasa nimebahatka kua na jumla ya Tsh milion 3, toka zamani nina wazo la kuanzisha saloon ya kiume ambayo ni ya kisasa kabisa na mtaa ninao kaa mpaka sasa ipo saloon moja tu ambayo sio ya kiwango sana mimi nimeona chance na kuweka hiyo saloon yangu ambayo itakua ni ya kisasa kuliko hiyo iliyopo mtaani kwetu vipi wadau niko vizuri au ntakua naleta bifu na huyo ambae tayari anayo ya kwake.

Je pia hili ni wazo zuri au ntakua nimeingia choo cha kike harusini?
 
Ni wazo zuri ila huo mtaji hautoshi kuanzisha Saloon ya KISASA kama ulivyosema, kusanyakusanya mkuu.
 
wazo zuri!lifanyie kazi,usiogope kufungua biashara kwa sababu tayari imeshafunguliwa mtaani au sehemu nyingine!biashara haigombi kila mtu na ridhiki yake!fungua!
 
safi sana ndio challenge ya biashara ila angalia usije ukaviteka vichwa vyangu ntalala njaa na watoto wasiende shule
 
Good idea ungefungua tu kwanza kwa kuboresha mazingira ya nje na ndani hela yako itatosha kwa hapo halafu viti ndio ghali uwe na 4m
 
asanteni sana wadau ngoja nianze na hii afu ya kuboresha ntapata taratibu maana hela mwanaharamu mno atapata matumizi mengne
 
Hongera mkuu we anza na hiyo then vingine unaongeza kidogo kidogo mpaka unafikia sehemu uliyoitaka mwenyewe hata ROMA haikujengwa mara moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…