Habari za majukumu wakuu...
Nimekua na mawazo sana ya kutaka kufanya hiyo shughuli ya uuzaji wa samaki lakini sio mimi binafsi ni kumpa mtu mwengine.
Sasa kinachomifanya hadi leo sijapata ufumbuzi ni kwamba,.. Sijajua faida, hasara na malipo kwa mtu ambae nataka nifanye nae hiyo biashara.
Naamini hapa ni sehemu imara na penye vichwa na wingi wa kila idara. Hapa naamini hawakosi madalali wa ferry pia wataalam waliowahi kufanya huo mchakato.
Nisiwapotezee mda sana, ishu ni kwamba, nataka niingie na mtaji wa milioni 3 kwanza niangalie mwenendo na halisi ya pale. Je naweza kufanikisha zoezi kwa mtaji huo?