Wazungu wavamia Kariakoo kusaka SAMSUNG feki

Huo Msako ufike mpaka mikoani, zipo simu nyingi sana feki. Saaafi sana Samsung, safisha simu zote za kichina takataka hizo. Kama anavyosema Preta siku hizi hakuna heshima bidhaa feki zimejaa madukani
 
Kwa nini wanazichukua tayari ziko sokoni mie naona waanze kuzichukua kuanzia air port/bandarini wakati zinaingia kama wameamua wafanye kazi ya TBS effectively.
 
Good move, ukishindwa kutunza familia atayesaidia ataamua kuanzia popote,kama ada,akiamua nguo za ndani za wife sawa,akiamua kupeleka watoto boarding twendeee!!!!!!

Si umeshindwa bana,tulia tuliiiiiii!!!!!
 
Huu ni wizi mkuu, huwezi chukua simu iliyoandikwa SAMSANG au SINGSUNG kwa kuadai kuwa ni fake ya SAMSUNG kwa kuwa brand name hazifanani hata kidogo.
Hao wazungu watakuwa matapeli wakishirikiana na polisi maana sisi kwa kuogopa ngozi nyeupe hatujambo.
Na je wakizichukua wanazipeleka wapi what if ukija kusikia hawa wazungu ni matapeli tu wanachukua nao kwenda kuuza.
Wangekuwa wanachukua simu zilizoandikwa SAMSUNG wakati sio SAMSUNG original ningeelewa. Laking Singsung na Samsang hizi ni brand name tofauti. Nokia na NAKLA ni brand names tofauti.
Huo Msako ufike mpaka mikoani, zipo simu nyingi sana feki. Saaafi sana Samsung, safisha simu zote za kichina takataka hizo. Kama anavyosema Preta siku hizi hakuna heshima bidhaa feki zimejaa madukani
 
Vizuri si ndio mnavyotaka hivyo,mshawatia watu hasara na bidhaa zenu feki tena wapost humu tuwateteee??jipange kachukue mzigo origanal
 
sipendi bidhaa feki zinatutia hasara sana ila nashangaa kwanini hayo makampuni mama ya huko majuu yasidili na hivyo viwanda hukohuko China? na pia wamepitia wapi hadi kumfikia muuzaji wa rejareja na sio aliyewaagizia au wa jumla. Naona kuna kamchezo hapa wazungu nao wezi wengi tu hata wa ATM wamejaa tele, si ingetangazwa rasmi kwamba kampuni ya Samsung au sijui Nokia wamegundua simu feki na watu wasipokee hizo bidhaa. hii nchi ya ajabu sana kwanini wanazipitisha hizi bidhaa? wenzetu EAC sio walizima na kupiga marufuku toka mwaka juzi sie danadana tu....
Kwa nini wanazichukua tayari ziko sokoni mie naona waanze kuzichukua kuanzia air port/bandarini wakati zinaingia kama wameamua wafanye kazi ya TBS effectively.
 
mpaka zinasafirishwa toka china mpaka tz nani anatakiwa azuie zisiingie sokoni? kwanini wasiende huko china kuzuia hivyo viwanda? au wanaogopa kupigwa kareti na wachina.
 
Saaaaafiiii sanaaaa kamateni na muje huku mikoani kuna mchukue kuna mpaka vijiko feki
 
Sawa bidhaa feki hatuzipendi lakini na huu utaratibu wa kuzunguka na wazungu kuchukua bidhaa za watu ni kinyume cha sheria kabisa na kama nyie wenye maduka mkiwa smart mnaweza kuwashitaki mkala hela ya hatari sana hakuna utaratibu kwenye sheria wa kuzunguka na wazungu mtaani na kuchukua mali za watu na kupotea nazo.Kama mtu akija kuchukua bidhaa yako lazima akueleze yeye ametoka kwenye chombo gani cha kisheria na amekuja kufanya nini na lazima kuwe na exchange ya documentations na barua sio kubeba tu kama nyanya na kuondoka nazo.

Lakini kabla ya kufanya hivyo nendeni kituo cha polisi kilichopo karibu mripoti hiyo incident kama mkikosa ushirikiano wa polisi fanyeni hivi.

Jiungeni changeni hela ya kulipa wakili hao wazungu wakija tena na huyo polisi chukueni details za huyo polisi ikiwemo namba yake jina lake mfanye mahesabu mali zenu zilizochukuliwa na huyo polisi na wazungu zina thamani ya kiasi gani muende kwa wakili wenu muuzieni hiyo deal mtapiga hela hapo ya njenje.

Nyie wafanyabiashara itabidi muwe wadadisi wa kusoma sheria.
 
Wizi wa mchana mchana hapo matapeli wa kizungu wameungana na wakitz kuiba. Samsung ni wakorea sio wazungu ningetegemea sura za kichinchina hapo. wanatakiwa wakamate vitu huko vinakotoka sio vimeshasafiri na kufika dukani na nyie wafanyabiashara mkome kutuchakachua.
 
kama ni hivyo basi na Apple waje haraka.....tunashindwa kuheshimiana huku mjini.........

Mkuu umenichekesha kweli kweli! Nina jamaa yangu aliingizwa mjini akauziwa iPhone 4 kwa 105k, lakini mpaka leo hawezi ku-access internet! ukiiweka mezani in APPLE kabisa, lakini magumashi kwa kwenda mbele! Kweli APPLE nao waje haraka!
 
Nasubiri kwa hamu TCRA watangaze kuziondoa hewani simu FEKI zoote! Wenzetu Kenya walishafanya hivyo, ni vema tuanze kuzoea kutumia vifaa genuine/original, hayo magumashi ya wachina ni janga!
 

Hawa jamaa wameajiri watu kutoka dunia nzima, Samsung ni Global company(MNC) hivyo hiyo bado si justification. Ila nakubaliana na wewe kwamba, kwenye border zetu kuna watu wa TBS na pia nchini tuna watu wanaodeal na counterfeit; hivyo si sahihi wazungu/wachina/wakorea kupita kwenye maduka na kuchukua bidhaa za watu. Wana ushahidi (vipimo) gani unaonyesha kwamba kati ya Samsung A na B ipi feki. Na kama Brand ni Samsang au vinginevyo ndio kabisa hawana jeuri hiyo kwani ni Brand mbili tofauti. Kwanini wasifuate taratibu kama zilivyo kupitia IPR au kuzizuia huko zitokazo. Ila ndio hivyo tuna polisi wajinga na feki so lolote linawezekana.
 
si kuna mamlaka husika zinazo chunguza bidhaa feki hapa nchini? Kwa nn haya yatokee? Yan hii serikali ni majanga kabisa aifai

Hapo hapaitaji mganga kutambua mchawi ni nani. Samsung is a South Korean Electronic Company na hao wazungu wa south nilisikia hadi rafudh yao wapi na wapi
 
Kwa nini wanazichukua tayari ziko sokoni mie naona waanze kuzichukua kuanzia air port/bandarini wakati zinaingia kama wameamua wafanye kazi ya TBS effectively.
Hii ni aibu kwa taifa, yaani nchi iachilie bidhaa feki zinazovuruga biashara ya makampuni hadi waje wenyewe kuchukua hatua!
Hivi ni nini jukumu la TBS, kama wananchi wanaibiwa mchana kweupee na wezi hawa wa Kariakoo wakishirikiana na Wachina? Tumesikia mara kadhaa eti wakikamata bidhaa feki ambazo huishia balbu za umeme na vimdoli vya kuchezea watoto huku wakiziacha bidhaa feki zinazotuliza kila leo na ambazo mara kadhaa tunauziwa kwa bei ya orijino!
Wakati wenzetu Kenya wanatangaza kuzipiga marufuku bidhaa feki hizi zinazovuruga si uchumi wetu tu, bali hata wa wenye viwanda wanaowekeza katika tafiti na kutengeneza bidhaa halisi, nilimsikia kiongozi mmoja 'akiwahakikishia' watanzania eti nchi yetu haitazifungia; maana yake tutaendelea kuwa sehemu ya wahalifu hawa wanaoharibu biashara ya watu!
Yafaa sasa serikali hii dhaifu kuchukua hatua madhubuti za kuondoa bidhaa zote feki zinazozagaa nchini ili kulinda heshima ya nchi hii kwa kujipambanua kuwa si taifa la kuchangamkia takataka za bidhaa feki na za daraja duni kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…