We si unaona kingereza dili..ebu msome jose chamelion

heaven on desert

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2013
Posts
1,025
Reaction score
393
Unaweza kuwa ni miongoni mwa
watu wanaokichukulia poa Kiswahili
na kudhani kuwa kujua Kiingereza
ndio dili! Muulize Jose Chameleone
jinsi Kiswahili kilivyobadilisha
maisha yake. Kupitia Twitter, Jose
Chameleone amekiri kuwa Kiswahili
alichojifunza akiwa nchini Kenya
miaka 10 iliyopita kimemfikisha
hapo alipo leo akiwa mwanamuziki
tajiri na mwenye mafanikio
makubwa barani Afrika.
“The SWAHILI I learnt 10yrs ago
brought mi here. Am JOSEPH,”
ametweet.
Chameleone anajulikana kwa hits
nyingi alizoimba kwa Kiswahili na
kama ukikutana naye na
akakuongelesha Kiswahili huwezi
kudhani ni Mganda, anakijua
vilivyo.
 
Huwezi kumtumia Chameleon kuhalalisha ubora wa kiswahili. Kimsingi Kiswahili ni lugha ya taifa la Tanzania na itabaki kuwa hivyo. Hata hivyo, lazima tuone mbali. Katika soko la dunia ya biashara usomi na sayansi, Kiswahili hakina bao. Chameleon kama mwanamuziki asiyejua Kiingereza vizuri ulitegemea atumie nini? Wanaotaka Kiingereza kitumike mashuleni si kwamba wanapinga kuwa hakina maana. Kiswahili kinafaa kwenye nchi chache na maskini na kwa watu wachache kama Chameleon. Kama Kiswahili kingekuwa ndiyo msingi na chanzo cha mafanikio ya Chameleon basi wanamuziki wote wa Tanzania wangekuwa wamefanikiwa. Nadhani wakati Kiswahili ni lugha ya taifa, Kiingereza ni lugha ya dunia. Ni ushauri tu.
 

wachina wanatumia hicho kingereza chako??
Ji**ga kweli wewe
 
Kiswahili ni muhimu nakubaliana nawe, ila wasanii wetu hawana mikakati ya kazi pamoja na kukosekana kwa mazingira mazuri ya kufanya kazi zao za sanaa ndo maana hawana shavu km "kinyonga".
 
Kuna wakati chameleone alikwenda nchi za marekani. Wakati huo alikuwa anaimba hip hop kama sijakosea (kwa mujibu wake). Na alikuwa akitumia kiingereza katika kuimba. Anadai baada ya show "mlevi" mmoja akamwambia kuwa alidhani ameleta kitu kipya huko marekani kumbe ni yale yale waliyoyazoea, tena (yeye chameleone) ameharibu mno na amejiabisha.

Tangu wakati huo chameleone anadai akabadili staili na lugha katika kuimba. Tangu hapo akaona mafanikio makubwa sana.
 
Kuna swala la kimtazamo na tafsiri.... Hwezi kukipuuzia kabisa Kiingereza. katika soko la dunia ya leo... kiswahili ni lugha ya Tanzania na ukanda unaotuzunguka.. lakini usidanganyike hebu nenda nchi za wenzetu huko majuu na hujui kabisa kiingereza ...lazia utachekesha na utaona dunia chungu... tuheshimu kiswahili chetu lakini kiingereza lazima kukifahamu kupambana na hali zote katika dunia hii
 
wachina wanatumia hicho kingereza chako??
Ji**ga kweli wewe
Sasa ndo kuishiwa hoja au...?? Matusi ya nini..?? Hivi wale mashoga na machangudoa waliofanikiwa kwa shughuri hiyo, unataka tuwaige kwa vile nao imewasaidia??
 
Ni kweli Wachina, hawajui Kiingereza lakini ni nchi ya pili kwa uchumi mkubwa.
Pia muziki hautegemei lugha, kwa sababu wanamziki wengi kutoka KONGO, wamevuma ulimwenguni bila hata kuimba kwa Kiingereza. Fikiria; kama kila kitu kingekuwa kwa lugha ya kiswahili tungehitaji watafsiri na wakalimani wengi & hiyo ingefanya kuwe na ajila nyingi kwenu nyie mnaojua Kiingereza.
>Swali si lugha unayojifunzia bali ni yale unayojifunza.

Mtakumbuka zamani kulikuwa na, SAYANSI YA KILIMO, SAYANSI KIMU[home science], na masomo mengine..watu wanahitaji elimu ambayo wataweza kutumia kwenye maisha yao.
 
Sio wote wa huko "majuu" wanatumia kiingereza kama lugha yao. Ni sisi tu tuliolewa kasumba za kikoloni ambao bado tunasujudia vya watu na kudharau vya kwetu!
 
Hapo nadhani umechemsha!
 
Sio wote wa huko "majuu" wanatumia kiingereza kama lugha yao. Ni sisi tu tuliolewa kasumba za kikoloni ambao bado tunasujudia vya watu na kudharau vya kwetu!

Hebu jaribu siku moja kupanda ndege aidha Ethiopia air line au ndege nyingine zinazokwenda majuu ... halafu uwe hujui kabisa kiingereza...

 
Hebu jaribu siku moja kupanda ndege aidha Ethiopia air line au ndege nyingine zinazokwenda majuu ... halafu uwe hujui kabisa kiingereza...

Acha ulimbukeni. Hebu vile vile jaribu kupanda ndege ya Qatar Airways (hapa nazungumzia 787 Dreamliner) kama hujaelezwa kwamba lugha zinazotumika humo ni pamoja na Kiswahili pia. Uduni wa fikra utakuharibu milele!
 
ukweli utabaki pale pale english bado inatakiwa tujifunze tena kwa kasi ya ajabu kiswahili kinazungumza na watu wengi ukanda wa africa mashariki lakini ikumbukwe kuwa nchi ambazo ni masikini ikiwemo Tanzania tunajitahidi sana kushawishi foreign direct investment na hawa jamaa wanavyokuja lazima ujue jins ya kucommunicate nao kwa lugha kamwe hawawezi kujifunza hicho kiswahili, tungekuwa ni nchi iliyoendelea ambayo ina viwanda vyake hatutegemei wawekezaji waje kwetu hilo naweza kukubali tubakie na kiswahili chetu, kiswahili bora kibaki uraiani kama kenya walivyofanya sioni shida ila shuleni kingetumika english, china wanasema wanaendelea wanatumia lugha yao ila ikumbukwe kuwa sasa hivi wachina ndio wamejaa ulaya kusoma lugha na vitu vingine na hao ndio wamechangia kwa kiasi kikubwa fees kupanda mara kwa mara kutokana na demand kubwa ya wachina kuja kusomea lugha na mchina akiwa ana jua english ni rahisi kupata kazi nchini kwake kuliko yule ambae hajui kwa sababu kampuni nyingi china zimekuja kuwekeza kule kwao wanataka mtu ambae anajua english ambae atawakilisha vyema katika mawasiliano, wakati china wanaingia kwenye FDI wananchi wengi kutoka hong kong walipata kazi mainland waliajiriwa kule kwa sababu wakati waingereza wanawatawala mpka 1997 walipoachiwa walikuwa wanasoma english tu kwa muda wa miaka 100 kwenye utawala wao so communication kupitia english ilikuwa poa, now na wenyewe wa mainland wameamka ni full kutembea dunia kujifunza lugha, hatukidharau kiswahili ila lazima tuendane na utandawazi, viongozi wetu wanatudanganya tukienzi kiswahili chetu ilingali hakuna hata mtoto wake ambae anasoma kwenye hizi shule zinazofundisha kiswahili ni international tu mwisho wa siku fursa ikitoka huyo mtoto ana chance kubwa ya kuajiriwa kuliko sisi wakina kayumba,
 
Aisee UKI, tafadhali hebu fafanua hapo. Ni Ulaya gani hao wachina wamejaa kusoma lugha. Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Uholanzi, au...?
 
Last edited by a moderator:
mkuu university nyingi sasa hivi za uk kwa jinsi nilivyoona na wala sio kusimuliwa ukiangalia class wanafunzi wanaongoza kuja kusoma uk ni wachina na hii foundation class zilikuwa hazipo ila zimeanzishwa siku hizi special for chinese kusoma lugha then unaendelea kusoma degree yako au master yako, foundation za lugha 80% wanaosoma huku ni wachina, vyuo muhimu tena vile vyenye high rank uk wanaongoza kuja kusoma kutoka nje ya uk ni chinese ukienda hata oxford city kipindi cha masomo utafikiri upo china wengi wao ni chinese na hata baadhi ya wachambuzi wa mambo walikuwa wanazungumzia kwenye mjadala wa elimu kuna project ilifanywa na oxford uni wakishirikiana na wanafunzi ila kuja kuangalia wanafunzi wenyewe kati ya 20 ni saba tu waingereza 10 ni chinese na 1 nigeria na 2 indian, na ukweli wachina ni wepesi sana kuifunza lugha hizi foundation za one year wanazosoma wakimaliza wanajua hasa na fees foundation ni karibia £8500 kwa mwaka, mkuu kwa reference tembelea tovuti za vyuo vya uk utaona hizo. kumbuka kuja kusoma uk lazima uwe unajua lugha na upimwe IELTS test ila hawa wachina huwa wanalipia hizi foundation class wakiwa hapo airport hata kujieleza ni inshu UK borders walilalamika sana suala hili kuwapa visa chinese kuja kusomea lugha uk ilingali hata lugha ya kujieleza hawajui ila mpka sasa hawajapata ufumbuzi wowote maaana vyuo vingi villilalamika endapo wasipopatiwa visa vyuo vingi vitakosa wanafunzi kumbuka sheria zao walizibadilisha mwaka jana 1st april 2012 na mpka december 2012 international students acha china kuja uk imepungua kwa 19,000 students lakini china imeongezeka kwa 14000 na inazidi kuongezeka na wachina ni wateja wazuri wa uk maana wao wakiingia uk hawana shida ya kutafuta kazi wao ni kutumia na kufanya shopping tu maana pesa wanazo kwao wanaona burudani. na ukiongea na chinese ukimuuliza kwanini umekuja uk anakuambia ukiwa unajua kiingereza kwao unapata kazi rahisi sana so wanajitahidi wajue lugha ili wakienda kwao wawe na kazi nzuri sio maneno yangu ni maneno yao maana hata china sijafika. na kumbuka wanafunzi report za 2011 wachina kwa wastani wa wanafunzi 540000 kwa mwaka walitoka kwenda nje kutafuta elimu sehemu walizoenda ni usa inaongoza inafuata uk, australia, canada, germany(psotgraduate wanafundisha kwa kiingereza baadhi ya vyuo) france na holland, hiyo ni kwa mwaka tu na wait usubiri report ya 2012 tutasikia walienda wangapi, hii idadi ni kubwa sana, wote hawa wanaenda kusoma kwa kiingereza na sio kichina kwenye hizo nchi husika,
 
Je vipi na Wajerumani (kwa mfano) nao wamejaa huko Uingereza kujifunza hiyo lugha? Umeandika mengi lakini sidhani kama yanao ushawishi wowote wa kile unachotaka kutilia mkazo! Swala litabaki pale pale: heshimu na tukuza utamaduni wako kama unataka kuheshimiwa hapa duniani. Kuendelea kutukuza Kiingereza na kudharau Kiswahili ni njia moja wapo ya kutufanya tuendelee kujiona duni maishani. Trust me, Bro, nipo huku "Ulaya" kwa miaka takriban thelathini na sioni ukweli wa hayo uyasemayo!
 

mkuu nahisi wewe ndio umenielewa vibaya kamwe sijazungumzia chochote kukidharau cha kwetu na kukiheshimu cha wageni mimi nimezungumzia pamoja na kufahamu lugha yetu vizuri ila lugha ya kiingereza nacho kina umuhimu wake mkubwa kwa ajili ya mawasiliano na wengine katika mataifa mengine na nilikuwa najibu hoja kuna mtu alisema china hawaongei english nikawa najibu kuwa hata wao wanajifunza english kwa nguvu zote ili waweze kuwasiliana na mataifa mengine. nikawa napinga viongozi kutuambia tuendelee na lugha yetu ilingali watoto wao wanawasomesha nje waanze wao na sisi watoto wa wakulima tutafuata, sijasema kamwe lugha yetu ni mbaya.
 
Sawa, nimekusoma. Tatizo ninaloliona ni lile la "wasomi" wetu kushobokea Kiingereza hadi wanashindwa kujieleza kwa Kiswahili ili kufanikisha mawasiliano na wananchi wa kawaida. Huu ni ulimbukeni chakari. Hapo hata hao Waingereza ni lazima watucheke!
 
Ni kweli kiswahili kidumishwe ila english pia muhimu ... nilikuwa nchi flan nikaenda hospital na hakuwepo hata dr kwa wakati huo anaeongea eng.. ilibidi nirudi na kupangiwa appointment siku nyingine kusomea majibu yangu akiwepo dr anaeongea eng. Kama ningekuwa sijui japo kidogo siijui ingekuwaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…