WEF yamtaja Mkurugenzi TWAWEZA, Aidan Eyakuze, miongoni wa watu 50 wenye ushawishi na wanaohamasisha mageuzi ya kiutawala

WEF yamtaja Mkurugenzi TWAWEZA, Aidan Eyakuze, miongoni wa watu 50 wenye ushawishi na wanaohamasisha mageuzi ya kiutawala

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
aidan.jpg

Eyakuze ni mmoja kati ya Waafrika watatu pekee kwenye orodha hiyo na mmoja kati ya 11 ambao hawako katika utumishi wa serikali.

Taasisi ya Jukwaa la Uchumi Duniani (WEF) inayoshughulika na utawala bora na Apolitical, zimemtambua Eyakuze kwenye orodha ya watu 50 wanaohamasisha maboresho na mageuzi ya kiutawala baada ya mapendekezo ya wataalamu, utafiti kufanywa kwa waliopendekezwa na baadaye mapendekezo hayo kupitiwa na taasisi ya WEF.

Washiriki huchaguliwa kutokana na sifa mbalimbali za uongozi zikiwamo: Kuweka msisitizo kwenye matokeo, ubunifu na kufanya majaribio, pamoja na uhusiano na wadau kijamii, kitaifa na kimataifa.

Taarifa iliyotolewa na TWAWEZA kwa vyombo vya habari jana ilisema, Eyakuze alichaguliwa kama mmoja wa watetezi bingwa wa wananchi wa kawaida.
 
Pamoja na kuwa "quite" mda mrefu hivyo? Mbona hatusikii tafiti zao siku hizi? Ninahisi wamekabwa koo.
 
Twaweza Mbona Walikubali Matokeo Siku Nyingi. Nadhani Kwa sasa wapo wapo tu ili Tonge liende Kinywani.
 
Aandaye vyeti vya kuzaliwa vya bibi, babu na nyanya zake. Jiwe hawapendi Sana watu wenye akili kama Eyakuze.

Jiwe anapenda walamba viatu na vilaza.
 
Back
Top Bottom