Tutor B
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 9,025
- 6,598
Iko hivi:
Wazo la mradi / biashara likitolewa na mtu ambaye hana mtaji - pesa - (star-up capital) huonekana kama ni upuuzi. Sio kwamba huwa ni upuuzi bali upuuzi huwa ndani ya anayelipokea wazo hilo. Wazo lenyewe huwa liko pale pale na thamani yake iko pale pale na likifanyiwa kazi linazaa matunda mema. Hivyo upuuzi ni ndani ya anayelipokea.
NA PIA
Mtaji (Pesa) kwa ajili ya mradi / biashara (Star-up capital) alio nao mtu ambaye hana wazo lolote ni kama makaratasi. Sio kwamba thamani ya mtaji huo haipo bali ubovu wa thamani ya mtaji huo upo ndani ya mmiliki wa mtaji huo.
Hivyo katika hali zote mbili mwenye kukwamisha maendeleo ya sehemu yoyote ile ni yule mwenye umiliki wa mtaji (pesa) pasipo kuwa na akili za kuifanyia kazi.
Jiulize: Una wazo lolote au una mtaji pesa.
Wekeza kwenye fikra / maarifa; huko ndo kunakosemekana kwamba hakuna uharibifu wowote ule (hata Biblia inaweka ilo wazi) ila kwenye vitu vya kuonekana kuna uharibifu wa wazi.
Ni kwa nini pesa huondoa uwezo wa mtu kufikiri?
Wazo la mradi / biashara likitolewa na mtu ambaye hana mtaji - pesa - (star-up capital) huonekana kama ni upuuzi. Sio kwamba huwa ni upuuzi bali upuuzi huwa ndani ya anayelipokea wazo hilo. Wazo lenyewe huwa liko pale pale na thamani yake iko pale pale na likifanyiwa kazi linazaa matunda mema. Hivyo upuuzi ni ndani ya anayelipokea.
NA PIA
Mtaji (Pesa) kwa ajili ya mradi / biashara (Star-up capital) alio nao mtu ambaye hana wazo lolote ni kama makaratasi. Sio kwamba thamani ya mtaji huo haipo bali ubovu wa thamani ya mtaji huo upo ndani ya mmiliki wa mtaji huo.
Hivyo katika hali zote mbili mwenye kukwamisha maendeleo ya sehemu yoyote ile ni yule mwenye umiliki wa mtaji (pesa) pasipo kuwa na akili za kuifanyia kazi.
Jiulize: Una wazo lolote au una mtaji pesa.
Wekeza kwenye fikra / maarifa; huko ndo kunakosemekana kwamba hakuna uharibifu wowote ule (hata Biblia inaweka ilo wazi) ila kwenye vitu vya kuonekana kuna uharibifu wa wazi.
Ni kwa nini pesa huondoa uwezo wa mtu kufikiri?