Wema, aunt, kajala: Aibu yao!

Lugano5

R I P
Joined
Jul 15, 2010
Posts
4,520
Reaction score
757
WEMA, AUNT, KAJALA: AIBU YAO!

Stori: Imelda Mtema, Arusha


Jambo limezua jambo! Mastaa ‘hot' Bongo wanaotingisha kwenye tasnia ya sinema, Kajala Masanja, Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wamepata aibu baada ya kugandwa na skendo ya kwenda kujiuza jijini Arusha.


Mastaa wa filamu kutoka kushoto ni Wema Sepetu, Aunt Ezekiel na Kajala Masanja.


Skendo hiyo ilikuja baada ya mastaa hao kutimba jijini humo ikiwa ni ziara ya kwenda kumtambulisha msanii wa Bongo Fleva anayesimamiwa na kampuni ya Wema ya Endless Fame Films aliyetajwa kwa jina moja la Mirrow.

ETI WALIITWA NA MABILIONEA WA ARUSHA

Habari za chini kwa chini zilidai kwamba nyuma ya ziara ya mastaa hao kulikuwa na msukumo wa mataita (mabilionea wa Arusha) ambao waliwaita ili ‘wajilie vyao'.
"Kuna mtu alipewa tenda awapeleke akina Wema na kweli walifanikiwa kuwateka matajiri wa Arusha.
"Nakwambia mapedeshee wa mawe (madini) waliposikia tu watoto (akina Wema) wapo Arusha walifurika pale Club Tripple A na baadaye hotelini walikofikia pale Point Zone maeneo ya Mianzini.


Mastaa Wema, Aunt na Kajala wakionyesha maungo yao.

"Shughuli za kisanii, sijui eti kumtambulisha Mirrow ilikuwa ni gia tu ya kwenda kuwaburudisha mapedeshee wa A Town," kilidai chanzo chetu ambacho huwa hakichezi mbali na mastaa hao na kuongeza:

WALIVAA KIHASARA MNO

"Wewe angalia tu walivyokuwa wamevaa kihasara, lengo lao lilikuwa ni kuwatega wanaume."
‘Kikulacho' huyo aliendelea kudai kwamba mastaa hao wakiwa Arusha, namba zao ziligeuka ishu baada ya kuuzwa kwa bei mbaya kwa kila tajiri aliyehitaji.
"Nakwambia hata ungetokea ukasema una namba ya mmojawapo ungelamba mshiko mrefu maana kuna shosti yao mmoja aliondoka na fedha ndefu kwa kutoa tu namba zao," alisema na kuongeza:
"Aisee hata pale hotelini wahudumu walisumbuliwa sana kutumwa kwenda kuomba namba za simu za akina Kajala."

WENYEWE WAFUNGUKA

Baada ya kujazwa madai hayo, gazeti hili lilizungumza na mastaa hao mmoja baada ya mwingine ambapo wote walinena juu ya skendo hiyo.

Mastaa wakipozi kitandani pamoja na Mtangazaji Zamaradi.

KAJALA

Akizungumzia ishu hiyo baada ya kupewa mkanda mzima, Kajala alikuwa na haya ya kusema:
"Kwanza haiingii akilini kabisa, nitoke Dar niende Arusha kujiuza kwa sababu gani? Au kwa ajili gani? Sisi ni watu ambao tunajiheshimu, mtuone hivihivi.
"Tunajua tulienda Arusha kwa sababu gani na ndicho tulichokifanya na si vinginevyo.
"Kuhusu nguo tulizovaa, mbona ndiyo mavazi yetu ya kawaida sana? Siku zote tunavaa hivyo jamani, wanaosema tulitaka wanaume hawana jipya.
"Kuhusu namba zetu kuuzwa, watu watakuwa ni wao maana sisi muda mwingi tulikuwa hotelini."

AUNT EZEKIEL

Kwa upande wake Aunt Ezekiel alitiririka: "Kwanza kabisa majibu yote ungekuwa nayo wewe (mwandishi wetu) maana kila dakika tulikuwa wote na kila mtu unajua alilala na nani.
"Hao mapedeshee kama walikuwa wakizunguka hotelini ni juu yao lakini sisi tulienda kwa ajili ya kazi tu na si vinginevyo.
"Kuhusu nguo fupi, kwa upande wangu sioni kipya kwa sababu tangu nikiwa mdogo ndiyo nguo zangu.
"Siku zote mtu akisema nguo zangu ni za kujiuza, hana jipya tena ni mzushi wa hali ya juu."


Mastaa hao wakiwa stejini ndani ya Triple A.

WEMA

Alipotafutwa ‘mama lao', Wema aliwaka: "Huyo aliyesema hayo mambo ni mpuuzi. Kwanza mawazo yangu yalikuwa hayawazi huo upuuzi kabisa.
"Akili yangu yote ilikuwa kwenye shoo tu maana nilikuwa nawaza itafanikiwa au vipi na ndiyo maana imefana kama ulivyoona.
"Tangu nilipofika hotelini nilikuwa nikilala na Kajala hadi siku naondoka maana tulikwenda na kitu kimoja kwa nini tujichanganye na vitu vingine visivyokuwa na manufaa kwetu?
"Kwa sasa nimetulia na mtu wangu, niende kuhangaika na mapedeshee wa nini?
"Mbona hakuna nafasi hiyo kwa sasa? Mavazi yangu ni ya kawaida siku zote
 
Mbona kawaida yao ila Kajala kawafunika ile mbayaaa duu
Hako kengine ni ka Zama au nakafananisha.....
 
Makahaba wenye viwango wako bongo movie....nani asiyejua hawa ni Makahaba. ..wao wanadhani kujiuza ni mpk wasimame barabarani....huyo wema kauza kwa wangapi.?? Aunt naye kauza kwa wangapi.?? Kajala nae ndo wale wale ss hivi.anauza kwa mghana....umri unaenda ustaa una mwsho ohoo
 
Hao ni wanawake hat wakitoa nanii zao ni haki yao, ilimrad tu wabaki njia kuu
 
hii habari yakimbea sana no wonder imeandikwa na zile zile tabloids. mimi nimechek leo kwenye kipindi cha wema, unasema show ilijaza watu ndip kujaza kweli pale? nonsense!
 
kipi kipya hapa?

ngoja nisubiri kesi ya lulu nijue hatma yake..! najua mwisho wa siku ni fine ya laki tano!
 
Hao ni wanawake hat wakitoa nanii zao ni haki yao, ilimrad tu wabaki njia kuu

Alafu cha ajabu utakuta hata mwanaume naye anawaponda wakati wao ndio chanzo kikuu....na ukibahatika kumkuta kona anavyobembeleza huku analia apewe njia kuu.........wanagawa kwa sababu nyie ndio mnaowasumbua wawape......................MWE......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…