Wema: Nitalipa pesa matibabu ya baba Diamond

Mimi nafikiri Baba yake Diamond ni mtata sana, labda ndio maana aelewani na mtoto wake - kama mzazi kwa nini atafuti njia ya kistaarabu ya kumaliza tofauti zao - haya mambo ya kukimbilia wana habari, kupiga piga picha kumlalamikia mwanae anafikiri kutamsaidia nini - si ndiyo kutawafanya Diamond na mama yake kukasirika zaidi?

Yeye anazungumzia upande wake tuu - mbona watu/waandishi awaendi kwa Diamond na mama yake wakasikia wana malalamiko gani kuhusu mzee huyo - siyo vizuri Baba yake kila siku kutafuta sababu za kumdhalilisha mwanae.
 
Alieleza kwa kirefu sana chibu kuhusiana na hii makitu hii, (kuwa baba ni kazi ya ziada), sio kusababisha tu kupatikana kwa mtoto
 


Anazungumzia upande wake au usio wake! Hakuna haja ya mtu kuchangia 20m mahali huku Baba yake anaugua, hata Kama anafanya kosa gani, Baba Ni Baba tu na wengi.
 
Dada Wema tenda Wema nenda zako M/mungu atakuzidishia pale ulipotoa/utakapo toa.

ONYO:
Tafadhali usijejutia msaada utakaotoa/ulioutoa Kwa baba Diamond pindi kauli zitakapo pishana na wenye baba yao.
Mfano:
1. Kilichotokea Kwa kajala baada ya kumlipia pesa mahakamani.
Ulijilaumu na kujuta kumsaidia.
 
Unapokuwa umenenewa neno baya nenda huko alikokunenea ukasema huyu alilonena c kweli kuna hivihivi lkn kama linasemwa ww uko kimya basi kunajambo?ww bahat sjui kama unazifaha tabia za wanawake juu ya watoto wao hasa wa kiume lkn ukiwa mtoto ww ni mtoto tu neno baba ni kubwa sana na lenye baraka,kumbuka watu hawa Hawa (eva)Delira,Sarah na wengi wa mifano hiyo ndo utajua mwanamke ni nani,mungu akupe akili ya kuwatambua hao watu wanaoitwa wa mama.
 
Hizi ni family issues zina mizizi na mlolongo wa matukio tusishadadie tusiyoyajua tusiwe na upande bali matukio kama haya yatupe nafasi ya kujifunza na kujitafakari
Laiti ungekuwa ww unazani kifo chako ingekuwa fundisho kwako?mbona inaonekana ww katiri.
 
Kujipendekeza pendekeza tu kwa chibu
Kwa kawaida kujipendeka mtu humfanyia ihsani mtu ampendae mfano wema akimfanyia ihsani mama chibu waweza kusema anajipendekeza ili mama chibu amseme wema kwa chibu kuwa kuna na, wema atakufaa na sio kwa babayake mtu ambae sikuzote huonekana kama hatakiwi hivi alafu mtu akajipendekezesizani kama kutakua na mafanikio au nawe unapenda kusikia baba chibu akiteseka?
 
Soma kwa makini nilichoandika kisha tafakari kwa makini
Je hiyo mizizi. Ndo iwe sehemu ya kukimbiana?mungu ana maana sana ww kuitwa baba lkn ikumbike Eden baada ya shida ile ni nani alikuwa mdanganyifu?wa mama wameumbwa kwa namna ya ajabu sana wafitinishi tena wenye kudanganyika swala la matatizo ya kifamilia eneo kubwa chanzo cha mambo yote ya matatizo ni mwanamke.
 
Huyu alijidai mjanja wakati diamond akiwa bado dogo.
Sasa anajuta na kutaka kulazimisha ha ha ha.
 
Ni ujinga upi tena inamaana mtu akikosa msaada kwako ndio baasi asitokee mtu mwingini akamsaidia ndio unakua mjinga? Hapana kiongozi tujifunze kuhurumiana
sawa sijakataa kua asaidiwe!hv wa kumsaidia kamuona mzazi wa diamond tu!!?!!
wangapi wana shida!?kila siku wanatangazwa kuna yule binti wakonta kapunda mbona sijaona aliposema atamsaidia?!
na wengine wengi,hizo ni sifa tu za kijinga kwake….!!anatafuta kuwin majority!![emoji57]
 
Bado nasisitiza hii ni ishu ya kifamilia na kwakuwa ni Diamond
Huku mitaani kuna worst cases kuliko hii...kuna watu wako hoi hasa wako kwenye hospitali zetu huyo mzee daily yuko kwenye vyombo vya habari...tuwe watu wa tafakuri
Baadhi hapa wanajifanya kumuonea huyo mzee huruma na kumlaumu Diamond wakati nao wana vimeo kama hivyo kwenye familia zao....nasisitiza Tujitafakari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…