Wema Sepetu atumbuliwa jipu

Nachojua mimi mteja akigundulika kaliibia shirika anashitakiwa na akipatikana na hatia anafungwa na kulipa gharama zote za kesi pamoja na pesa anayodaiwa na faini juu,sasa inakuwaje huyu analipishwa tu bila ya kupelekwa mahakamani kujibu shitaka lake ??????????????
 
leo kwenye orodha ya wadaiwa sugu wa tanesco yupo staa wetu wema sepetu.deni ni tsh milioni 8.sijui imekuwaje mtu adaiwe kiasi chote hicho wakati sis hata deni la buku 2 wanakata umeme??

Umemsahau deni la mil 9 la maji Dawasco.
 
Anaweza kuwa sio kosa lake kutokulipa TANESCO ni wazembe mi nilikaa mwaka na zaidi hawaleti bill kwenda kufuatilia na wakaanza kuniletea nikaanza kulipia bil ilikuwa ndogo sana mpaka nikawa nashangaa mwisho wa siku kutaharuki hao wamefika wanataka kukata umeme wananiambia ni mdaiwa sugu nadaiwa M2 na laki mbili kufuatilia wakaniambia nilikuwa nalipa service charge tu hapo nani wa kulaumiwa pengine na mwezetu yamemkuta hayo na vile hatujapata nafasi ya kumsikiliza na yy hatuwezi Kumjudge moja kwa moja kwamba mwizi
 
Ila hilo deni linachekesha, matumizi ya nyumbani tu million 8,au ana kakiwanda humo....na tanesco walikua wanaanglia tu hadi deni linafikia hivo, au wanamsingizia?
Tanesco hawakua wanaangalia tu, huyu alikua anaiba umeme, umeme ulikua hausomi kwenye mita ulikua unaingia moja kwa moja kwenye nyumba.
Hiyo milioni 8 ni gharama ya umeme alioiba toka hiyo mita haijawahi kusoma umeme hadi siku ya ukaguzi.

Wema alifanya kitu wanaita internal bypassing. Umeme unakua unaingia ndani ila hausomi kwenye mita,kila siku mita inasoma 0 units ila umeme unawaka ndani.
 
Si kweli kwamba Wema Sepetu alikua na deni hilo la milioni 8,hii ni special alliance kati ya Wema Sepetu na Tanesco Mass Com Department kuhakikisha jamii inaogopeshwa vya kutosha watu walipe madeni...


Ni kuogofya watu waone "haa kumbe hadi staa anaeabudiwa na waswahili nae anashikwa basi wapo serious ngoja niache kuiba umeme",hii itakua special alert kwa domestic users ambao ni ngumu kumpitia mmoja mmoja watu wanafunga mageti yao...ila viwandani wanawaweza wanaingia ndani any working time...

Mi sidanganyiki eti wema kashikwa na deni la mil8,na siku anashikwa ni uigizaji mtupu
 

Wee nawe kwani hukuona ile mita ilivyokua? Ile mita waliifungua na kuchomeka kiwaya na kuufanya umeme usisome uingie direct alafu wakaifunga basi wakaendelea kula umeme. Sasa kama sio wizi wewe mpaka unaibomoa luku na kuongeza viwaya vyako alafu unasema usikilizww ili iweje
 
Hii ya Wema ni hoax....wameenda na ile "ogopesha watu ,watalipa tu"....na hii kampeni itakua imefanikiwa sana,mno...wezi wote domestic lazima wakae sawa...good strategy
 
Waliomtuma kutukana matusi watu wenye umri wa marehemu baba yake wamlipie hiyo bili kumsitili na aibu hii...Mama Samia anaangalia tu campaign manager wake anavyodhalilishwa

Mama ongea na mwanao!
 
Waliomtuma kutukana matusi watu wenye umri wa marehemu baba yake wamlipie hiyo bili kumsitili na aibu hii...Mama Samia anaangalia tu campaign manager wake anavyodhalilishwa

Mama ongea na mwanao!

Ahahahah eti mama ongea na mwanao, wewe chiz kwel
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…