wenye diploma ya MEDICAL tuwaitaje au nao ni MADOKTA??????


Kitanda usicho kilalia huwajui kunguni wake, kutokana na uhaba wa madaktari ni kweli wanafanya kazi, ila kazi zao nyingi ni za mazoea, suala la ufaulu usidanganye, fuatilia profile zao kwa karibu, wapo ambao hata kuandika majina yao ni ishu.

Kwanini wanadharaulika? Hilo ni kosa la kimfumo wa mafunzo ya udaktari kwa Tanzania, kwa nchi za wenzetu advanced diploma ya medicine haipo, tunayo sisi tu Tz, hivyo kimataifa hawatambuliki!
 
ndio, kuna ambao wanachukua AMO za medicine na wengne AMO za immunology, parasitology..kama kuna mtu anaesoma AMO muhimbili ungejaribu kumuuliza kuhusu hili

Hata wakati nasoma undergraduate(hapo hap muhimbili) hakukuwa na kitu kama hicho, labda miaka hii mambo yamebadilika.

Mkuu..nijuavyo mimi kuna postgraduate diploma..na ndio maana nikasema mwanzoni tusitafsiri postgraduate kama specialization...How can you specialize into s'thing you havent done in full measure?

na ndio maana kuna watu kama Anaesthesiologist na Anaesthetist, au Optician na Optometrist..simply kwa kuangalia utaita "wame_specialize" wote lakini si hivyo.
 
Tofauti ya tabibu na daktari ni ipi?
Kwa mimi naona tofauti lugha (na kama tofauti lugha, kwa mujibu ya maneno yako ACO na AMO watakua sawa)

Tabibu stands for low cadres, ni sawa na mwalimu wa upe,
 

Fikiria hiyo red!
Hata nyumbani baba asipokuwepo mama anakuwa kichwa cha Nyumba, but haimaanishi mama ni sawa na baba!!
 

Huo ni uongo Mkuu, hakuna kitu kinaitwa AMO in medicine!!

Na muhimbili hicho kitu hakipo, labda Tanga, ifakara na Mbeya,
 
Huo ni uongo Mkuu, hakuna kitu kinaitwa AMO in medicine!!

Na muhimbili hicho kitu hakipo, labda Tanga, ifakara na Mbeya,

Nliandika mimi icho kitu (bold), apo nimechemka. I'm not medical specialists
 

Majibu kumbe unayo, nadhan utakubaliana nami kuwa hawa jamaa kiwango chao cha kufaulu ni cha chini, tofauti na ilivyoelezwa hapo juu

Napenda kuvijua hivyo vyuo nje ya bongo ambapo mtu anaweza kusoma masters speciality bila ya kuwa na 1st degree
 

Well stated colleague
 
Majibu kumbe unayo, nadhan utakubaliana nami kuwa hawa jamaa kiwango chao cha kufaulu ni cha chini, tofauti na ilivyoelezwa hapo juu

Napenda kuvijua hivyo vyuo nje ya bongo ambapo mtu anaweza kusoma masters speciality bila ya kuwa na 1st degree

Nje ya Tz sivijui, bt nliskia Mzumbe wanatoa masters kwa advanc diploma (kama sikosei ipo course inaitwa health management) kwa fani ambazo si za afya, IFM pia wanatoa masters kwa advance dip
 
Kuna ambao wanachukua diploma halafu advanced diploma halafu post graduate/masters..sasa hawa si madoctor kwasababu hawakuchukua medical doctor (MD)?
Doctor ni mtu yeyote ambae ana diagnose na ana treate, ACO,CO,AMO,MD..wote wana kazi nlizotaja

Post graduate masters ni lazima uwe na 1st degree, ila post graduate diploma si lazima uwe na 1st degree.
Halaf coarse content ya post graduate masters ni tofauti na post graduate diploma!

Doctor hawezi kuwa mtu yeyote mwenye sifa hizo, kama ni kweli hata mama zetu ni madaktari, sababu wanaweza kujua mtoto anaharisha wakampa maji mengi na labda maji ya chumvi chumvi na mtoto akapona.

mambo si marahisi kihiiivyo!!
 
Nje ya Tz sivijui, bt nliskia Mzumbe wanatoa masters kwa advanc diploma (kama sikosei ipo course inaitwa health management) kwa fani ambazo si za afya, IFM pia wanatoa masters kwa advance dip

Hizo ni post graduate diploma, tatizo wabongo tunapenda sana kujipaisha, kwa mfano tunaita kidato cha tano na sita high school ( Mzumbe High School), ni uzushi huo, hiyo ni Mzumbe swcondary school, na hata vyeti vya necta ni ASCEE
 
Hizo ni post graduate diploma, tatizo wabongo tunapenda sana kujipaisha, kwa mfano tunaita kidato cha tano na sita high school ( Mzumbe High School), ni uzushi huo, hiyo ni Mzumbe swcondary school, na hata vyeti vya necta ni ASCEE

Hahah Tz tupo juuu.
High school inakuaje mkuu, mana high school Tz zipo nying?
 
Hahah Tz tupo juuu.
High school inakuaje mkuu, mana high school Tz zipo nying?

Hakuna high school bhana, nenda kaulize usajili baraza la mitihani au wizara ya Elimu kama hicho kitu kipo!

Mimi sikusoma high school vyeti vyangu vyote ni secondary school na university!
 
let the community decide!kadri kiwango cha elimu kitakapokuwa ndivyo utofauti utakapo onekana.leo hii ukiwaambia watu wa vijijini wanahudumiwa na wakunga badala ya madaktari watataharuki mno.
 
let the community decide!kadri kiwango cha elimu kitakapokuwa ndivyo utofauti utakapo onekana.leo hii ukiwaambia watu wa vijijini wanahudumiwa na wakunga badala ya madaktari watataharuki mno.

Haha..na heri kwetu wazee na watu wa makamo maana vijana wakisema hivyo huambiwa "kijana, huna heshima...yaani daktari wetu unamuta hivyo?, ametutibu tangu zamani, miaka yote hii tunajua ni daktari, na anatutibu tunapona, sasa unasemaje yeye si daktari?"..anyway, uelewa wetu(watanzania bado ni mdogo-no offense)..na wale wasio na uelewa ni wabishi, kwa kile kidogo SANA wanachokijua wako tayari kukibishia hadi kufa, kuliko kutumia nguvu kidogo zaidi kuongeza ufahamu.
 

Acha niwaachie wenye kitanda mtiririke maana mie sijui kiwango cha kunguni waliopo ila nilichosema mie huo ni mwanzo kuelekea huko kwenye degree maana watu huwa tunaponda taaluma za watu wakati tatizo sio lao ni la kimfumo kama ulivyosema hasa ukizingatia kwa muda mrefu tumekuwa na chuo kimoja cha udaktari zamani chuo kikuu kishiriki Muhimbili na ili uingie Muhimbili ulikuwa unahitaji upate ufaulu wa hali ya juu na waliokuwa wanabaki ndio walikuwa wanaingia kwenye hivi vyuo na kuwa AMO (kwa waliosoma miaka 90 wanajua kwamba ili mtu uingie chuo kama Muhimbili ulikuwa unahitaji maksi nzuri sana) (kama mtu hata kuandika jina ni issue hilo sasa ni lingine either limetokana na uchakachuaji wa udahil maana sifa za anaetakiwa kuchukua Diploma zinajulikana kama amemaliza form 6 maana yake O -level alifaulu na kupata credit na mara nyingi ili uchukuliwe lazima Chemistry na Biology uwe umepata kiwango cha C kwa O level hata huku chini tumeshuhudia watu wanaingia form 1 hawajui kusoma na kuandika), mie observation yangu ni hiyo maana nachojua kuna ambao ni RMO (Rural Medical Officer) hawa wengi wao hata mie nimewashuhudia kuna utata kuhusu ufaulu na wengi wao hupelekwa vijijini kabisa kwenye zahanati alafu hawa AMO wanakuwepo kwenye vituo vya afya na wengine wapo mpaka kwenye hospitali za wilaya na mikoa ila pia kuna hawa AMO wengi ninaowajua performance yao ilikuwa nzuri O level na wengi ni wale ambao kidato cha sita walifaulu kiwango cha kawaida ambacho hakikuwazesha kuingia university pia baada ya kufanya kazi kwa kutumia vyeti vyao hivyo hivyo huingia university za Tanzania na wengine mpaka Urusi wamekwenda

Mie sio kitanda nacholalia ila kwenye sekta hii kuna levels nyingi mpaka wakati mwingine inachanganya na ukifanya mashala unahudumiwa na mtu ambae sie mfano wewe umeleta tena Advanced Diploma (ambayo ni 3 years sijui kwa upande wa medical ni miaka mingapi), kuna hao wenye Ordinary Diploma (ambao mdau ndio amewazungumzia) alafu kuna ambao wameishia O-level wakaenda kupata certificate ambao hawa ndio RMO sasa ndio huwa kwenye zahanati.

Kiukweli sio madaktari ila nimesema kibongobongo ni madaktari maana tunaowaita ni sie wananchi na hasa ukizingatia wengi masomo ya sayansi tuliyakimbia hivyo akitupa zile terminology zao za kitabibu awe RMO, AMO au Daktari mwenyewe tunajua ni madaktari hivyo hata kisaikolojia tu ukishamjua mtu sio full dokta mfano sidhani kama utamwamini kama atakuhudumia na ndio maana kwa kutambua hilo kuna huduma ambazo zimeanishwa kufanyika kwenye Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitari za Wilaya, Mikoa mpaka Hospitali za rufaa ili kutoa ukomo wa huduma zinazotokana na complication za kitabibu na staffing tulizonazo.

Hii ni changamoto tu mkuu kinachotakiwa ni kuwatia moyo wataalamu wetu hawa pia vijana wetu huku kwenye mashule kuwatia moyo kuchukua masomo ya sayansi mwisho wa siku tutaondoa tatizo though bado hawa watu watahitajika tu kwa kufanya kazi chini ya usimamizi (na hicho ndicho kinachotakiwa ila kwa sababu ya changamoto hizo ndio unamkuta mtu amekalia kiti akitoa huduma na imekuwa mazoea ya kuwaita madaktari ila kwa werevu huwa tunajua si madaktari kwa kuwa wananchi wengi wanajua ni madaktari acha wawaite madaktari kwani kisaikolojia ukiwa na imani na mtu anekutibu pia inaongeza kasi ya kupona kwa kuwa unakuwa huna mawazo na hofu)
 

advanced diploma ya medicine haiko sawa na md hata siku moja. Md ni muunganiko wa bachelor mbili ambazo ni bachelor of surgery na bachelor of medicine. Module yake ilivyowekwa siyo sawa na bachelor za kawaida. Amo akitaka kusoma master of medicine ni lazima akasome md kwanza.
 
Kuna ambao wanachukua diploma halafu advanced diploma halafu post graduate/masters..sasa hawa si madoctor kwasababu hawakuchukua medical doctor (MD)?
Doctor ni mtu yeyote ambae ana diagnose na ana treate, ACO,CO,AMO,MD..wote wana kazi nlizotaja

mkuu mtu aliyesoma ftc ni engineer? Au mtu aliyesoma certificate ya sheria ni hakimu/wakili?
 
ndio, kuna ambao wanachukua AMO za medicine na wengne AMO za immunology, parasitology..kama kuna mtu anaesoma AMO muhimbili ungejaribu kumuuliza kuhusu hili

ni lazima awe amo kwanza aafu anaenda kusomea kile anachokitaka lakini siyo kwa level ya masters. Hiyo ni postgraduate diploma kama sijakosea. Pia muhimbili hakuna amo mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…