Wenye Mamlaka nchini Tanzania mnatuhangaisha mno Wananchi wenu hasa kuhusu Uvaaji wa Mask na CORONA

Wenye Mamlaka nchini Tanzania mnatuhangaisha mno Wananchi wenu hasa kuhusu Uvaaji wa Mask na CORONA

Mzukulu

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2020
Posts
1,401
Reaction score
2,641
Kuna Tangazo la Redioni nalisikia karibu katika Redio zote Kubwa nchini ambalo linatoka katika Mamlaka husika linasema kuwa Uvaaji wa Barakoa ( Masks ) ni kwale Walioathirika tu na Maambukizi ya COVID-19 na Wanaowahudumia na si kwa Watu wengine na kwamba wakifanya hivyo watakuwa wanajihatarishia Afya zao.

Hapo hapo tena tokea Juzi nimenza Kusikia Matamko kutoka kwa Watu wenye Dhamana za Kiuongozi ( Serikalini ) zikiwahimiza na kuwataka tena kwa Kuwalazimisha kabisa Watanzania kuwa wanatakiwa sasa Kuvaa hizo Barakoa ( Masks ) ili wajikinga na COVID-19. Na nimeona Mitandaoni na hata Kusikia na Kuona Runingani wengine wakitishiwa kuwa wasipozivaa basi watashtakiwa.

Tafadhali kama Watu ( Wakubwa ) wa Serikalini wapo hapa JamiiForums watusaidie kutuambia lipi ni Jambo sahihi na ni nani kwa sasa Sisi Watanzania tunapaswa tumsikilize kati ya Mtaalam wa Afya anayezuia Uvaaji wa Barakoa kwa asiyeathirika au Mwanasiasa anayetulazimisha tusivae ili tusife?
 
Sasa kma hujapimwa utajuaje kama umeathrika? Dawa ni kuweka sheria kila mtu avae maski

Sent using Jamii Forums mobile app

Mtaalam katika hilo Tangazo ambalo tena Mmoja wa Wadhamini wake ni Wizara ya Afya amesisitiza na Kuonya kuwa wanaotakiwa Kuvaa Barakoa ( Masks ) ni wale tu waliopatwa na Maambukizi na akaenda mbele hadi Kuelezea Kitaalam kabisa Madhara yake. Sasa leo hii Wewe Mwanasiasa au Mwananchi wa Kawaida sana kama Wewe mnatutaka tuzivae je, hapo hamuoni kuwa mnatuchanganya zaidi Watanzania na pengine hata Kutuumiza zaidi Kisaikolojia huku tukwa na hofu na CORONA?
 
Back
Top Bottom