Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 22,168
- 39,118
Huwa nasema timu za Kariakoo ni Kulwa na Doto na àmbao tulishafanikiwa kuvuka mitego ya siasa zake tuna Amani zaidi.
Miaka ya 1990 Simba walikuja na Nick name ya Simba TAIFA KUBWA na ikahit vibaya. Kaulimbiu ya TAIFA KUBWA iliwabeba Simba ndani na. nje ya nchi maana ni kipindi hiki walifika fainali ya Kombe la shirikisho na kukosa ubingwa chupu chupu mbele ya Stella Abidjan ya Ivory Coast wakiwa chini ya udhamini wa Mzee Azim Dewji. Pacha wake alipoona huyu anafaidi yeye akajiita Yanga UMOJA WA MATAIFA na shabiki wao mmoja akawalipia wakatungiwa wimbo wa YANGA AFRICA UMOJA WA MATAIFA na Marehemu Peppe Kalle baada ya kuchukua ubingwa wa klabu bingwa Afrika mashariki pale Kampala Uganda Kwa kuifunga Sports Club Villa wakiwa chini ya udhamini wa Marehemu Abbas Gulamali Mbunge wa Kilombero.
Miaka 4 Hadi 6 iliyopita Simba walikuwa wanajitambulisha kama Simba MNYAMA wakatoa kofia, mizula, khanga na baadhi ya mashabiki wakawa na logo za MNYAMA. Ni kipindi hicho cha ufalme wa Simba chini ya ufadhili wa Mohamed Dewji "Mo" Pacha wake alipokuwa Hoi kiuchumi na kuendesha timu Kwa michango ya Wanachama wake alipoibuka na kauli mbiu ya "TIMU YA WANANCHI, MWEKEZAJI NI MWANANCHI". Mashabiki waliokuwa wanachangia timu wakaitwa "WANANCHI". Jambo hili likawa kubwa na likamvuta GSM kuwekeza baada ya kuona Fan base kubwa na hamasa ya kishabiki inavutia uwekezaji kwani angefanikiwa kutangaza na kuuza bidhaa zake kupitia nembo ya WANANCHI.
Kama ilivyo ada, Jana Pacha kajibadili naye kaamua kutumia slogan inayoendana na hiyo. Yeye anajiita MWENYE NCHI. Yaani kama wewe ni Mwananchi basi Mimi ni Mwenye nchi. Wanaojua kupima watapima na kuona faida na hasara za kudandia Slogan Tangu kipindi cha TAIFA KUBWA vs UMOJA WA MATAIFA Hadi Sasa MWANANCHI vs MWENYE NCHI.
Miaka ya 1990 Simba walikuja na Nick name ya Simba TAIFA KUBWA na ikahit vibaya. Kaulimbiu ya TAIFA KUBWA iliwabeba Simba ndani na. nje ya nchi maana ni kipindi hiki walifika fainali ya Kombe la shirikisho na kukosa ubingwa chupu chupu mbele ya Stella Abidjan ya Ivory Coast wakiwa chini ya udhamini wa Mzee Azim Dewji. Pacha wake alipoona huyu anafaidi yeye akajiita Yanga UMOJA WA MATAIFA na shabiki wao mmoja akawalipia wakatungiwa wimbo wa YANGA AFRICA UMOJA WA MATAIFA na Marehemu Peppe Kalle baada ya kuchukua ubingwa wa klabu bingwa Afrika mashariki pale Kampala Uganda Kwa kuifunga Sports Club Villa wakiwa chini ya udhamini wa Marehemu Abbas Gulamali Mbunge wa Kilombero.
Miaka 4 Hadi 6 iliyopita Simba walikuwa wanajitambulisha kama Simba MNYAMA wakatoa kofia, mizula, khanga na baadhi ya mashabiki wakawa na logo za MNYAMA. Ni kipindi hicho cha ufalme wa Simba chini ya ufadhili wa Mohamed Dewji "Mo" Pacha wake alipokuwa Hoi kiuchumi na kuendesha timu Kwa michango ya Wanachama wake alipoibuka na kauli mbiu ya "TIMU YA WANANCHI, MWEKEZAJI NI MWANANCHI". Mashabiki waliokuwa wanachangia timu wakaitwa "WANANCHI". Jambo hili likawa kubwa na likamvuta GSM kuwekeza baada ya kuona Fan base kubwa na hamasa ya kishabiki inavutia uwekezaji kwani angefanikiwa kutangaza na kuuza bidhaa zake kupitia nembo ya WANANCHI.
Kama ilivyo ada, Jana Pacha kajibadili naye kaamua kutumia slogan inayoendana na hiyo. Yeye anajiita MWENYE NCHI. Yaani kama wewe ni Mwananchi basi Mimi ni Mwenye nchi. Wanaojua kupima watapima na kuona faida na hasara za kudandia Slogan Tangu kipindi cha TAIFA KUBWA vs UMOJA WA MATAIFA Hadi Sasa MWANANCHI vs MWENYE NCHI.