Wenye Nyumba kaeni kitaalamu: Kama mpangaji wako atakutwa na dawa za kulevya nyumba yako itataifishwa!

Lyimo nadhani ameikuta hiyo sheria. Sijui kanuni zake zipoje.
Njuavyo, mahakama inapaswa kujiridhisha pasi na shaka kuwa anayeadhibiwa ni yule anayehusika na kosa.
Kirahisirahisi mtu ajipatie canter, ghorofa, n.k kisha mkodishaji alipakia unga
 
Viongozi wengi wa serikali uwezo wao wa kufikiri ni mdogo sana , sasa badala ya kutafuta mbinu za kisasa kupambana na hili la madawa wao wanatafuta wepesi wa kazi kupitia wenye nyumba ,

akili ya hovyo sana sasa mimi mwenye nyumba najuaje kama aliye panga ni muuza dawa wakati hilo ni jambo linafanywa kwa usiri mkubwa , hawq ma zero brain waliopo serikalini waache kutunga sheria za hovyo kuwarahizishia kazi wao huku wakiumiza watu wasio na hatia ,
 
Ile kauli ya Assad kwamba serikalini kumejaa vilaza ilikuwa kweli kwa asilimia mia
Ni muda sasa wa kuwakataa wajinga na sheria za kijinga.
 
Hilo ni tamko, sio sheria, na ndio maana Africa kuendelea ni shida sana, kumejaa matamko kede kede.
Shida ya matamko ni kuwa yanarudisha nyuma maendeleao, mfano kwa tamko hili watu waneza wasitamani tena kujenga nyumba za kupangisha, maana ni risk kama tu kununua gari la biashara.
 
Huyo kijana amenukuu hicho kifungu cha sheria? Au maneno tu. Ndio maana serkali yetu inaingia kesi ambazo itashindwa huko mbele na kulipa gharama kubwa.
Kwani sheria za upangaji zinasema ukipangisha mtu unaingilia faragha zake?
Mahakama ndio inaweza kutofasri hiyo sheria feki na nitashangaa kweli kama ipo
 
Je itakuwaje kama mpangaji wa shirika la nyumba la taifa NHC mpangaji wake akakutwa na bange
 
Kwa sheria hii watu watakomolewa kwa kuwekewa mihadarati kwenye nyumba zao, ukute huwa hulimi nyasi kwenye nyumba yako utakuta umeoteshewa miche ya bangi au mirungi inakua bila wewe kujua, mwisho utabambuliwa kuwa unalima bangi na mirungi
 
Low level of thinking. Kwa upelelezi huu usiofata sheria na kuoneana, kuna watu watakuwa target na watu watadhulumiwa sana mali zao
 
Ukisha mpangisha mtu nyumba Ina maana tayali hiyo nyumba niyakwake kwa mda alio lipia

Huwezi kuingia chumbani kwake kumchunguza tena

Hivyo utaratibu huo haukubaliki
 
Hawa wapuuzi kuna wakati wanalewa madaraka na kuropoka ovyo kama watu waliokula madawa ya kulevya. Huyo aliyetamka hayo maneno inawezekana naye amelewa madawa ya kulevya. Akamatwe apimwi madawa mwilini mwake.
 
kweli!? ndio tulikofika? hii hapana
yaani nimpanishe kijana chumba kimoja halafu polisi wamkamate na bangi kisha wachukue nyumba?
awapi!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…