Wenye nyumba wana nafuu kuliko wapangaji jijini

DarProperty Tz

Senior Member
Joined
Apr 24, 2011
Posts
168
Reaction score
29
Watanzania wanaonunua nyumba kwa mikopo ya nyumba kutoka kwenyye taasisi za mikopo wanaokoa mpaka Tsh. 51,336,000 (USD 18600) kwa mwaka tofauti na wanaoamua kupanga.

Marejesho ya mkopo wa nyumba ya makazi ni nafuu kulinganisha na kodi ya nyumba ya kupanga katika maeneo ya jirani na jiji. Kwa wastani marejesho ni Tsh. 2,052,000 (USD 950) kwa mwezi kulinganisha na kodi ya nyumba vinne ambayo kwa kawaida hufika Tsh. 5,400,000 (USD 2500) kwa mwezi.

Kusoma makala yote kwa lugha ya kiingereza tembelea..

DarProperty >> Read Article
 
ngoja nifuate link ili nikuongezee traffic kwenye site yako.
 
Marejesho ya wastani wa mil 2,052,000/=kwa mwezi na bado unamwitahuyo mtu Mtanzania wa kawaida?
Hivi nyie Watanzania wa kawaida mnawajua kweli???!!!
 
Mtu anaeweza kupanga nyumba kwa $2500 kwa mwezi wala haitaji mkopo wa nyumba. Aidha ananunua cash au anajenga ndani ya muda mfupi.
 
Mnaongelea watanzania wapi? Watanzania wengi kodi zinaanzia 40,000 mpaka laki 8 kwa mwezi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…