Wenye ugonjwa wa(GERD )Gastoesofphagas reflux deases naomba tukitane Happ tujadiliane tafadhali.

Daah aise.. Naomba unitag na mm mkuu... Ninia mwaka sasa nasumbuliwa na tatizo hilo
 
Kuna aina za dawa zinajulikana kama PPI mfano omeprazole, lansoprazole, pantoprazole, rabeprazole au zinginezo, ushawai tumia hizo?
Zinasaidia sana kama unatumia kwa muda unaotakiwa. Pia hazina madhara kwa matumizi ya muda mrefu (kwa ninavyofahamu).

Tumia aina ya vyakula ambavyo havina acid (au havisababishi ongezeko la acidity tumboni). Mfano epuka vyakula vya kukaanga na viungo vingi hasa mda wa jioni.

Uwe una kula kwa muda, hasa chakula cha jioni. Namaanisha ule mapema jioni.

Tumia mtoo wakati wa kulala. 'Elevate' kichwa vya kutosha(ila angalia usiumize shingo na mgongo). Hiyo itasaidia kuzuia 'reflux'.

Nawasilisha mawazo yangu
 
We ni me au ke na ushawahi tumia hizo dawa. Nijibu halafu nikueleze kitu kwa experience
 
Jamani mm ninashida ya huu ugonjwa naomba msaada was mawazo na ushauri ili niweze kurelux nao maana naona Hali yangu sio nzuri.
Weka kiswahili inawezekana tunao hatujui
 
You Nailed it bro..
Mm nina huu ugonjwa mwaka wa 9 sasa, Na ninakwepa kula baadhi ya vitu, na ndio pona yangu..
naweza umwa mara 2 au 1 kwa mwez na natumia omeprazole na Riflux ant acid...

sana sana epuka vyakula vinavyomengenywa kirahisi na venye acid kubwa ndan yake.

Bia tu ndio nimeshindwa kuacha kabisa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
 
Yaani acid inapanda juu kutoka tumboni hadi muda mwingine inafika kwenye koromeo, inapandaje ndio kuna sababu nyingi, inatoka wapi pia kuna sababu nyingi,

Ehee ulinitesa sana huo ugonjwa nikiwa mjamzito pole kwa wanaoumwa aisee...muda wote Rabeloc ilikua haiishi kwenye mkoba wangu.
 
Wakuu ebu wekeni hata picha ili nasisi wa huku Ushirombo ndanindani tuelewe.....
Maana naona hapa mnaelezana kwa lugha ya bepari tu...[emoji30][emoji30][emoji30][emoji30]
 
Kwann unalemba jina la ugonjwa wako. Si useme tu kwa kiswahili kma ni utapiamlo au mdondo tuelewe tu. Kuumwa uumwe wewe alfu urembe jina la ugonjwa. Tutakusaidiaje sasa.
 
😁😁😁 unaweza kukuta mtu anao huo ugonjwa na alitibiwa, ila kwa jina uliloweka hapo anaweza asijue nini unamaanisha
 
Kiungilia kina kuwa hivi ukicheuwa unacheuwa kitu kichungu na tumbo kujaa gasi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…