Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Haya.. mapumziko time!
Wewe unataka hiki, naye anataka kile,
Mkononi unachaki, ubao wake ni ule,
Mwaitana marafiki, tangu nyie mko shule,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mwaringiana?
Wajua anakitaka, anajua wakitaka,
Wote mwajua mwataka, mmebaki na mashaka,
Mmebaki na dhihaka, na kicheko mnacheka,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnazungushana?
Cha kwake unakipenda, cha kwako anakipenda,
Sasa wote mmekonda, zinawadondoka denda,
Kwa wenzako wamponda, kwa wenzake akuponda,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnategeana?
Usiku unapolala, ndotoni unakiota,
Naye anashindwa kula, kutwa anaona nyota,
Wawacheka wenye hila, kwa jinsi mnavyosota,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnaumizana?
Unasubiri aombe, anasubiri uombe
Sasa mmeota pembe, za kiburi na kimbembe,
Ati hutaki atambe, naye hivyo hivyo kumbe,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnangojeana?
Sasa nenda utamke, uwe wa kwanza kunena,
Fanya hima mualike, hilo ungefanya jana,
Cha kwako ukipeleke, anakungoja kijana,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mwachelewashana?
Umpe kilichojaa, si kibaba bali pishi,
Umpe kama kichaa, mfike Kapirimposhi
Na umpe kwa ridhaa, akupe bila ubishi,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mwakodoleana?
Ushauri nawapeni, msipende kutegana,
Mkitaka peaneni, vile mnavyoombana,
Msinyimane jamani, ni vizuri kugawana,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnakubaliana?
Wewe unayo sukari, na yeye ana kikombe
shirikianeni kutengeneza chai..
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Wewe unataka hiki, naye anataka kile,
Mkononi unachaki, ubao wake ni ule,
Mwaitana marafiki, tangu nyie mko shule,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mwaringiana?
Wajua anakitaka, anajua wakitaka,
Wote mwajua mwataka, mmebaki na mashaka,
Mmebaki na dhihaka, na kicheko mnacheka,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnazungushana?
Cha kwake unakipenda, cha kwako anakipenda,
Sasa wote mmekonda, zinawadondoka denda,
Kwa wenzako wamponda, kwa wenzake akuponda,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnategeana?
Usiku unapolala, ndotoni unakiota,
Naye anashindwa kula, kutwa anaona nyota,
Wawacheka wenye hila, kwa jinsi mnavyosota,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnaumizana?
Unasubiri aombe, anasubiri uombe
Sasa mmeota pembe, za kiburi na kimbembe,
Ati hutaki atambe, naye hivyo hivyo kumbe,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnangojeana?
Sasa nenda utamke, uwe wa kwanza kunena,
Fanya hima mualike, hilo ungefanya jana,
Cha kwako ukipeleke, anakungoja kijana,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mwachelewashana?
Umpe kilichojaa, si kibaba bali pishi,
Umpe kama kichaa, mfike Kapirimposhi
Na umpe kwa ridhaa, akupe bila ubishi,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mwakodoleana?
Ushauri nawapeni, msipende kutegana,
Mkitaka peaneni, vile mnavyoombana,
Msinyimane jamani, ni vizuri kugawana,
Ulichonacho ataka, alichonacho wataka
Mbona mnakubaliana?
Wewe unayo sukari, na yeye ana kikombe
shirikianeni kutengeneza chai..
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Last edited by a moderator: