WFP: Wakimbizi wengi wa Msumbiji wanakimbilia Tanzania kutikana na mapigano kuongezeka

WFP: Wakimbizi wengi wa Msumbiji wanakimbilia Tanzania kutikana na mapigano kuongezeka

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Kaskazini mwa Msumbiji, mapigano yanaendelea na kuongezeka hali ambayo imelazimisha maelfu ya watu kutoroka makazi yao.

Sasa hivi idadi kubwa ya raia hao wanakimbilia nchi jirani ya Tanzania kulingana na mkurugenzi wa Shirika la Chakula Duniani eneo la Kusini mwa Afrika alipozungumza na BBC.

Makadirio kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa na wadau wengine ni kwamba idadi ya kundi hilo la wakimbizi ni karibu watu 1000.

Aidha kulingana na Shirika la Chakula Duniani, sasa hivi serikali ya Tanzania ndio inayosimamia mahitaji ya kundi la wakimbizi walioingia nchini humo kutoka Msumbiji hivi majuzi.

Pia kuna taarifa kwamba unyanyasaji wa haki za binadamu katika eneo la Cabo Delgado umekuwa ukiongezeka huku mapigano kati ya wanamgambo wa Kiislamu na vikosi vya serikali yakiendelea.
Mpaka kati ya Msumbiji na Tanzania ni mto Ruvuma, na eneo la pwani ya bahari.

Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, Msumbiji imeshuhudiwa idadi kubwa ya watu wakilazimika kutoroka makazi yao hasa katika mkoa wa Cabo Delgado huku wengine wakielekea eneo la kusini la Nampula, amesema mkurugenzi wa WFP.

Kulingana na Lola Castro mkurugenzi wa Shirika la Chakula Duniani eneo la Kusini mwa Afrika, wiki kadhaa zilizopita Shirika hilo lilipata taarifa kwamba kulikuwa na kundi la watu lililovuka mpaka kutoka mto Ruvuma na kuingia eneo la Mtwara nchini Tanzania.

Inasemekana kwamba baadhi ya watu walitumia boti huku wengine wakiogolea katika mto Ruvuma kuingia nchini Tanzania.

''Usafiri ulizoeleka katika mto Ruvuma ni mtumbwi pia wanavuka kwa kutumia boti hadi visiwani eneo la delta la Msumbiji na Tanzania,'' amesema Lola Castro.
 
Kaskazini mwa Msumbiji, mapigano yanaendelea na kuongezeka hali ambayo imelazimisha maelfu ya watu kutoroka makazi yao.

Sasa hivi idadi kubwa ya raia hao wanakimbilia nchi jirani ya Tanzania kulingana na mkurugenzi wa Shirika la Chakula Duniani eneo la Kusini mwa Afrika alipozungumza na BBC.

Makadirio kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa na wadau wengine ni kwamba idadi ya kundi hilo la wakimbizi ni karibu watu 1000.

Aidha kulingana na Shirika la Chakula Duniani, sasa hivi serikali ya Tanzania ndio inayosimamia mahitaji ya kundi la wakimbizi walioingia nchini humo kutoka Msumbiji hivi majuzi.

Pia kuna taarifa kwamba unyanyasaji wa haki za binadamu katika eneo la Cabo Delgado umekuwa ukiongezeka huku mapigano kati ya wanamgambo wa Kiislamu na vikosi vya serikali yakiendelea.
Mpaka kati ya Msumbiji na Tanzania ni mto Ruvuma, na eneo la pwani ya bahari.

Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, Msumbiji imeshuhudiwa idadi kubwa ya watu wakilazimika kutoroka makazi yao hasa katika mkoa wa Cabo Delgado huku wengine wakielekea eneo la kusini la Nampula, amesema mkurugenzi wa WFP.

Kulingana na Lola Castro mkurugenzi wa Shirika la Chakula Duniani eneo la Kusini mwa Afrika, wiki kadhaa zilizopita Shirika hilo lilipata taarifa kwamba kulikuwa na kundi la watu lililovuka mpaka kutoka mto Ruvuma na kuingia eneo la Mtwara nchini Tanzania.

Inasemekana kwamba baadhi ya watu walitumia boti huku wengine wakiogolea katika mto Ruvuma kuingia nchini Tanzania.

''Usafiri ulizoeleka katika mto Ruvuma ni mtumbwi pia wanavuka kwa kutumia boti hadi visiwani eneo la delta la Msumbiji na Tanzania,'' amesema Lola Castro.
Miss Zomboko Nakupenda sana sijawahi kusoma habari za hovyo kutoka kwako, inaonekana ni Mtu makini sana. Kongole kwako
 
Mabeberu wapo kwenye majaribio, mungu iepushe pwani ya afrika mashariki, maana imebaki tz tu
 
Taizo hata wafanyakazi wa WFP sio wa kuamini sana - nao upenda penda sana kupalulia masuala ya ukimbizi ili waendelee na ajira zao - kumbuka walivyo kuwa wanawashurutisha wakimbizi wa Burundi wasirudi kwao, tukirudi kuhusu masualavya ugaidi kaskazini mwa Msumbuji cha muhimu hapa Taifa letu liwe makini na nyenendo za kudi hilo linaweza kuwa linatumiwa na Mataifa ya magharibi kuchochea vurugu katika kanda zenye utajiri mkubwa wa Mali asili - hicho ndicho kinaendelea nyuma ya pazia, hakuna cha kuwasingizia waislaam wenye itikadi kali wala nini sijui?
 
Tuilinde amani yetu na sisi yasijetukita haya ya kuogelea kwenda nchi nyingine.
 
Back
Top Bottom