What happened to Julius Nyerere Airport?

What happened to Julius Nyerere Airport?

menny terry

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2011
Posts
509
Reaction score
670
Wakuu,

Nimetembelea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Airport kwakweli ni mzuri mno na unavutia sana sana hususani Terminal 3.

Ujenzi wake umebadilisha kabisa muonekano wa uwanja mzima na kuufanya uwe wa kimataifa haswa. Kwa hilo naipongeza sana serekali yetu.

Lakini najiuliza why idadi ya ndege za kimataifa na wageni ni ndogo sana? Yaani terminal 2 ndo angalau iko busy. Tatizo liko wapi?

Yaani hata ule wa Zanzibar unatupita aisee? Idadi ya wageni kule Zanzibar ni kubwa kuliko Bara kwanini? Hapo wala sijataka kuitaja Jomo Kenyatta International Airport.

Nini kifanyike wadau? Kwa muda niliyo kaa pale kusubiri wageni wangu ndege zilizo shusha wageni ni mbili tu Rwanda Air na Ethiopian Airlines.

Nawasilisha.
 
labda wale wageni tuliowapata wengi kutokana na ile Filamu wanapitia pengine (huko ambapo wageni wanatuzidi)
 
Naomba kujua terminal 2 na one zinatua ndege gani

Terminal 2 zinatua ndege za ndani tu kwa mfano Air Tanzania pamoja na Presicion Air wakati Terminal one zinatua zile ndege ndogo kabosa kama Auric Air .
 
Kuna mtu alitaka kunitembelea kutoka inje,
Jana kanihoji kuhusu panya road na akanambia anaogopa!!
Kiukweli nilishangaa sana kuwa amesikia wapi??
🤣🤣🤣Aliwaitaje Sasa kwa kizungu?
 
Umeasahau kwamba haya ni majira ya Covid-19, si watu wengi wala mashirika mengi yanayokuja Afrika...

Pia inategemea wewe umeenda muda na siku gani, sababu kuna wakati huwa ni busy hour hapo T3, kiasi kwamba hadi hiyo sehemu ya departure huonekana haitoshi...
 
Umeasahau kwamba haya ni majira ya Covid-19, si watu wengi wala mashirika mengi yanayokuja Afrika...

Pia inategemea wewe umeenda muda na siku gani, sababu kuna wakati huwa ni busy hour hapo T3, kiasi kwamba hadi hiyo sehemu ya departure huonekana haitoshi...

Thanks mkuu.
 
Back
Top Bottom