Moja kati ya swali ninalolichukia toka kwa mwajiri ni "What is your salary expectation ?"
Huwa najiuliza kwanini mwajiri aniulize hivi wakati tayari ana scale yake kashaiandaa kwa position husika
Ni ngumu sana kumshawishi mwajiri aliepanga kukulipa 1,000,000 basic salary kisha akulipe 1,500,000 mana unakua uko nje ya bajeti yake.
Hili swali huwaga naona kama limekaa kimtego flani hivi, utaje kiasi kidogo ujipunje mwenyewe au utaje kiasi kikubwa mwajiri akuone kama una tamaa.
Binafsi nilikua naonelea ni bora waajiri kwenye kampuni binafsi wangekua wanafanya kama serikali kwamba tangazo la ajira linapotoka wanaweka scale ya mshahara kwa kila position kulingana na level yako ya elimu.
Mfano kampuni inahitaji ICT Officer, Operation Manager, Accountant n.k sio mbaya wangekua wanaweka wazi kiasi cha mshahara kwa kila post ili muombaji awe anajua kabisa kwamba hii kazi naaplai lakini malipo yake ni kiasi flani na kwa kufanya hivi watakua wanawapata watu ambao tayari washakubaliana na kiasi cha mshahara kilichopangwa hata kabla ya kufanya usaili.
Mana kuna muombaji mwingine wa ajira anatuma maombi kisha anaitwa kwenye usaili na kupata kazi lakini akija kutajiwa kiasi cha mshahara atakacholipwa anakua hayupo tayari kusaini mkataba mana inakua kinyume na matarajio yake.
Mtu alitegemea kulipwa 1,500,000 kama basic salary kisha unakuja kumtajia 700,000 kama basic kiukweli hawezi kukuelewa
Am done
Huwa najiuliza kwanini mwajiri aniulize hivi wakati tayari ana scale yake kashaiandaa kwa position husika
Ni ngumu sana kumshawishi mwajiri aliepanga kukulipa 1,000,000 basic salary kisha akulipe 1,500,000 mana unakua uko nje ya bajeti yake.
Hili swali huwaga naona kama limekaa kimtego flani hivi, utaje kiasi kidogo ujipunje mwenyewe au utaje kiasi kikubwa mwajiri akuone kama una tamaa.
Binafsi nilikua naonelea ni bora waajiri kwenye kampuni binafsi wangekua wanafanya kama serikali kwamba tangazo la ajira linapotoka wanaweka scale ya mshahara kwa kila position kulingana na level yako ya elimu.
Mfano kampuni inahitaji ICT Officer, Operation Manager, Accountant n.k sio mbaya wangekua wanaweka wazi kiasi cha mshahara kwa kila post ili muombaji awe anajua kabisa kwamba hii kazi naaplai lakini malipo yake ni kiasi flani na kwa kufanya hivi watakua wanawapata watu ambao tayari washakubaliana na kiasi cha mshahara kilichopangwa hata kabla ya kufanya usaili.
Mana kuna muombaji mwingine wa ajira anatuma maombi kisha anaitwa kwenye usaili na kupata kazi lakini akija kutajiwa kiasi cha mshahara atakacholipwa anakua hayupo tayari kusaini mkataba mana inakua kinyume na matarajio yake.
Mtu alitegemea kulipwa 1,500,000 kama basic salary kisha unakuja kumtajia 700,000 kama basic kiukweli hawezi kukuelewa
Am done