What Is Your Strategy?

TF mikakati yangu iko zaidi kwenye kutunza ndoa yangu na kwenye uchumba sikutumia nguvu nyingi maana nilijua ni kitu cha muda
Ila muda wangu mwingi nautumia kuhakikisha kuwa naitunza ndoa yangu
Kwahiyo Rocky kwenye uchumba haina haja ya kuwa na strategic plan yenye nguvu nyingi??
 
finest naona ukwepaji wa maswali kwa rocky ngoja tusimbane tusijetafutiwa RB

Unajua BPM ndoa ni raha ukiipatia na ukiielewa na ukiwa na mtu ambaye anakuelewa
Ni raha kama mtakuwa mnaenda kwenye the same target na kama mna nia ya kulifikisha gari lenu kwenye the same destination
Huwa hutumii nguvu nyingi kukuhakikishia kupendwa wala hutumii resources nyingi kukuhakikishia ndoa yako inadumu
just maneno matamu na vitendo kiasi
na hata kama vitendo vinaambatana na zawadi kidogo huwa ndoa unaiona raha yake
tatizo ni pale unapotumia nguvu nyingi kutafuta kupendwa wakati pendo lenyewe halipo au kutumia resources zako ntingi kutafuta kupendwa wakati ushapoteza upendo huo zamani
 
Kwahiyo Rocky kwenye uchumba haina haja ya kuwa na strategic plan yenye nguvu nyingi??

Kuwa na plan ila usitumie nguvu nyingi kumaintain upendo
Kama halipo ni kwamba hata ulipake asali na mafuta halipo tuu TF
Utajitahidi weee kuupendezesha mbuyu kwa mategemeo kuwa utaupasua mbao ila matokeo yake utapata mti wenye nyizi nyuzi tuu haufai kwa mbao
 
I wonder what goes in The Finest mind his topic are always very challenging
 
Mkuu naomba unifafanulie hapo kidogo
 

naamini mikakati mikubwa ambayo naamini mkuu inatakiwa iwepo ni kama
  1. kusikilizana
  2. kusameheana
  3. kuelewana
  4. kushauliana
  5. kuridhishana
etc
 
Mkuu naomba unifafanulie hapo kidogo

Unajua tunatumia nguvu nyingi na resources nyingi sana wakakti wa uchumba yaani unajikuta mwanaume unajikamua balaa kuhakikisha kuwa kila anachohitaji mchumba apate
Wakati mwingine hatuna mategemeo kama huyo huyo mchumba ndio atakuwa mke maana wengine wanaishia kuja kuoa watu ambao hawakuwahi kuwatamkia kuwa wataishi pamoja
So ni better kuwa macho kujua kuwa je hizi nguvu na resources ninazotumia kwa huyu mtu je ni za real life au ni life la mpito
 
naamini mikakati mikubwa ambayo naamini mkuu inatakiwa iwepo ni kama
  1. kusikilizana
  2. kusameheana
  3. kuelewana
  4. kushauliana
  5. kuridhishana
etc

Ongezea na uvumilivu
na kuwa na roho ya Mungu katika kila mnalolifanya
 
Umeona eehhh
tena weekend kama leo unaleta topic ngumu hivi


tena weekend inakuwa ni sahihi kwani unatakiwa ukitoka hapa mmu unaenda kurekebisha kwani kuna mambo utakuwa umeyapata
 
Not having Strategy is Strategy as well au nikisema hivyo nitakuwa nakosea
 

huwezi kuwa na plan bila utekelezaji na utekelezaji ni nguvu na muda
 
tena weekend inakuwa ni sahihi kwani unatakiwa ukitoka hapa mmu unaenda kurekebisha kwani kuna mambo utakuwa umeyapata

haya mkuu ila sasa kujibu maswali yake inakuwa issue ni magumu mno
 
Aisee!!! Kuna kitu umenikumbusha hapo, halafu hivi inawezekana Strategy yako ikaangukia kwa wrong person
 
huwezi kuwa na plan bila utekelezaji na utekelezaji ni nguvu na muda

Sawa ila sio nguvu zako zote unaelekeza kwenye kuukumbatia mbuyu wakati u know kuwa hutaweza
 
...the road to the unknown!...



...mikakati aka strategies kwenye mapenzi hazi apply, unless kwa makusudi kabisa unajitafutia magonjwa ya mlipuko.
 
haya mkuu ila sasa kujibu maswali yake inakuwa issue ni magumu mno

si kila swali linahitaji majibu japo yanatakiwa yatolewe maelezo ili yaweze kuwa mwanaga kwa kile kinachotakiwa
 
...the road to the unknown!...



...mikakati aka strategies kwenye mapenzi hazi apply, unless kwa makusudi kabisa unajitafutia magonjwa ya mlipuko.
Kwahiyo mkuu in other words unamaanisha kwamba tukiwa kwenye mahusiano tusiwe na strategies zozote zile?
 
Reactions: Mbu
Sawa ila sio nguvu zako zote unaelekeza kwenye kuukumbatia mbuyu wakati u know kuwa hutaweza

lakini elewa unapoanza utakuwa uko gizani .. kawaida unapokuwa karib na mwenza kuna mambo mengi utayabaini kwa hiyo hutatambua hadi uwe na hicho kitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…