Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la afya duniani (WHO), Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema kwamba corona inaweza kuisha mwishoni mwa mwaka huu iwapo nchi zote duniania zitachukua hatua kabambe za kukabiliana na maambukizi.
Kiongozi huyo wa WHO alilkuwa akizungumza kakitaka kikao cha 150 cha shirika hilo la afya duniani cha kamati kuu kilichofanyika mjini Geneva. Akizungumza katika mkutano huo , Tetros alisema kuwa WHO inashirikiana katika ngazi za kikanda, kitaifa na kimataifa katika juhudi za kuutokomeza ugonjwa Covid.
Alisema kwamba shirika lake limekuwa likitoa raslimali, mikakati, na ujuzi wa kiufundi unaohitajika katika kudhibiti corona kwa nchi husika.
Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus alisisitizia haja ya kujifunza kutokana na corona na kubuni suluhu moya katika kukabiliana na hali za mzozo zinapojitokeza.
BBC Swahili
Kiongozi huyo wa WHO alilkuwa akizungumza kakitaka kikao cha 150 cha shirika hilo la afya duniani cha kamati kuu kilichofanyika mjini Geneva. Akizungumza katika mkutano huo , Tetros alisema kuwa WHO inashirikiana katika ngazi za kikanda, kitaifa na kimataifa katika juhudi za kuutokomeza ugonjwa Covid.
Alisema kwamba shirika lake limekuwa likitoa raslimali, mikakati, na ujuzi wa kiufundi unaohitajika katika kudhibiti corona kwa nchi husika.
Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus alisisitizia haja ya kujifunza kutokana na corona na kubuni suluhu moya katika kukabiliana na hali za mzozo zinapojitokeza.
BBC Swahili