Who is the best rapper, and who is the most recognized legend kati ya Profesa Jay na Mr II/SUGU!?

Who is the best rapper, and who is the most recognized legend kati ya Profesa Jay na Mr II/SUGU!?

Joined
Apr 23, 2012
Posts
76
Reaction score
71
Who is the best rapper, and who is the most recognized legend kati ya Profesa Jay na Mr II/SUGU!?

.., Joseph Haule 'Profesa Jay' na Joseph Mbilinyi 'Mr II/SUGU'.., wote ni rapa wa muziki wa Hip-hop, waandishi, watunzi, waasisi wa muziki, wakongwe na wanamuziki bora sana kuwahi kutokea kwenye kizazi cha muziki wa Bongo Flava/Hip hop...

Joseph Haule' Profesa Jay' amezaliwa 29 December 1975 (ana miaka 40 sasa) huko Ruvuma, Songea, Joseph Mbilinyi 'SUGU' amezaliwa 1 May 1972 (ana miaka 44 sasa) huko Mtwara, lakini ni mwenyeji wa mkoa wa Ruvumq, Songea..

Profesa Jay kaanza kufanya muziki mwaka 1993.., SUGU kaanza kufanya muziki 1990.. (wote ni moja kati ya mizizi ya muziki wa Bongo flava)

Wote hawa sasa ni viongozi wa umma, watumishi wa watu katika siasa, Profesa Jay anaongoza jimbo la Mikumi, Morogoro, Mr II anaongoza jimbo la Mbeya-Mjini (awamu ya 2).., wote wanatoka CHADEMA

Hapo awali wote waliwahi kutumia majina kadhaa kabla ya kubadilisha na kufikia kwenye majina waliyonayo sasa.., awali SUGU aliwahi kujiita Mr II, pia aliwahi kujiita 2 Proud.., Profesa Jay aliwahi kujiita Nigga Jay..,

Inawezekana SUGU akawa ndiye msanii wa muziki wa HipHop mwenye santuri nyingi...,hafi sasa ametoa santuri takribani tisa. Santuri hizi ni kama "Ni Mimi" iliyotoka mwaka 1995, Ndani ya Bongo (1996), Niite Mr II (1998), Nje ya Bongo (1999), Millennium (2000), Muziki na Maisha (2001), Itikadi (2002), SUGU (2004), Coming of Age-Ujio Wa Umri (2006) na VETO iliyotoka mwaka 2009.

Profesa Jay ana santuri kadhaa, ukiacha ile walitoa na Hard Blasters (Funga kazi)., zake binafsi ni 'Machozi, Jasho na Damu (2001)', 'mapinduzi halisi (2003)', J.O.S.E.P.H (2006), Aluta Continua (2007)

.., wanamuziki/wanasiasa hawa kwa nyakati tofauti, wamefanikiwa kuufanya muziki wa 'kizazi kipya' upate nguvu ya kusikilizwa na rika lote nchini, wametumia nguvu, muda, akili kufikisha muziki nje ya mipaka ya nchi nyakati hizo...

.., vibao vyote walivyowahi kuandika (Profesa Jay) na (SUGU/Mr II) ni vibao vikali, vyenye ujumbe, vyenye kuburudisha na vyenye kuishi muda mrefu kuliko vibao vingi vya wasanii wa sasa... nitajarajibu kutaja vibao kadhaa... (kila moja nitajaribu kutaja vibao vyake 14)

VIBAO 14 VYA PROFESA JAY..
1.Nikusaidiaje, 2.Zali la mentari, 3.Bongo Dar es Salaam, 4.Jina langu, 5.Ndio Mzee, 6.Msinitenge, 7.Hakuna noma, 8.Niamini, 9.sauti ya ghetto, 10.chemsha bongo, 11.Kipi sijasikia, 12.Piga Makofi, 13.UNA, 15.Kikao cha dharula.

VIBAO 15 VYA SUGU.
1.Hali Halisi, 2.Haki, 3.Hold on, 4.Chini ya miaka 18, 5.Hayakuwa mapenzi, 6.Mikononi mwa polisi, 7.Kiburi, 8.Siku nikianguka, 9.Wapi tunakwenda, 10.Nje ya Bongo, 11.Mambo ya fedha, 12.Deiwaka, 13.Freedom, 14.Far Dar es Salaam, 15.Mchakamchaka.

.., unafikiri nani anaweza kuwa bora kuzidi mwenzake kati ya 'Legends' hawa wawili wa muziki nchini kwetu..!?

Martin Maranja Masese,
Mwananchi wa kawaida.
 
Umeandika vzur sana mkuuu.

Mim kwa upenz wangu wa music na hits time zinazo bonga.

Prof hata leo ukipga ngoma zake watu wanaenjoy sana.


Ila Sugu watu wanaeza sio kwa sababu mziki mtamu ila labda wanakumbuka matukio wakihusianisha na mziki ukipigwa.

Prof namuelewa
 
Umeandika vizur sana, alafu huwaga siku zote Prof J anapoulizwa ni msanii gan bongo ambaye ni kama kioo chake? Jibu la husema Sugu,.. Kiukweli wametengeza historia nzur sana katka maisha yao
 
mi kwangu hao wote wawili nawakubali sana
 
Wote hao hakuna mwenye bars Nzuri, wala hawana style nyingi yani hawana versatility, Hakuna techniques kama wordplay, metaphors basic, rhymes zako very simple, walibahatika wakati Hakuna wasanii wengine, otherwise ni very average cats.
 
Wote hao hakuna mwenye bars Nzuri, wala hawana style nyingi yani hawana versatility, Hakuna techniques kama wordplay, metaphors basic, rhymes zako very simple, walibahatika wakati Hakuna wasanii wengine, otherwise ni very average cats.

Duuuuuiuuuuu
 
utapataje best rapper kwa kushindanisha rappers wawili tuu!!!hapo unatafta better than sio best!!!!,ili kupata best rappwr lazma ujumuisha legendary rappers wote km akna balozi,fid,msafiri kondo nk
 
Wananiita sugu wananiita sugu sugu sugu suguuuuu naupendaje sasa
 
Profesa Jay ni zaidi kwenye uandishi ingawa wote ni wakali, Sugu naweza kumpa heshima zaidi kwakuwa ndiye aliyefungua milango, kabla ya Sugu watu walikuwa wanarap rap tu mistari ya viingereza vya kukopi wamarekani, Sugu ndio msanii wa kwanza kuwa siriaz kurap mistari ya kiswahili na wengi kumuelewa
 
Wote hao hakuna mwenye bars Nzuri, wala hawana style nyingi yani hawana versatility, Hakuna techniques kama wordplay, metaphors basic, rhymes zako very simple, walibahatika wakati Hakuna wasanii wengine, otherwise ni very average cats.
We jamaa!!!
 
Wote hao hakuna mwenye bars Nzuri, wala hawana style nyingi yani hawana versatility, Hakuna techniques kama wordplay, metaphors basic, rhymes zako very simple, walibahatika wakati Hakuna wasanii wengine, otherwise ni very average cats.
Hakuna kama Sugu na Prof Jay, kurap mistari migumu haimaanishi we ndio mkali sana. Sugu na Prof wanadeliver msg kwa maneno ya kawaida yanayoeleweka kwa wanajamii, ukitumia ma 'panchaline' sana unataka nani akuelewe?
 
Kiundishi ProfJay mkali,ila kuufanya mziki wetu utambulike ndani na nje ya bongo,Sugu ana nafasi na umuhimu wake,ilani watu wanaoshabihiana sana,Sugu alikuwa anaufanya mziki waHip hop ujulikane,ila Prof alikuja kuifanya hiyokazi ya kuufanya mziki wa Hip Hop iwe rahisi,mi nakumbuka baba yangu naw ana miaka 62 alikuwa miakaya 2000 ukiweka nyimbo za Joseph Haule,hata kazini haendi tena,mpka leo huwa anamsikiliza nyimbo zake,ingawa kidogo Prof ameshuka sana kiundanishi,ila alitengeneza fan base kubwa sana ya wasikilizaji wa mziki wa Hip hop,wazee kwa watoto
 
Kiundishi ProfJay mkali,ila kuufanya mziki wetu utambulike ndani na nje ya bongo,Sugu ana nafasi na umuhimu wake,ilani watu wanaoshabihiana sana,Sugu alikuwa anaufanya mziki waHip hop ujulikane,ila Prof alikuja kuifanya hiyokazi ya kuufanya mziki wa Hip Hop iwe rahisi,mi nakumbuka baba yangu naw ana miaka 62 alikuwa miakaya 2000 ukiweka nyimbo za Joseph Haule,hata kazini haendi tena,mpka leo huwa anamsikiliza nyimbo zake,ingawa kidogo Prof ameshuka sana kiundanishi,ila alitengeneza fan base kubwa sana ya wasikilizaji wa mziki wa Hip hop,wazee kwa watoto
Sugu yeye alikuwa mkali kwenye suala la Hati miliki ndo maana zikawepo movement mbali mbali kama Bongo summit na Anti vrus kutetea maslahya mabwana mdogo wa baadae,akina Diamond leo mpaka wanalamba mamilioni
 
Hakuna kama Sugu na Prof Jay, kurap mistari migumu haimaanishi we ndio mkali sana. Sugu na Prof wanadeliver msg kwa maneno ya kawaida yanayoeleweka kwa wanajamii, ukitumia ma 'panchaline' sana unataka nani akuelewe?
Hujui maana ya punchline. Haimaanishi ni ngumu. Message ata babaako kakupa nyingi, 2Pac alikuwa anatoa message sana, lakini Kuna saa lazma uoneshe unaweza kucheza na clever rhymes, ndiyo hiphop.
 
Hujui maana ya punchline. Haimaanishi ni ngumu. Message ata babaako kakupa nyingi, 2Pac alikuwa anatoa message sana, lakini Kuna saa lazma uoneshe unaweza kucheza na clever rhymes, ndiyo hiphop.
Siyo kweli
 
Hujui maana ya punchline. Haimaanishi ni ngumu. Message ata babaako kakupa nyingi, 2Pac alikuwa anatoa message sana, lakini Kuna saa lazma uoneshe unaweza kucheza na clever rhymes, ndiyo hiphop.
Haya naomba nitajie wasanii wako bora wa Hiphop Tz
 
Back
Top Bottom