Uchaguzi 2020 Why Bernard Membe is not a presidential material, at all!

Kiukweli CCM ya leo siyo ile CCM yenye pesa nje nje mzee kabana
mkuu inasemekana wanaccm asili wanaona wametengwa na wapinzani wanapendelewa hasa. siri ya kina Sofia simba kuteuliwa kwenye nyadhifa serikalini ni jitihada za Magu kujaribu kuzima hizo lawama za chinichini.
 
Hii ni sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano...
 
Kwanza:Kama kuna mtu anatamani kuiepusha Tanzania kwa sasa na mwanzo mbaya wa VISASI anapashwa aje na ajenda ya katiba mpya, tunaponzwa na kuamini katika nguvu ya mtu badala ya nguvu ya Taasisi husika.
Pili: naichungulia Tanzania inayoanza kuwaza matumizi ya nguvu badala ya matumizi ya hoja
Tatu:Yanayotokea sasa yananikumbusha enzi za chama kimoja ambapo njama za mapinduzi ya serikari zilijitokeza Mara name, Tangu 1992 hakujawahi kuwa na njama hizo kalini nahisi hali hii imeanza kurudi katika mawazo wa watu
Mwisho: KATIBA NI SURUHISHO, naamini sasa hata akija malaika inawza kuwa ngumu kutawala kwa katiba hii
 
Nyalandu Vs Membe
wote wanajiita Majasusi wabobezi
tuone itakuaje
masikini mzee lowassa washamtupa kabaki kivuli na masalia
 
Wachunguzwe kwa kuwaza tofauti ma wewe?!
 
Benard Membe hawezi kusimama na John Magufuli hata kwa dakika 20. Kazi ya Magufuli inaonkena lakini ya Membe ni kusimulia/kujinadi zaidi, kila Mtu anaamini katika ishara na Vitendo sio rahisi kuwaaminisha Watanzania kwamba Membe anamzidi Magufuli sio rahisi!
 
Niaminishe hata kidogo mkuu, kuwa Membe ana nguvu kuliko alizokuwa naxo Lowassa ndani ya ccm, make huku kanda ya ziwa hata hatumjui, kma tulivyomjua Lowassa.
Nguvu ya Membe kufika 2020 itategemea sana matendo ya jiwe.Jiwe linaweza either kujimaliza or kujijenga pale tu litakapoanza kuwekeza katika ustawi wa jamii kifedha na si katika vitu kama lifanyavyo sasa!Any way muda ni mwalimu mzuri
 
Membe wanamtaka ili arudishe ufisadi Tanzania.

Lissu na Malim Seif wanawataka ili kuja kuvunja muungano na umoja wetu. Tanzania iwe Tanganyika dependent state na Zanzibar irejeshwe tena kwa Sultan wa Oman.
Ndio nyimbo za CCM hizi sio enzi za Marehemu KOMBA.
 
Hapana mkuu hapo nakupinga. Kwa kusema hivyo humtendei haki Rais wetu.

Nakubali maisha ya watu hayajabadilika sana zaidi ya kuwa watumishi wa serikali wananidhamu na kidogo hawajioni kama wao ni miungu wadogo na ofisi sio zao tena. Watu walio bahatika kuajiliwa kwenye ofisi, makampuni na mashirika ya umma walikuwa wanatumia ovyo sana nafasi na madaraka yao kwa kuwa nyanyasa watanzania wenzao.

Mfano; Nakumbuka siku za nyuma sana, dada yangu aliyekuwa anafanya kazi NPF wakati ule, alilia wiki nzima baada ya yeye kwa amri ya boss wake kumdhulumu baba wa watu mzee pension yake. Huyo mzee wakati ule, kulingana na maelezo ya dada yangu, ilikuwa apate shilingi elfu 21, kwa wakati ule ni hela nyingi sana, badala yake alipata shilingi elfu 13 tu.

Sasa kwa bahati mbaya au mzuri huyo dada yangu alimkuta huyo mzee kwenye ngazi za mlango wa kuingilia hiyo ofisi, wakati anarudi kutoka lunch mchana, machozi yakimtoka kwa kudhulumiwa hela zake ambazo mwenyewe alikwisha zipangia bajeti, labda ya kununua nyumba nakadhalika.

Dada yangu alikuwa mhasibu (book keeping). Alipo mwuuliza shida ni nini? Ndiyo akapata hiyo story. Ilimuuma sana.

Kwa hiyo mkuu kama wewe hukupata manyanyaso kama hayo kwenye serikali za awamu za nyuma basi inawezekana mwenzetu utakuwa aidha ndiyo mmojawao wa watendaji wa manyanyaso hayo au kwa uwezo na fursa uliyo kuwa nayo wakati huo, haikukubidi kuwa confronted na watumishi wa umma. Hiyo ilikuwa karibu kila sekta.


Na yeye aliwahi kusema kuwa kazi yake ni ngumu anajuta, CCM impumzishe tu Dr Magufuli.
Kwa hili hata mimi naona Rais hakustahili kusema hivyo. Kama yeye mwenyewe aliamua kuchukua form za kugombea urais hanabudi kulalamika. Kama kazi zina mhelemea basi ajiuzuru, lakini sio kuwakatisha tamaa viongozi wa kesho. Kama Pop anaweza kujiuzuru kwanini ishindikane kwa Rais?

Kwa kukupa matumaini tu mkuu, mimi binafsi nina uhakika Magufuli hakuwa chaguo la kwanza la Rais Kikwete na makada wa CCM, ila baada ya wao kuona Lowassa ameingia upinzani kwa kishindo, hapo nafikiri plan yao iliwatoka. Wakaona hatari iliyo kuwa mbele yao kama yeye angeshinda uchaguzi. Angelipiza kisasi, maana alikuwa na Bifu nao. Wangemkoma!

Katika kupiga mahesabu yao wakaona hawana budi kumteua mgombea ambaye kidogo wananchi wengi wanaimani yaye, ambaye ni Magufuli tu ili ku-neutralize hasira ambazo wananchi walizo kuwa nazo dhidi ya viongozi wa CCM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…