"Wife material" kindakindaki nina salamu zenu

"Wife material" kindakindaki nina salamu zenu

Sheillah Sheillah

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2020
Posts
653
Reaction score
1,698
Mume wako anakuambia mke wangu leo tutoke tukapate hata dinner nje, wewe unajidai wife material unamwambia mtapoteza hela bora mpike nyumbani. Siku nyingine anakuambia mtoke hata mkamwagilie moyo kidogo kama kawaida wife material unakataa unamwambia ni bora mnunue mmwagilie nyumbani.

Unamwambia ni matumizi mabaya ya pesa hiyo pesa ya kwenda dinner nje ni bora sijui mfanyie hivi au vile na hiyo pesa anayotaka mkapige maji ni bora muwatumie wazazi wenu.

Ukiiangalia kwa mbali inaonekana kama wewe una akili na ni wife material ambaye mwanaume yeyote anahitaji ,ofc ni wife material, na hautampoteza mume wako ila madhara yake ni makubwa.

Wewe haufikirii labda mumeo anataka mtoke ili awe na wewe nje ya mazingira ya nyumbani akuone vile ukivaa kimtoko mtoko unapendeza ( ukizingatia wengi tukiwa nyumbani ni madera tu). Yaani wewe haufikirii kwamba mume wako anahitaji huo muda kwa ajili yenu , mbali na kelele za watoto nk?

Basi juzi rafiki yangu kaenda Bar kumfumania mume wake na mchepuko wanakunywa mapombe na makange ya kuku huku wanafurahia live band. Mume pale pale kamwambia mkewe nikikuambia tutoke out hautaki wewe endelea kuwa mama wa nyumba maana hautaki kuiacha pekee yake.

Haya endeleeni kuwagomea wanaume zenu kutoka, kule kwenye bata kuna wadada wanaovizia wababa wanaokuja pekee yao, watakula hizo hela ulizokataa kuzila wewe.
 
images (1).jpeg


PambanaZaidi/CottonandMore
 
Sijawahi kuona Mke/Mpenzi akakataa Mtoko/Outings

Nimeanza kutoka na wife tukiwa Wachumba hadi Ndoa.

Na ukitaka akupee hadi uchoke Siku hiyo, mtoe out

Nafikiri ni jambo jema Kwa Wapenzi wapya hata Kwa Wana Ndoa.

Kuna wakati inafaa unamtoa out na mkalale hata nje ya Mji huko ili kupunguza msongo wa mawazo na kujaribu kuyachepua mapenzi yenu
 
Sijawahi kuona Mke/Mpenzi akakataa Mtoko/Outings

Nimeanza kutoka na wife tukiwa Wachumba hadi Ndoa.

Na ukitaka akupee hadi uchoke Siku hiyo, mtoe out

Nafikiri ni jambo jema Kwa Wapenzi wapya hata Kwa Wana Ndoa.

Kuna wakati inafaa unamtoa out na mkalale hata nje ya Mji huko ili kupunguza msongo wa mawazo na kujaribu kuyachepua mapenzi yenu
Ni vizuri mke wako anaelewa. Wengine huwa wanakataa wanaona ni matumizi mabaya ya pesa. Kuna huyo mmoja alisema hawezi kuponda raha na mume huku wazazi wake wana shida
 
Ni vizuri mke wako anaelewa. Wengine huwa wanakataa wanaona ni matumizi mabaya ya pesa. Kuna huyo mmoja alisema hawezi kuponda raha na mume huku wazazi wake wana shida
Yeah sure

Siku Moja Moja sio vibaya kwenda kuupa mwili raha 🤗
 
Lakini ilikuwa si sababu yenye nguvu kum cheat mkewe, unashindwa vipi kumtoa mkeo dinner kama unataka kutoka nae, lazima umshawishi akuelewe mtoke, kama unashindwa kushawishi mwanamke wako mtoke dinner sasa we ni mwanaume ama kituko.
 
Mume wako anakuambia mke wangu leo tutoke tukapate hata dinner nje, wewe unajidai wife material unamwambia mtapoteza hela bora mpike nyumbani. Siku nyingine anakuambia mtoke hata mkamwagilie moyo kidogo kama kawaida wife material unakataa unamwambia ni bora mnunue mmwagilie nyumbani.

Unamwambia ni matumizi mabaya ya pesa hiyo pesa ya kwenda dinner nje ni bora sijui mfanyie hivi au vile na hiyo pesa anayotaka mkapige maji ni bora muwatumie wazazi wenu.

Ukiiangalia kwa mbali inaonekana kama wewe una akili na ni wife material ambaye mwanaume yeyote anahitaji ,ofc ni wife material, na hautampoteza mume wako ila madhara yake ni makubwa.

Wewe haufikirii labda mumeo anataka mtoke ili awe na wewe nje ya mazingira ya nyumbani akuone vile ukivaa kimtoko mtoko unapendeza ( ukizingatia wengi tukiwa nyumbani ni madera tu). Yaani wewe haufikirii kwamba mume wako anahitaji huo muda kwa ajili yenu , mbali na kelele za watoto nk?

Basi juzi rafiki yangu kaenda Bar kumfumania mume wake na mchepuko wanakunywa mapombe na makange ya kuku huku wanafurahia live band. Mume pale pale kamwambia mkewe nikikuambia tutoke out hautaki wewe endelea kuwa mama wa nyumba maana hautaki kuiacha pekee yake.

Haya endeleeni kuwagomea wanaume zenu kutoka, kule kwenye bata kuna wadada wanaovizia wababa wanaokuja pekee yao, watakula hizo hela ulizokataa kuzila wewe.
Sasa fundisho lako ni nini? Kwamba hao wife materials wafumbie macho matumizi holela ya waume zao? Yaan badala ya kuwakemea hao wakina dada wanaodanga na kujiuza uko bar ili waamke na kujitafutia shughuli halali za kuwaingizia kipato au watulie na kuwa wake wema wewe unawachamba wife materials ambao wana nia njema na pesa za waune zao. Kweli wanawake mwalimu wenu ni kipofu.
 
Back
Top Bottom