Wilaya ya Musoma - Fursa za Kukuza Uchumi na Maendeleo

Wilaya ya Musoma - Fursa za Kukuza Uchumi na Maendeleo

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WILAYA YA MUSOMA - FURSA ZA KUKUZA UCHUMI NA MAENDELEO

Tarehe ya Kongamano: Jumatatu, 30 Dec 2024

Mahali: Kiwanja cha Mukendo, Manispaa ya Musoma

Mgemi Rasmi: Mhe Juma Issa Chikoka, Mkuu wa Wilaya, Wilaya ya Musoma

Mchango wa Prof Sospeter Muhongo, Mbunge, Jimbo la Musoma Vijijini

Mbunge ameainisha maeneo ya uwekezaji yatakayokuza uchumi wa Wilaya ya Musoma, kwa haraka (8-10% growth), na kuongeza kwa kasi ya upatikanaji wa ajira mpya na maisha bora zaidi.

Maeneo makuu ya uwekazaji:
(i) Elimu bora na Elimu ya ufundi
(ii) Uvuvi: vizimba na viwanda vya samaki
(iii) Kilimo cha umwagiliaji na viwanda vya usindikaji mazao, na kiwanda kipya cha nguo
(iv) Ufugaji: maziwa na kiwanda cha maziwa, n.k.
(v) Uchimbaji madini: dhahabu, gesi ya helium, n.k.
(vi) Utalii: visiwa ndani ya Wilaya yetu, n.k.

VIDEO/CLIP iliyoambatanishwa hapa: tafadhali sikiliza sehemu ya mchango wa Prof Sospeter Muhongo, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Jumatatu, 30 Dec 2024
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2024-12-31 at 09.02.03.mp4
    24.6 MB
Musoma, na wilaya zingine za mkoa wa Mara kuna umasikini mkubwa sana mzungukonwa pesa hapo Musoma mjini ni mdogo vibaya mno.

Furusa ni ndogo sana na Furusa pekee pale ni ile ziwa ambalo pia kwa sasa hakuna Samaki za maana pale.

Aridhi ya mkoa wa Mara sio rafiki kwa kilo cha maana sana.
 
Kilimo cha mazao gani na wapi? Ikotoa Tarime mkoa wa mara sehemu zinazo bakia hazina aridhi nzuri ya kilimo ni full kichanga.

Pale labda wambie wawekeze kwenye kilimo cha Viazi, wanaweza export viazi wakiwa serious, mazoa mengine waachame nayo labda Pamba lakiki Pamba nayo imekaa kisiasa sana.

Uvuvi na utalii ndio vitu vinaweza saidia mkoa, ila utalii unahitaji uwekezaji mkubwa sana hasa Water sport ndani ya ziwa Victoria ila pia inaelekea watalii wa waywe sport ni wachache make hii ni mambo ya hobby.

All in all Musoma imejaa umasikini sana mzunguko wa pesa ni wa kusiktisha sana na niliuliza nikaambwa hata wenyeji, wanakimbilia mwanza na Kahama kufanya biashara.

Musoma pia imekaa pembeni sana,ilipaswa kusetiwa pale Makutano labda angalau. Ila pia ukisema makutano inakaa make Bunda ile nayo imelala sana na inapitiwa na barabara.

Pia Mpaka wa Sirali sio Mpaka ulioko busy ukilinganisha na mipaka mingine, unaweza toka Mwanza hadi Tarime hapo katikati ukapishana na roli za maana 2 tu.
 
Kilimo cha mazao gani na wapi? Ikotoa Tarime mkoa wa mara sehemu zinazo bakia hazina aridhi nzuri ya kilimo ni full kichanga.

Pale labda wambie wawekeze kwenye kilimo cha Viazi, wanaweza export viazi wakiwa serious, mazoa mengine waachame nayo labda Pamba lakiki Pamba nayo imekaa kisiasa sana.

Uvuvi na utalii ndio vitu vinaweza saidia mkoa, ila utalii unahitaji uwekezaji mkubwa sana hasa Water sport ndani ya ziwa Victoria ila pia inaelekea watalii wa waywe sport ni wachache make hii ni mambo ya hobby.

All in all Musoma imejaa umasikini sana mzunguko wa pesa ni wa kusiktisha sana na niliuliza nikaambwa hata wenyeji, wanakimbilia mwanza na Kahama kufanya biashara.

Musoma pia imekaa pembeni sana,ilipaswa kusetiwa pale Makutano labda angalau. Ila pia ukisema makutano inakaa make Bunda ile nayo imelala sana na inapitiwa na barabara.

Pia Mpaka wa Sirali sio Mpaka ulioko busy ukilinganisha na mipaka mingine, unaweza toka Mwanza hadi Tarime hapo katikati ukapishana na roli za maana 2 tu.
taarifa nzuri ila kidogo bado inamapungufu katika uwasilishaji
 
Hakuna gesi ya helium Musoma na Mkoa wa Mara Kwa ujumla wake.

Prof muhong.. ni Prof Muongo!
 
Back
Top Bottom