William Tyndale alichomwa moto mpaka kufariki kwa kutafasiri Biblia kutoka kwenye lugha ya Kigiriki kuiingiza kwenye kingereza

William Tyndale alichomwa moto mpaka kufariki kwa kutafasiri Biblia kutoka kwenye lugha ya Kigiriki kuiingiza kwenye kingereza

Jackwillpower

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2017
Posts
2,467
Reaction score
3,687
William Tyndale alikuwa mwanatheolojia Mwingereza, kasisi ya kanisa na mtaalamu aliyetafsiri Biblia mara ya kwanza katika Kiingereza cha kisasa. Alizaliwa huko Gloucestershire mnamo mwaka 1494 - aliuawa Vilvoorde (Brabant - Ubelgiji ya leo) tarehe 6.9.1536. Tafsiri yake ya Biblia ilikuwa toleo la kwanza lililochapishwa kwa kutumia mitambo mapya ya uchapaji vitabu.
1619390420147.png



Mawazo yake yalipingwa kwa nguvu zote na watawala na watu wa ROMA yalionekana kama upinzani wa kidini hivyo aliamua kukimbilia Ujerumani kwa usalama wake, huko alitafuta mchapishaji aliyetoa nakala ya kwanza ya Agano Jipya kwa lugha ya kingereza nakufuatiwa baadaye na agano la kale.

Askofu Kardinali Wolsey alimtangaza kuwa mzushi.

Tyndale aliishi wakati ambapo waalimu tu walionekana kuwa wenye ujuzi wa kusoma na kwa usahihi kutafsiri Neno la Mungu. Biblia bado ilikuwa "kitabu kilichokatazwa" na mamlaka ya kanisa la ROMA huko Ulaya Magharibi.

Mwaka wa 1524 Tyndale alikwenda Hamburg, Ujerumani, ambapo kwa Martin Luther aliyebadilisha sura ya Ukristo huko. Wanahistoria wanaamini Tyndale alimtembelea Luther huko Wittenberg na kushauriana na tafsiri nyingine ya BIBLIA ya Luther ya Kijerumani. Mnamo 1525, akiwa akiishi Wittenberg, Tyndale alimaliza tafsiri yake ya Agano Jipya kwa Kiingereza.

Uchapishaji wa kwanza wa Agano Jipya la Kiingereza la William Tyndale ulikamilishwa mnamo 1526 Worms, Ujerumani. Kutoka huko "toleo la" octavo "ndogo lilipelekwa Uingereza kwa siri kwa kufichwa katika bidhaa, mapipa, na magunia ya unga.
Henry VIII aliipinga tafsiri na maafisa wa kanisa waliihukumu. Maelfu ya nakala zilichapishwa na mamlaka ikazichoma kwa umma.

Lakini upinzani ulionyesha kuwa na kasi, na mahitaji ya Bibles zaidi nchini Uingereza iliongezeka kwa kiwango cha kutisha.

Mwaka 1536,Muingereza, William Tyndale alichomwa moto mpaka kufariki kwa kutafasiri Biblia kutoka kwenye lugha ya Kigiriki kuiingiza kwenye kingereza.
Na neno lake la mwisho kabla ys kufa alisema "Mungu, fungua macho ya Wafalme wa Uingereza.

1619391407794.png


KABURI LAKE HUKO Vilvoorde (Brabant - Ubelgiji ya leo)

1619391501609.png


1619391642633.png


NB:UNAPOIONA BIBLIA LEO JUA KUNA WATU WALIFANYA KU SUCRIFICE MAISHA YAO ILI IKUFIKIE HAPO ULIPO, WALIOULIWA KWA KUTAFSIRI BIBLIA KUTOKA KIGIRIKI KWENDA LUGHA NYINGINE NI WENGI , ASILIMIA KUBWA WALIPOTEZA MAISHA KWA KUCHOMWA MOTO, KULIWA NA WANYAMA WAKALI HUKO ROMA

1619391382170.png
 
Huyo mwamba ni moja ya binadamu waliokufa kifo cha mateso kosa ni kutounga juhudi za bwana Papa
Mwingine ni
Galilei Galileo aliyegundua darubini upeo na kugundua uwepo we sayari nyingine na kuwaambia dunia ni duara wafia dini wanaoamini dunia ni flati wakaishia kumfungia asitoke nje maisha yake yote eti kisa
Mzushi!

Enzi hizo kuitwa mzushi
Ni sawa na enzi za mtu pori jiwe
Kuitwa kibaraka wa maBeberu au sio mzalendo!.
😂😂😂😂😂
 
Huyo mwamba ni moja ya binadamu waliokufa kifo cha mateso kosa ni kutounga juhudi za bwana Papa
Mwingine ni
Galilei Galileo aliyegundua darubini upeo na kugundua uwepo we sayari nyingine na kuwaambia dunia ni duara wafia dini wanaoamini dunia ni flati wakaishia kumfungia asitoke nje maisha yake yote eti kisa
Mzushi!

Enzi hizo kuitwa mzushi
Ni sawa na enzi za mtu pori jiwe
Kuitwa kibaraka wa maBeberu au sio mzalendo!.
😂😂😂😂😂
upapa unakadiriwa kuua watu zaidi ya million 50

MARTIN LUTHER sijui aliwakimbiaje, ilikuwa auwawe
 
Hata Sir Issack Newton alifukuzwa kanisani kwa kupinga utatu mtakatifu katika zama hizo, naye angalikuwepo katika zama za huyo Bwana bila shaka naye angalichomwa moto.
 
William Tyndale alikuwa mwanatheolojia Mwingereza, kasisi ya kanisa na mtaalamu aliyetafsiri Biblia mara ya kwanza katika Kiingereza cha kisasa. Alizaliwa huko Gloucestershire mnamo mwaka 1494 - aliuawa Vilvoorde (Brabant - Ubelgiji ya leo) tarehe 6.9.1536. Tafsiri yake ya Biblia ilikuwa toleo la kwanza lililochapishwa kwa kutumia mitambo mapya ya uchapaji vitabu.
View attachment 1764296


Mawazo yake yalipingwa kwa nguvu zote na watawala na watu wa ROMA yalionekana kama upinzani wa kidini hivyo aliamua kukimbilia Ujerumani kwa usalama wake, huko alitafuta mchapishaji aliyetoa nakala ya kwanza ya Agano Jipya kwa lugha ya kingereza nakufuatiwa baadaye na agano la kale.

Askofu Kardinali Wolsey alimtangaza kuwa mzushi.

Tyndale aliishi wakati ambapo waalimu tu walionekana kuwa wenye ujuzi wa kusoma na kwa usahihi kutafsiri Neno la Mungu. Biblia bado ilikuwa "kitabu kilichokatazwa" na mamlaka ya kanisa la ROMA huko Ulaya Magharibi.

Mwaka wa 1524 Tyndale alikwenda Hamburg, Ujerumani, ambapo kwa Martin Luther aliyebadilisha sura ya Ukristo huko. Wanahistoria wanaamini Tyndale alimtembelea Luther huko Wittenberg na kushauriana na tafsiri nyingine ya BIBLIA ya Luther ya Kijerumani. Mnamo 1525, akiwa akiishi Wittenberg, Tyndale alimaliza tafsiri yake ya Agano Jipya kwa Kiingereza.

Uchapishaji wa kwanza wa Agano Jipya la Kiingereza la William Tyndale ulikamilishwa mnamo 1526 Worms, Ujerumani. Kutoka huko "toleo la" octavo "ndogo lilipelekwa Uingereza kwa siri kwa kufichwa katika bidhaa, mapipa, na magunia ya unga.
Henry VIII aliipinga tafsiri na maafisa wa kanisa waliihukumu. Maelfu ya nakala zilichapishwa na mamlaka ikazichoma kwa umma.

Lakini upinzani ulionyesha kuwa na kasi, na mahitaji ya Bibles zaidi nchini Uingereza iliongezeka kwa kiwango cha kutisha.

Mwaka 1536,Muingereza, William Tyndale alichomwa moto mpaka kufariki kwa kutafasiri Biblia kutoka kwenye lugha ya Kigiriki kuiingiza kwenye kingereza.
Na neno lake la mwisho kabla ys kufa alisema "Mungu, fungua macho ya Wafalme wa Uingereza.

View attachment 1764300


KABURI LAKE HUKO Vilvoorde (Brabant - Ubelgiji ya leo)


View attachment 1764301

View attachment 1764302

NB:UNAPOIONA BIBLIA LEO JUA KUNA WATU WALIFANYA KU SUCRIFICE MAISHA YAO ILI IKUFIKIE HAPO ULIPO, WALIOULIWA KWA KUTAFSIRI BIBLIA KUTOKA KIGIRIKI KWENDA LUGHA NYINGINE NI WENGI , ASILIMIA KUBWA WALIPOTEZA MAISHA KWA KUCHOMWA MOTO, KULIWA NA WANYAMA WAKALI HUKO ROMA

View attachment 1764299
Kwani hakuwa na kazi ya maana ya kufanya?
 
Hata Sir Issack Newton alifukuzwa kanisani kwa kupinga utatu mtakatifu katika zama hizo, naye angalikuwepo katika zama za huyo Bwana bila shaka naye angalichomwa moto.
kasome historis vzr
 
kasome historis vzr


Ni kweli hakufukuzwa Kanisani bali alifukuzwa ualimu huko Cambridge university alipokuwa mwalimu kutokana na kupinga imani ya utatu mtakatifu, ifuatayo ni kipande kidogo cha kadhia iliyomkuta Newton.


---- But the "Holy and Undivided Trinity" itself stood in his way. His stubborn refusal to subscribe to the doctrine of Trinity cost him not only his fellowship, but also the handsome stipend of ₤60 a year. Not small amount indeed, judging by the value of money in those days. He was dispossessed of his fellowship and chair from the university (Cambridge) on the charge of heresy . The charge of heresy was levelled against him only because in Newton's eyes worshipping Christ was idolatry , to him a fundamental sin. R.S. Westfall writes on Newton:

"He recognised Christ as a divine mediator between God and humankind , who was subordinate to the Father Who created him"


Extract from the book: Revelation, Rationality, knowlegde and Truth. Page 41.
 
NB:UNAPOIONA BIBLIA LEO JUA KUNA WATU WALIFANYA KU SUCRIFICE MAISHA YAO ILI IKUFIKIE HAPO ULIPO, WALIOULIWA KWA KUTAFSIRI BIBLIA KUTOKA KIGIRIKI KWENDA LUGHA NYINGINE NI WENGI , ASILIMIA KUBWA WALIPOTEZA MAISHA KWA KUCHOMWA MOTO, KULIWA NA WANYAMA WAKALI HUKO ROMA
Kwa namna ambavyi biblia inatumika vibaya na hawa manabi wa kileo, ni bora ingeachwa katika lugha ile: Mwamposa angeijulia wapi?
 
Nafikiri aliyetaka biblia ibaki kwenye lugha moja alikuwa na lengo zuri lakini alitumia njia hovu( ya kishenzi) kwa kuwaua waliokuwa na wazo la kuitafsiri. Mfano bila tafsiri za bible huu uongo wa mitume na manabii feki husingekuwepo.
Nafikiri Either ulikuwa mpango wa Mungu ili watu wengi wapate ujumbe au Mpango wa Shetani ili awadanganye wengi kwa uwepesi.

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
 
Nafikiri aliyetaka biblia ibaki kwenye lugha moja alikuwa na lengo zuri lakini alitumia njia hovu( ya kishenzi) kwa kuwaua waliokuwa na wazo la kuitafsiri. Mfano bila tafsiri za bible huu uongo wa mitume na manabii feki husingekuwepo.
Nafikiri Either ulikuwa mpango wa Mungu ili watu wengi wapate ujumbe au Mpango wa Shetani ili awadanganye wengi kwa uwepesi.

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
Bado yangekuwa yale yale maana watu wangejifunza kigriki ba kiibrania alaf waje kupiga ela tena.
 
Halafu huko kwenye kanisa katoliki ndiko kwenye watakatifu wengi walioko mbinguni , sijui huo utakatifu hapo Vatican unatafsiriwaje aisee?
 
Bado yangekuwa yale yale maana watu wangejifunza kigriki ba kiibrania alaf waje kupiga ela tena.
Ni kweli lakini siyo kwa utitiri kama huu tulio nao, Leo hii nikiweke sentensi moja ya kiswahili nikawaita watu sita wa lugha tofauti kila mtu aitafsiri kwenye lugha yake utapata mkanganyo wa ajabu sana.
Pamoja na Mapungufu yao tuwapongeze ndugu zetu Waislamu kwenye kudhibiti lugha imewasaidia sana ndo maana kwao unaona wapotoshaji ni wachache sana ukilingana na sisi wakristo.

Ukijaribu kuangalia baada ya Yesu kuondoka kanisa la kwanza liliendelea kupanua huduma zake pande nyingi za Dunia na ivyo wahubiri au tuseme wainjilishaji wapya walianza kuwepo lakini kwa kukwepa kusije kuwepo upotoshaji walibaki kuwa na centre moja Pale Jerusalem kwa akina petro, mambo yakijitokeza huko wanakuja kuuliza pale: mfano Paulo na kisa cha kutahiri, lakini kwa sasa hamna Centre kama hizi kila mtu ni mjuaji anafanya inavyomfaa, angalau tungekuwa standard moja ingesaidia.

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
 
Kwa namna ambavyi biblia inatumika vibaya na hawa manabi wa kileo, ni bora ingeachwa katika lugha ile: Mwamposa angeijulia wapi?
Amgetumia google translator mkuu😁
 
Back
Top Bottom