Naichukia ccm hadi kichwa kinaniuma
Ccm imenajisi hii nchi kwa kipindi kirefu na kwa kiwango kisichoelezeka. Ccm hata tukiwapa miaka 1000 hakuna kitu cha maana watafanya, hawana mbinu wala mkakati wowote wa kulizogeza hili taifa mbele.
Wameshindwa kwenye kila kitu, miundombinu barabara wanajenga leo kesho imebomoka, wanajenga gena, mipango miji ni hovyo haijawahi kutokea, nishati, miaka 60 bado nchi ina umeme wa megawati 1500?, maji, kuanzia vijiji hadi kwenye majiji hakuna uhakika wa maji, huduma za kijamii, elimu, ccm wanatoa elimu ya hovyo isiyo na mfano, mfumo wa elimu ni wa hovyo afya, leo hii Karne ya 21 mwanamke Tanzania akibeba mimba ni kama amejitoa mhanga, any time anaweza kufa. You can go on and on and on.
Ccm ni failure, baada ya Nyerere na Mwinyi, ccm ilivamiwa na magenge ya wezi na mafisadi, sasa wanachofanya ni kulindana tu na kula nchi. Wameuza almost kila kitu, madini, bahari, mbuga za wanyama na kila kitu.
Ccm hata uwape miaka 2000 hakuna kitu chochote cha maana watafanya.