Wizara tatu zajadili hali ya uzalishaji chumvi nchini Tanzania

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Wizara ya Mipango na Uwekezaji pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara zimekutana kujadili namna ya kuondoa changamoto katika sekta ndogo ya chumvi nchini.

Wizara hizo zimekutana jijini Dodoma kufuatia taarifa zilizowasilishwa kwa Serikali na Chama cha Wazalishaji Chumvi Tanzania (TASPA) kuhusu changamoto zinazoikabili sekta hiyo ndogo ya chumvi ikiwemo kudorora kwa biashara ya chumvi hapa nchini.

Kikao hicho kilijumuisha Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Suleiman Jaffo,Waziri Wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo na Waziri wa Madini Anthony Mavunde pamoja na Wadau wa Chumvi Nchini.

Pamoja na mambo mengine yaliyojadiliwa,Wizara ya Madini kupitia STAMICO imewahakikishia wadau juu ya ufungwaji wa kiwanda cha kusindika Chumvi katika Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi kabla ya mwisho wa Mwezi Desemba 2024.


 
Duh! Hata chumvi nayo imekuwa issue/challenge? Tuna safari ndefu! Au mimi ndiyo sielewi?! 😄
 
Duh! Hata chumvi nayo imekuwa issue/challenge? Tuna safari ndefu! Au mimi ndiyo sielewi?! 😄
Wewe ndio huelewi kuna watu bila Chumvi Maisha hayaendi kuna watu wanabugia Chumvi balaa yaan mezani unakutana kabisa na kikopo cha Chumvi Mboga imetiwa Chumvi Ila anaona haitoshi anaongezea paketi zinakatika ndani ya Wiki kuna watu wanabugia Chumvi ndugu yangu Mimi nimejionea mpaka nimeshangaa maharage yamejazwa Chumvi mpaka nasikia kiungulia Ila wao ni raha mu starehe yaan hapo wanasema Chumvi imekolea
 
Sema chumvi imatumika kidogo sana na haijawahi kuwa na uhaba kama sijakosea.
 
Sema chumvi imatumika kidogo sana na haijawahi kuwa na uhaba kama sijakosea.
Kuna Watu wanaitumia vilivyo yaan wanaitumia Chumvi mpaka unaona sasa kuna uhaba kuna Siku nilichoma kuku nikafanya yote nilichosahau ni kutia Chumvi maana inabidi umchanechane alafu unakua km unampaka Chumvi na viungo vingine kuleta radha si nikasahau kumtia Chumvi Jamaa wapenda chumvi acha wanilaumu wanasema sasa huyu bila Chumvi atalika Vipi nani atakula kuku wa baridi?
 
Taifa hili waje wakoloni tu, watulioishe kodi ya kichwa, ijulikane moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…