Wizara ya Afya Wekeni chanjo za kutosha vituoni

Wizara ya Afya Wekeni chanjo za kutosha vituoni

mama dunia

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2011
Posts
420
Reaction score
84
Tangu saa 3 tupo kituoni chanjo hizi za kampeni zimeisha.wametuambia tusubiri wataleta tumesubiriiii weee bado hadi sasa.itabidi kuondoka na kurudi tena.

Ushauri kwa wizara: mnapotangaza muwe mmehakikisha chanjo zipo za kutosha jamani maana lazima watu watakuja wengi tu.
 
Ni wapi huko ndugu yangu nifatilie ili niangalie tunatatua vipi,
kwani baadhi ya maeneo chanjo zimeingia jana usiku na gari la MSD
 
Tangu saa 3 tupo kituoni chanjo hizi za kampeni zimeisha.wametuambia tusubiri wataleta tumesubiriiii weee bado hadi sasa.itabidi kuondoka na kurudi tena.

Ushauri kwa wizara: mnapotangaza muwe mmehakikisha chanjo zipo za kutosha jamani maana lazima watu watakuja wengi tu.
Jamaaa kwani mnahisi mtaumwa ugonjwa gani hadi mnasubiri chanjo namna hiyo? Tuwe makini isije kuwa kama west africa....wamepewa chanjo ambayo ni ugonjwa wa ebola, na pia kuna watoto pia walipigwa chanjo kumbe waliambukizwa virusi vya ukimwi....tuweni makini wa tz
 
  • Thanks
Reactions: aye
Binafsi nakerwa sana na hii inayoitwa chanjo! hivi zile chanjo wanazopewa watoto mpaka kufikia umri wa miezi tisa hazitoshi?? JF ina doctors hebu tupeni majibu tafadhali??
 
Tangu saa 3 tupo kituoni chanjo hizi za kampeni zimeisha.wametuambia tusubiri wataleta tumesubiriiii weee bado hadi sasa.itabidi kuondoka na kurudi tena.

Ushauri kwa wizara: mnapotangaza muwe mmehakikisha chanjo zipo za kutosha jamani maana lazima watu watakuja wengi tu.
Samahani hiyo ni chanjo ya ugonjwa gani?
 
Jamaaa kwani mnahisi mtaumwa ugonjwa gani hadi mnasubiri chanjo namna hiyo? Tuwe makini isije kuwa kama west africa....wamepewa chanjo ambayo ni ugonjwa wa ebola, na pia kuna watoto pia walipigwa chanjo kumbe waliambukizwa virusi vya ukimwi....tuweni makini wa tz

Acha upotoshaji wako chanjo zinaepusha magonjwa na ulemavu baadae.Unapoandika mada bila kujua unachoandika aheri upite ukiwa unasoma tu.Huko Afrika Magharibi kuna ukweli gani ya unayoyasema zaidi ya propaganda na kulishana matango mwitu mitaani.Yaani serikali iwekeze pesa nyingi kwenye miradi ya chanjo kulinda raia wawe salama wajenge nchi na kukuza uchumi wewe unakuja na mchango kama huu.
 
mimi wanangu sijawapeleka,walishapata hizi chanjo walipokuwa na miezi 9,wakapewa ile ile tena wakiwa na miezi 18
 
Samahani hiyo ni chanjo ya ugonjwa gani?

Ni magonjwa mengi tu Kuharisha(Diarhea),homa ya uti wa mgongo (Meningitis),Kichomi (Pneumonia),Mchochota wa ini B (Hepatisis B),Surua (Measles),Polio,Kifaduro,Dondakoo na mengineyo.
 
mimi wanangu sijawapeleka,walishapata hizi chanjo walipokuwa na miezi 9,wakapewa ile ile tena wakiwa na miezi 18

Victoire wakamilishie chanjo watoto wako ili kuwaepusha na magonjwa.Ugonjwa wa Surua kwa mfano imebidi muda wa kupewa chanjo uongezwe kwani chanjo za awali zinapungua nguvu hivyo ugonjwa ukilipuka inakuwa hatari.Tupo radhi kupuuzia chanjo lakini tuje tutumie pesa nyingi kutibu au uhai kupotea.Tuamke jamani kuasi chanjo na maneno ya mitaani hayatusaidii.
 
Last edited by a moderator:
hili lilikuwa ni tatizo la kukosa target population! hivyo waliopata wamepata na waliokosa pole sana! wizara ilitoa idadi ya watu wanaotakiwa kuchanjwa na si idadi ya watu wanaohitaji kuchanjwa! NI JANGA NA AIBU KWA WIZARA!
 
Back
Top Bottom