Wizara ya Ardhi, taifa linasubiri uchambuzi wa kitaalamu unaotokana na data mlizokusanya katika kliniki zenu, mje na suluhu ya kudumu

Wizara ya Ardhi, taifa linasubiri uchambuzi wa kitaalamu unaotokana na data mlizokusanya katika kliniki zenu, mje na suluhu ya kudumu

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Kliniki za ardhi, walau kwa kiasi fulani, hazitarajiwi kuwa suala la kudumu. Zitumike kutambua chanzo cha tatizo, na wizara iwasilishe andiko la kitaalamu kuhusu hasa kilichotufikisha hapo, na ikiwezekana lisomwe kwa watu wote, likiwa na mapendekezo ya suluhusho.

Mapendekezo hayo yarejeshwe kwenye jamii, ili jamii iangalie kama yanakidhi, na kama inawezekana jamii nayo ichangie, kwa kuwa ndio inaishi na kero hizo.

Mimi nazifananisha na jamii yenye wagonjwa wengi wa maleria, lakini iko bize kuwatibu, halafu wanarudi majumbami kwao kwenye mazalia ya mbu.

Kliniki zitumike kuonyesha viashiria vya mapungufu ya kisera, kiutendaji na kisheria, na jinsi ya kushughulikia tatizo hilo.

Hivyo ndivyo tunajenga mifumo imara ya kitaasisi.
 
Serikali iache kuchukua maeneo ya wananchi bila fidia, halimashauri zimekuwa kichocheo Cha migogoro.
 
Maeneo kama masoko, shule na maeneo ya wazi wananchi wanatapeliwa na halimashauri ndiyo maana migogoro haiishi. Migogoro mingi ya Ardhi ni Kati ya wananchi na serikali za mitaa hususani halimashauri za wilaya.
 
Maeneo kama masoko, shule na maeneo ya wazi wananchi wanatapeliwa na halimashauri ndiyo maana migogoro haiishi. Migogoro mingi ya Ardhi ni Kati ya wananchi na serikali za mitaa hususani halimashauri za wilaya.
Kwa kweli, hivi wanashindwa kuja au kutafuta teknolojia rahisi za upimaji kwa maeneo ya vijijini, ambazo zinaweza kutumiwa hata na mjumbe wa serikali ya kijiji kutambua mipaka ya wakazi wa hapo?

Au kwa nini mpaka leo mabenki wanapigwa kutokana na mfumo wa RITA kushindwa kuoana na mifumo ya msajili wa hati na ardhi, ili kama mtu ana mke, benki wanamsoma moja kwa moja kwa lengo la kibali cha mwanandoa?

Hata Samia juzi aliswma mifumo isomane
 
Kwa kweli, hivi wanashindwa kuja au kutafuta teknolojia rahisi za upimaji kwa maeneo ya vijijini, ambazo zinaweza kutumiwa hata na mjumbe wa serikali ya kijiji kutambua mipaka ya wakazi wa hapo...
Ni hatari mkuu Samia atarekebisha am sure.
 
Hayo yalikuwa mambo ya Jerry Silaa zaidi
 
Hayo yalikuwa mambo ya Jerry Silaa zaidi
Jerry hamna kitu, kaishia kupiga limudomo tu, hakufanya mabadiliko yoyote ya kimifumo, alidhani nchi hii ni kama nyumbani kwake kwamba anaweza kuingia kila chumba, jengo la wizara tu mpaka anaondokq kuna vyumba hajafika, sembuse utembee nchi nzima?

Ukiweka mifumo, inakandamiza nchi nzima kiutekelezaji

Na mudomo wake ndio umemyindoa kwenye uwaziri kwa kumdogosha yule mzee wa Morogoro, msitu wa kuni
 
Back
Top Bottom