Wizara ya Elimu ianzishe mtaala mashuleni kufundisha nukuu, mausia, maono, maelekezo ya Rais Samia

Wizara ya Elimu ianzishe mtaala mashuleni kufundisha nukuu, mausia, maono, maelekezo ya Rais Samia

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wadau hamjamboni nyote?

Nawaslisha hoja ya kizalendo kwa Wazalendo nikiomba mniunge mkono kwa maslahi mapana ya taifa letu.

Niombe Wizara ya Elimu iandae mtaala mahsusi mashuleni kufundisha nukuu, mausia, maonyo, maono, maelekezo, maagizo na ushauri wa Rais Samia na Viongozi wajao

Niombe mtaala huo utakaofundishwa kuanzia shule za msingi uwe endelevu kwa Marais wa Tanzania watakaochukua madaraka siku za usoni.

Naamini mtaala huo utawafanya wanafunzi wetu wawe Wazalendo,
Utawaimarisha kifikra, utawajengea uwezo wa Kiuongozi na uelewa kuhusu Serikali yao na taifa lao.

Maono ya Viongozi wetu wakuu yasiwe kwa ajili ya wanasiasa na watendaji waliopo Serikalini na kwenye Chama pekee bali pia kwa wanafunzi wetu.

Karibuni tujadili
 
Jamani mama ake Lucas Mwanshamba yupo Korea huko na huko Korea hali si hali na Korea kaskazini muda wowote
 
Back
Top Bottom