Wizara ya kazi: Tatizo la ajira nchini lapungua toka 16% mpaka 13%

Hofstede

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2007
Posts
3,577
Reaction score
1,109

Nilikuwa sijui kuwa Tanzania ni moja kati ya nchi chache zinazoongoza kwa ajira maana kuwa na Unemployment rate ya 13% miongoni mwa vijana ni hatua kubwa. Ila swali langu ni kwa nini uhalifu upo juu na vijana wengi wanashinda vijiweni?, je katibu mkuu wa wizara anaposema ajira anaingiza na wapiga debe na vibaka na dadapoa? au ni ajira gani hasa?
 
Takwimu za kupika kabisa, haiwezekani dunia nzima iko katika matatizo ya ajira Tanzania nchi maskini kuliko zote iwe na takwimu za kinyume nyume namna hii. hiki ndio kipindi ambacho kuna vijana wengi kabisa wanamaliza shule kwa wingi kuliko kipindi chochote kile katika historia ya nchi hii na vijana wanao ingia mtaa ni wengi na ushahidi ni huku uswazi na mkoa ambapo vijana kibao wako kijiweni.

Takwimu hizi kaandaliwa mtu atiwe changa la macho kama sio wafadhili basi JK, sidhani kama sie wabongo zinatuhusu manake sio za kwetu na haionyeshi picha halisi kuna mshauri kavuta hela na kupika data.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…