Wizara ya Nishati na Madini: Tanzania kuuza umeme Kenya na Zambia

Wizara ya Nishati na Madini: Tanzania kuuza umeme Kenya na Zambia

makolola

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2014
Posts
765
Reaction score
289
Najiuliza kabla ya kuanza kuuza wameshatenga ni kiasi gani watatumia kuanzisha viwanda vipya ili kuongeza ajira nchini?

wamefikiria ni namna gani nchi nzima itafaidika na umeme huo kabla ya kuanza kuugawa kwa wageni hasa ukilinganisha ni 10% ya watz wanafaidika na umeme kwa sasa?

wameshaangalia namna ya kuwapatia wananchi unafuu wa maisha kwa kushusha bei ya umeme?


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI UENDELEZAJI WA MRADI WA KUUNGANISHA GRIDI ZA
UMEME ZA ZAMBIA-TANZANIA NA KENYA (ZTK)
Napenda kuwajulisha kwamba Wizara ya Nishati na Madini itakuwa mwenyeji wa Mkutano wa Mawaziri wa Nishati wa wa nchi za Zambia, Kenya na Tanzania unaotarajiwa kufanyika tarehe 30 Septemba, 2014 ambapo Wizara ya Nishati na Madini itakuwa mwenyeji wa mkutano huo utakaofanyika katika hoteli ya JB Belmonte jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo utajadili juu ya utekelezaji wa mradi wa kuunganisha mtandao wa umeme katika gridi za nchi hizo tatu (Zambia, Tanzania, Kenya) ‘ZTK power interconnector project).

Aidha, Mkutano huo utatanguliwa na mikutano ya Makatibu Wakuu tarehe 29 Septemba, 2014 na mkutano wa wataalam wa sekta ya Nishati ya umeme kutoka nchi hizo tatu.

Katika mkutano huo, Mashirika ya umeme kutoka katika nchi hizo zitawasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi ya kuunganisha mtandao wa umeme pia watajadili na kusaini mkataba wa makubaliano ya utekelezaji wa mradi (Heads of Agreement – HOA).

Mwaka 1995, Mashirika ya umeme ya Zambia, Tanzania na Afrika Kusini yalianza kufanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kutathimini uwezekano wa kuunganisha mifumo ya gridi za umeme za Zambia na Tanzania. Upembuzi huo ulikamilika mwaka 1998 na kuthibitisha kuwa kuunganishwa kwa gridi za nchi husika kuna faida za kiuchumi, kijamii, kiufundi na kifedha.

Mwezi Januari, 2001, Mawaziri wanaosimamia masuala ya Nishati wa Zambia, Tanzania na Kenya walikutana ambapo Serikali ya Kenya ilionesha nia ya kushiriki katika mchakato wa kuendeleza mradi kwa lengo la kupata fursa ya kununua umeme wa bei nafuu kutoka Zambia. Hali hii ilibadili upeo wa mradi na kujulikana kama Zambia -Tanzania - Kenya Power Interconnector Project. Mradi huu unahusisha sehemu kuu zifuatazo:

i. Ujenzi wa laini ya msongo wa 400kV yenye uwezo wa kusafirisha MW 400 kutoka kituo cha kupoozea umeme kilichopo Pensulo, Zambia hadi kituo cha kupoozea umeme cha Mwakibete, Mbeya kwa upande wa Tanzania,

ii. Kuimarisha mfumo wa usafirishaji umeme nchini kwa ajili ya kuwezesha kusafirisha umeme unaotosheleza, wenye ubora na uhakika katika maeneo ya kaskazini, kaskazini mashariki na magharibi hadi kufikia Kenya kwa kujenga njia mpya ya kusafirisha umeme kutoka Mbeya hadi Singida katika msongo wa kV 400, na

iii. Ujenzi wa laini ya kusafirisha umeme yenye msongo wa kV 400 kutoka Arusha hadi Nairobi

Aidha, mradi wa ZTK ni mmoja kati ya miradi ambayo kwa siku nyingi imekuwa katika Mpango Kabambe wa Kuendeleza Sekta ya Umeme (PSMP) kama miradi mhimili ambayo kuendelezwa kwake kutachangia kuwepo kwa vyanzo vya umeme mbadala kutoka nchi za jirani na hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa kero ya upungufu wa umeme ambayo imekuwa ikiikumba nchi yetu mara kwa mara ambayo imesababisha kutoa huduma ya umeme kwa mgawo. Aidha, mradi huu pia utafungua uhusiano wa kibiashara kati ya makampuni ya umeme ya nchi

wanachama kwani mifumo ya usafirishaji umeme imepangwa iwe na uwezo wa kusafirisha umeme pande mbili (bi-directional) kwa ajili ya kununua na kuuza umeme kupitia masoko ya East African Power Pool (EACPP) na Southern African Power Pool (SAPP).

Kuunganisha gridi za umeme za nchi jirani ni moja ya mkakati wa kipaumbele ili kuepuka matatizo ya nchi moja kukosa umeme wakati nchi ya jirani inao umeme wa ziada kama ilivyoainishwa katika Power System Master Plan (PSMP). Aidha, ni moja kati ya malengo ya shirikisho la NEPAD kuona kuwa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara zinakuwa na ushirikiano wa karibu katika masuala ya kuinua uchumi ambapo huduma ya umeme wa uhakika inahitajika.

Imetolewa na;

Badra Masoud
Msemaji,
Wizara ya Nishati na Madini
 
Utawezaje kutoa chakula ndani wakati watoto wako wakufa na njaa ? Utakuwa baba wainagani ww?
 
Najiuliza kabla ya kuanza kuuza wameshatenga ni kiasi gani watatumia kuanzisha viwanda vipya ili kuongeza ajira nchini?

wamefikiria ni namna gani nchi nzima itafaidika na umeme huo kabla ya kuanza kuugawa kwa wageni hasa ukilinganisha ni 10% ya watz wanafaidika na umeme kwa sasa?

wameshaangalia namna ya kuwapatia wananchi unafuu wa maisha kwa kushusha bei ya umeme?

Wewe kweli una akili?sisi hatuna umeme wakutosha utautoa wapi umeme wakuuza una chekesha mkuu nenda shule hata ya msingi
 
Ndo uchizi unaanza hivi Tz umeme wenyewe wa shida thn wauze nje....sa ndo hatutatumia umeme tenaaa
 
Wewe kweli una akili?sisi hatuna umeme wakutosha utautoa wapi umeme wakuuza una cekesha mkuu nenda shule hata ya msingi

BOMBA LA GESI LIKIKAMILIKA TANZANIA ITAZALISHA UMEME MWINGI SANA (3,000 megawatts) , ni kiasi kikubwa sana kiasi kwamba kama unaingia ubia na mtu yeye ndio atakuwa anachukua kwako. tunalia lia kuwa shirikisho la afrika mashariki liende taratibu kujua faida za kila mshirika lakini ukweli ni kuwa tanzania ni nchi yeye mali ghafi nyingi isiyokuwa na viwanda vya kutosha, sasa badala ya kuangalia ujijenge vipi ndani ndio utoke nje unazidi kumpa mpinzani wako nishati?
 
Utawezaje kutoa chakula ndani wakati watoto wako wakufa na njaa ? Utakuwa baba wainagani ww?

Yaani saa nyingine mtu unaweza kusema watu wamelogwa! lakini hili sio bure, niukosefu wa talanta ya uongozi katika serikali ya nchi yetu! wengi wa viongozi wetu niwaigaji wa maendeleo ya nchi kubwa kiuchumi duniani bila kuwaza wenzetu walijifanyia nini kwanza ndio wakaangalia na jirani zao! sasa huo umeme utatumika kwenye viwanda vya majirani zetu na uchumi wao kuwa mnono maradufu huku sisi tukingojea kubatizwa jina la WALAJI wa bidhaa na WATUMIAJI wa bidhaa hizo kutoka nchi hizo jirani! na uhakika wa malipo ya huo umeme matokeo yake itakuwa ni manufaa kwa wachache tukiachia MADINI na ARDHI kwani hakuna tunachofaidika nacho kwa miaka 50 sasa! lakini ujinga ni wetu sisi watanzania hatuchagui wanaofaa wacha tuteseke!
 
Kama tungekuwa na serikali makini, hili lingekuwa ni suala lililotimia mwishoni mwa miaka ya themanini. Lakini kwa serikali tuliyonayo, hata hili ni ndoto za alinacha.
 
Ahsante sana Mkuu ni upumbavu mkubwa kufikiria kuuza umeme nchi za nje wakati watumiaji wa umeme wa Tanzania hawajafika hata 20% ya population.

Utawezaje kutoa chakula ndani wakati watoto wako wakufa na njaa ? Utakuwa baba wainagani ww?
 
Post hii haina ukweli, hata ukisoma kwa makini hiyo taarifa ya Badra Masoud, haisemi kuwa Tanzania itauza umeme nje. Hapa Tanzania itakuwa ni njia ya kupitisha umeme kutoka Zambia hadi Kenya. Wanaouziana umeme ni Zambia na Kenya, Tanzania itapata faida ya kuhost mradi kati ya nchi hizi mbili, kama njiabya kupitia umeme huo. Tuwe makini wakati tunasoma taarifa kama.
 
Post hii haina ukweli, hata ukisoma kwa makini hiyo taarifa ya Badra Masoud, haisemi kuwa Tanzania itauza umeme nje. Hapa Tanzania itakuwa ni njia ya kupitisha umeme kutoka Zambia hadi Kenya. Wanaouziana umeme ni Zambia na Kenya, Tanzania itapata faida ya kuhost mradi kati ya nchi hizi mbili, kama njiabya kupitia umeme huo. Tuwe makini wakati tunasoma taarifa kama.

Tukiwaambiaga vijana wa ufipa uwezo wao wa kuchanganua mambo ni mdogo na ni wavuta bangi mnakataa. Wao huwa hawasomi threads na kuielewa bali huwa wanakurupuka kama watu waliofumaniwa guest kuja kuchangia pumba. Ndio maana wameshindwa hata kuwashawishi watu makini kujiunga na chama chao. Wao wanapenda watu local kuanzia mwenyekiti wao hadi bavicha wote ni empty set.

Ilikua ni aibu mtu kama Zitto kukaa na wapuuzi hao. Zaidi alikua anakibeba chama kwani chadema kumejaa vilaza wengi. Kuna taahila moja linaitwa BAK nafikiri ndo linaongozaga kwa kuandika pumba alafu linajiona nalo lina akili. Ushuzi mtupu.
 
DUH KAMA ZE COMEDI VILE AHHHHHH AHHH dada Badra umetisha mama
 
Back
Top Bottom