KERO Wizi kupitia Mita za umeme (LUKU)

KERO Wizi kupitia Mita za umeme (LUKU)

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Joseph41

Member
Joined
Mar 21, 2024
Posts
16
Reaction score
5
Kuna changamoto ambazo hatuzielewi sisi kama wananchi kuhusu ukusanyaji wa Kodi ya jengo kupitia "Luku", na Mimi naomba kupata ufafanuzi Kwa msaada pia wa wananchi wengine, yaani mimi nimekuwa nikinunua umeme Kila mwezi, na wanakata wakati mwingine hadi 6000 eti ni deni la pango, lakini Cha kushangaza zaidi Kila mwezi wanakata ninaponunua umeme, na haijalishi umeme umenunua hata Kwa mwezi mara mbili, ila wanakata Kila unaponunua.

Zaidi Jana nanunua "LUKU" naambiwa deni langu ni kubwa, nikachukua jukumu la kupiga simu Tanesco, wakaniambia MITA yangu inadaiwa zaidi ya Tsh 20,000 na wakaniambia hawahusiki Kwa hilo, ila wahusika ni TRA lakini pia kupiga simu TRA nao wanasema hawahusiki, eti ni manispaa, na manispaa nawapigia simu nipate ufafanuzi namba naambiwa sio sahihi.

Hii inasikitisha sana Kwa wakazi wa Arusha jiji na maeneo mengine maana nimekutana na wafanyakazi wenzangu wengi wanalalamikia hii issue.

Ombi langu ni kwamba wakae chini wapitie mifumo yao, na waone shida Iko wapi, then watoe taarifa Kwa wananchi, yaani mtu una 10,000 unataka kununua umeme unapewa 2 units?

Na kama Kuna changes zozote ni kwa nini taarifa isitolewe?
 
7
Kuna changamoto ambazo hatuzielewi sisi kama wananchi kuhusu ukusanyaji wa Kodi ya jengo kupitia "Luku", na Mimi naomba kupata ufafanuzi Kwa msaada pia wa wananchi wengine, yaani mimi nimekuwa nikinunua umeme Kila mwezi, na wanakata wakati mwingine hadi 6000 eti ni deni la pango...
Sasa najiuliza kwani hizo za Kila mwezi wanazonikata naponunua luku, zinaenda wapi na hilo deni limetokea wapi?

Maana kama ni hayo ni mwezi wa pili nimelipia waliyosema kuwa ni deni zaidi ya 6000, na sasa naambiwa deni ni 22,500 . Sasa hiyo ni ya lini na wakati Mimi kwenye nyumba hiyo nimelipia hayo madeni wanayosema mara mbili ambapo ni mwezi wa pili, mwezi wa 4, je wao wanataka za Nini tena, na huku umeme Kila nikinunua nakatwa hizo tozo?
 
Back
Top Bottom