Wizi niliofanyiwa na Vodacom

Wizi niliofanyiwa na Vodacom

Abeid L Msanganzila

Senior Member
Joined
Dec 30, 2018
Posts
163
Reaction score
343
Habari za jioni wana jf? Poleni na harakati za kutwa nzima.

Leo hii nimeamua kushare uizi mpya wa vifurushi vya internet nilioushuhudia kupitia kampuni ya VODACOM.

Jana jioni wakati nafanya jambo muhimu mtandaoni ghafla nikakuta simu imeganda kupakua files fulani, nikiangalia mtandao naona bado 4G inapepea, nikaamua kuangalia MB zilizobaki, nikakuta zimeisha.

Sasa nikaamua kuunga MB za jero ili nimalizie kupakua nyaraka zangu. Nikaenda menu yao ya JIMIXIE nikakuta 500=MB 285. Nikaunga, ila cha kushangaza nikapewa MB 110. nikahisi labda hizo ni za offer😂😂 kuangalia salio naziona zenyewe tu hakuna zingine. Nilipowasiliana nao wakadai nisubiri masaa 24. Sasa leo hii wamenijibu kirahisi tu eti tatizo langu limetatuliwa😂😂😂. Kiufupi wameniibia kihivyo wala hawajarudisha ata mia mbovu🤔,

Sasa wakuu, NAPE si huwa haamini kama tunaibiwa, na tayari nimeshaibiwa mm, nimewatumia maelezo hayo TCRA wapo kimya. Je nini kifanyike ili hawa jamaa wajue hela zinatafutwa wala haziibiwi au kuokotwa kokote!
Viambatanisho👇👇
Screenshot_20221011-181718.png
 

Attachments

  • Screenshot_20221011-182217.png
    Screenshot_20221011-182217.png
    8.8 KB · Views: 9
Voda wezi na hovyo kabisa. Halafu ukinunua vifurushi viwili vyote viwe na data. Kinatumika kile ambacho umenunua baadaye. Hakuna First in first out. Mfano kama kuna kifurushi cha data kinaishia tarehe 12/10/2022, na kingine tarehe 13/10/2022. Basi kinatumika hicho kinachoisha tarehe 13 badala ya cha tarehe 12 ambacho ndo umenunua kabla ya hicho cha tarehe 13. Wizi mtupu. Maana kuna uwezekano mb’s zako zikafia ndani.

Haya makampuni ni changamoto sana na hawa viongozi tunaowachaguwa wala hawajali kutetea wananchi.
 
Voda wezi na hovyo kabisa. Halafu ukinunua vifurushi viwili vyote viwe na data. Kinatumika kile ambacho umenunua baadaye. Hakuna First in first out. Mfano kama kuna kifurushi cha data kinaishia tarehe 12/10/2022, na kingine tarehe 13/10/2022. Basi kinatumika hicho kinachoisha tarehe 13 badala ya cha tarehe 12 ambacho ndo umenunua kabla ya hicho cha tarehe 13. Wizi mtupu. Maana kuna uwezekano mb’s zako zikafia ndani.

Haya makampuni ni changamoto sana na hawa viongozi tunaowachaguwa wala hawajali kutetea wananchi.
Umeongea ukweli mkuu. Mm niliwahi kuwauliza wakadai eti ili mb zitumike vzr inatakiwa kuunga mb hadi ukiishiwa mb kabisa. Ila najua lengo ni upigaji tu sidhani kabisa kama watu wao wa IT wameshindwa kuset namna ya mfumo kutumia mb za vifurushi viwili tofauti.
 
Back
Top Bottom