Tetesi: Wizi ulioko kwenye Bolt/Taxify kuwa makini

Tetesi: Wizi ulioko kwenye Bolt/Taxify kuwa makini

officialBossmtoto

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2019
Posts
370
Reaction score
1,189
Wanamaendeleo habari za leo
Leo naomba kuchangia mada na nyinyi kuhusu hawa ndugu zetu wanaojipatia kula yao ya kila siku na kuendesha familia kwa kutupeleka maeneo mbalimbali ya jiji. Mwanzoni Taxify na sasa ikifahamika kama Bolt imesaidia vijana wengi sana hasa ambao leseni zao zilikua zinatumika tu kama kitambulisho.

Balaa lililopo sasa tukiachilia mbali lile la zaman la kuendeshwa spidi ya 30 Km/h hata kama njia ni nyeupe ni hili la kuibiwa waziwazi.

Mara ya kwanza nilitoka msasani nikienda Airport nikalipishwa 65,000/- za kitanzania. Nilishangaa sana ila niliona kwa sim yake, yangu na mpaka Email ilisoma hivo. Basi nikalipa maana sikua na ujanja. Katika kuendelea kutumia tumia mara siku rafiki yangu ambae tulikua nae kwenye trip ya 65,000/- akanipigia na kuniambia ameshuhudia jamaa akiandika kwenye sim 10,000 na alivomaliza ikasoma 10,000 kote.

Yani ni kama app wameichokonoa au wana yakwao inayoingiliana na ya Bolt.

Hii ni ishara mbaya sana hasa ukishangaa hii Kampuni na zingine zimesaidia madereva tax wengi waliokua wanangoja abiria vijiweni.

Nawasilisha. Najua wapo watakaokuja na kusema kwamba suluhisho ni kununua usafiri binafsi, ila naamini wapo wenye usafiri wao ila kwa sababu za hapa na pale kuna mida inawalazim kuingia ubber ama Bolt


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Uhalisia haya makampuni haya faida,niliwahi weka gari langu kwenye kampuni lao lakin nothing new,nikaamua kulitoa...anayenufaika zaid ni kampuni,we uliyeweka dhamana kuendesha biashara yao na kukuza kampuni lao unabak kupata faida ndogo sana.na mda kupoteza...
Nadhan ndio maana mda huu client wa kampuni wanafanya ujanja ili angalau ku maximize profit.
 
Hakuna kama uber majuzi nilisahau iphone yangu kwenye uber nililetewa kwahilo wanaonekana ni watu waaminifu
 
Kama unajielewa panda Uber, hizo bolt sijui ping mara little ride ukiibiwa imekula kwako
 
Uhalisia haya makampuni haya faida,niliwahi weka gari langu kwenye kampuni lao lakin nothing new,nikaamua kulitoa...anayenufaika zaid ni kampuni,we uliyeweka dhamana kuendesha biashara yao na kukuza kampuni lao unabak kupata faida ndogo sana.na mda kupoteza...
Nadhan ndio maana mda huu client wa kampuni wanafanya ujanja ili angalau ku maximize profit.

Sasa janja janja inacost mteja. Na pia naona unachosema wewe ni sawa. Wao wanapata Faida kwa sababu wanaoperate magari mengi kwa io wanapata kidogo ila kwa wingi. Ila kwa wewe unakuta gari moja ndo inakuletea so lazima ile kidogo yako iwe kidogo tuu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kama unajielewa panda Uber, hizo bolt sijui ping mara little ride ukiibiwa imekula kwako

Ubber wako vizuri ila igomvi wangu na wao ni kwenye kuCancel ride. Unakuta dereva umemrequest dakika 30 zimekata hafiki wala kwenye raman hasogei, ukitaka kucancel unaambiwa utachajiwa next trip, huku dereva ukimpigia anasema siji huko mbali cancel tuu sasa hapo ndo duh. Unalipa fedha hujaitumia


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
hivi kwenye hizo app kabla hata hujaita si inaonesha kiwango cha nauli kwa route husika!? maana kwa uber ndio ipo hivyo kabla hujaita unakua unajua utalipa sh. ngapi.
 
hivi kwenye hizo app kabla hata hujaita si inaonesha kiwango cha nauli kwa route husika!? maana kwa uber ndio ipo hivyo kabla hujaita unakua unajua utalipa sh. ngapi.

Yes ila kunakuaga Na variant nyingi sana. Kuna mda bei inashuka unalipa chini na kuna mda unalipa juu zaidi.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Tatizo mnaofata bolt wengi mnapenda slope hyo ndo inawacost acheni muibiwe tuu unakuta bei ya gari sawa na bajaji ukija mwsho wa safari inakuwa mara 3 yakee uber hawanaga hizo mambo wako smart hata tantax na exicab


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom