Tarime wazee wa kazi wale hawqana masihara. Walicheleweshewa matokeo wakati wa uchaguzi mdogo kura zilikuwa zinataka kupigwa. Walivyochoka kusubiria matokeo wakaambizana wakasema "MRA, TUNAKAA KUSUBHIRHI NINI WAKATI TUNAJUA TUMEMCHAGUA NANI, TWENDENI NYUMBANI HALAFU KAMA KUNA MWANAUME HAPA ATANGAZE MATOKEO TOFAUTI NA YALE TUNAYOYAJUA", thubutu, kura hazikuibiwa tena na matokeo yalitangazwa kama yalivyokuwa. Hao waache tu ni wanaume wa shoka mi nawakubali mno!
Mnasahau mbinu moja ya serikali ya CCM ambayo niliwahi kuizungumzia humu miezi kadha iliyopita. Mbinu hii hushirikisha NEC. Mbinu hii pia imeripotiwa kutumiwa Ethiopia na Zimbabwe katika chaguzi zao.
Ni mbinu inayosababisha wapiga kura wengi wa upinzani kushindwa kupiga kura – kwa sababu ya kutaoyaona majina yao kwenye vituo vyao siku ya uchaguzi na kusababisha turnout kuwa ndogo kama ilivyokuwa hapa katika uchaguzi wa 2005.
Kwa mfano katika jimbo la Temeke ambalo ni ngome kubwa ya CUF – wapiga kura zaidi ya 100,000 hawakupiga kura mwaka 2005 kutokana na kutoyaona majina yao.
Kinachofanyika ni hiki: Hawa kumikumi (10-cell leaders) wa CCM hupita kila nyumba katika eneo lao na kukusanya majina ya wanachama wao waliojiandikisha kupiga kura pamoja na kuchukua namba za shahada zao za kupiga kura, na namba ya kituo (centre number). Nasikia kila mjumbe akikusanya na kuwasilisha majina 20 anapata Sh 50,000. Utaona basi kwa hali yetu ya umasikini, hii ni ajira kubwa ya kuishupalia.
Baada ya hapo, majina haya kutoka kila kituo hukusanywa pamoja na kupelekwa NEC ambako kazi yao kubwa ni ku-refer katika orodha ya wapiga kura katika vituo husika. Kazi ya NEC ni kuyaondoa majina ya wale wapiga kura wengine ambao hawamo katika orodha hizo zilizokusanywa na hao kumikumi wa CCM – yaani kubakiza wapiga kura wa CCM tu.
Majina ya wapiga kura wengine wote – ambao bila shaka watakuwa wa vyama vya upinzani -- ama hufutwa kabisa, ama huhamishwa kupelekwa vituo vingine ili wapiga kura husika wapate tabu kuyatafuta -- baada ya NEC kubandika hizo listi zao kwenye vituo wiki moja kabla ya uchaguzi.
Bila shaka kuna majina ya wapiga kura wachache wengine wa upinzani ambayo huachwa kama kudanganyisha tu.
Matokeo ya hujuma hii ni kwamba siku ya kupiga kura wafuasi wengi wa vyama vya upinzani hawayaoni majina yao katika vituo walikojiandikisha.
Na wale ambao waligundua kabla ya kupiga kura kwamba hayamo majina yao huwa wana muda mchache sana kurekebisha hali hiyo, hasa ukizingatia ile bureaucratic red tape ya NEC.
Nasema haya kwa sababu baada ya uchaguzi wa 2005, hapa Dar, mimi na rafiki zangu watatu tunaojuana hatukuyaona majina yetu katika kituo tulikojiandikisha – nasi wote siyo wafuasi wa CCM.
Wenzetu wawili waliyaona majina yao katika kituo kimoja huko katika kata ya Mchafukoge badala ya kituo chao walichojiandikishia. Mimi na mwenzangu mwingine hatukyaona majina yetu katika vituo vingine tulivyotembelea lakini bila shaka utakutwa yalipelekwa Manzese au Buguruni.
Lakini kuna hatari kubwa kwa CCM iwapo watatumia mbinu hii tena safari hii hasa kutokana na wafuasi wao wengi kukihama chama hicho na kuwa tayari kuwapigia kura wagombea wa upinzani, hasa baada ya zoezi lao la kura za maoni zilizojaa vurugu na uonezi.
CCM wanaweza kujikuta silaha yao inawageukia wao wenyewe…..
Aidha najaribu sana kutafakari hiyo hatua ya NEC kuyafuta majina zaidi ya milioni mbili kwa sababu waliyotoa ya kwamba wenyewe walikufa etc – as if hawakujiandikisha watu wengine waliotimiza umri wa miaka 18.
Inawezekana ni hao niliyosema hapo juu kwamba sasa wameondolewa kabisa katika orodha ya NEC?
KUNA jambo moja muhimu sana:
Sitaki kupingana na mbinu ambazo wamekuwa wakizieleza waungwana kuhusiana na wizi wa kura kwa vile sina ushahidi nazo, lakini nataka kueleza kitu ambacho mie mwenyewe mimekiona na nina hakika hiki ndicho kinawaliza watu wengi sana mara baada ya kupiga kura.
Katika kampeni Vyama vya upinzani wamekuwa wakihamasisha watu kuwachukua wagombea wa CCM na kuwahukumu kwa kura, lakini wamekuwa wakishindwa kuwaeleza wapiga kura wao kuwa ni namna gani kura zinapaswa kupigwa.
KOSA lipo hapa:
Wanapokwenda kupiga KURA; Katika orodha ya wagombea 2 ama 3:
Mfano 1. Mgombea wa CHADEMA: M.M Mwanakijiji.
2. Mgombea wa CCM: Sikonge wa Sikonge.
Kwa haki wananchi wanakuwa wamemchoka mgombea wa CCM na wanamhitaji mgombea wa Chadema, lakini wakiingia katika sanduku la kupiga Kura wanaanza kumpigia wanaemtaka (Mgombea wao wa Chadema) wakimaliza hawatoki badala ya kuondoka kabla ya kukunja karatasi yao ya kura wanamtoboa MACHO ama kuandika maneno ya HATUKUTAKI/ HUFAI/ MWIZI n.k kwa mgombea wa CCM. Wakati wa zoezi la kuhesabu kura kura hizi nyingie zimekuwa zikionyesha kushinda lakini kwa utaratibu wa Uchaguzi kuwa na alama za Wino kwa maeneo yote mawili kura HUARIBIKA na hivyo mgombea waliyemtaka huanguka.
Hili lilitokea Geita, Kiukweli hawakuwa wakimtaka mgobea wa Ernest Mabina (CCM) na chaguo lao lilikuwa ni Malebo wa CUF, katika kituo kimoja cha kata ya Kamhanga kura ambazo Malebo alipigiwa lakini kwa mtimndo nilioueleza ziliharibika zilikuwa 68 hivyo Mabina wa CCM katika Kata hiyo alibakiwa na kura 145 kati ya 130 za Malebo na kama ungejumuisha na zile 68 basi ni wazi Malebo angeshinda. Hali ilikuwa karibu hivyo kila kata huku kata nyingine idadi ya kura zilizoharibika zikionekana kuharibika ikizidi kupanda mpaka 85.
Source: Frederick Katulanda wa Gazeti la Mwananchi
Wizi wa kura unaanza na Tume ya Uchaguzi inapotangaza idadi ya wapiga kura waliosajiliwa. Katika idadi hii kunakuwa na pasenti kubwa ya WAPIGA KURA HEWA. Hawa wapiga kura hewa watatumika kujaza mapengo pale mgombea wa CCM atakapoonekana kuelemewa.
Ili kutumia hizi kura feki wanakuwa pia na VITUO VYA KUPIGA KURA FEKI ambavyo vinakuwa na masanduku ya kupiga kura kama yaliyoko kwenye vituo vya kweli.
Hizi kura zinapigwa kisirisiri largely na usalama wa taifa na kuwekwa kwenye haya masanduku ya vituo hewa siku kadhaa kabla ya uchaguzi.
Mawakala wa uchaguzi wanasimamia kura katika vituo halali tu na hivyo vingine vilivyo feki of course hawana habari navyo. Kwa hiyo matokeo ya kura wanayoyafahamu mawakala ni yale ya vituo waliko tu na hata haya yanaweza kukumbwa na matatizo ya
(i) orodha ya wapiga kura kuwa na majina kibao ya wapiga kura hewa na watu kuandaliwa kuja kupiga kura kwa niaba ya hayo majina bandia,
(ii) kura zao kuweko kwenye masanduku kabla ya kupiga kura au
(iii) watu walioandaliwa kutumbukiza bulunguti la kura kwenye sanduku.
Kura kadhaa zimeshapatikana kwenye masanduku zikiwa zimeshikamana kwa njia ambayo ni wazi kuwa zimetumbukizwa na mtu mmoja. Tatizo hili laweza kupunguzwa, ijapokuwa siyo kumalizwa, kwa kutumia masanduku yalio transparent lakini nasikia masanduku hayatakuwa hivyo.
Tume ya uchaguzi ndiyo inayoruhusu haya yote yatokee na ndiyo inayojumlisha kura na kutangaza matokeo na jinsi sheria ya uchaguzi ilivyoandikwa ni wazi kuwa waliyoitayarisha hiyo sheria walikuwa na dhamira ya kuwezesha wizi wa kura na kutumia Tume kuhalalisha wizi huo.
Kutumia wakurugenzi wa Halmashauri kama wasimamizi wa uchaguzi majimboni ni nyenzo kubwa ya kufanikisha haya kwani wakurugenzi wote wanateuliwa na Rais directly au indirectly na Waziri wa TAMISEMI na you can be sure that they are all loyal members of CCM. Mambo mengine kama kuwarubuni mawakala wa vyama vingine au kuwahonga wagombea wajitoe dakika za mwisho ni mwendelezo tu wa msingi huu wa kuwaibia wananchi haki yao ya kuchagua viongozi wao.
Kwa jinsi sheria ya uchaguzi ilivyoandikwa, Tume ya Uchaguzi inaweza kumtangaza mgombea ambaye actually amepata kura chache kuwa mshindi na kutoa namba tu zanazodai kuwa huyu kashinda kwa kura nyingi ijapokuwa si hivyo.
Wizi wa kura uliofanyika Iran na Afganistan kwenye chaguzi zao za mwisho ni mifano mizuri ya kuwafumbua macho Watanzania kuhusu tatizo hili.
Mnasahau mbinu moja ya serikali ya CCM ambayo niliwahi kuizungumzia humu miezi kadha iliyopita. Mbinu hii hushirikisha NEC. Mbinu hii pia imeripotiwa kutumiwa Ethiopia na Zimbabwe katika chaguzi zao.
Ni mbinu inayosababisha wapiga kura wengi wa upinzani kushindwa kupiga kura – kwa sababu ya kutaoyaona majina yao kwenye vituo vyao siku ya uchaguzi na kusababisha turnout kuwa ndogo kama ilivyokuwa hapa katika uchaguzi wa 2005.
Kwa mfano katika jimbo la Temeke ambalo ni ngome kubwa ya CUF – wapiga kura zaidi ya 100,000 hawakupiga kura mwaka 2005 kutokana na kutoyaona majina yao.
Kinachofanyika ni hiki: Hawa kumikumi (10-cell leaders) wa CCM hupita kila nyumba katika eneo lao na kukusanya majina ya wanachama wao waliojiandikisha kupiga kura pamoja na kuchukua namba za shahada zao za kupiga kura, na namba ya kituo (centre number). Nasikia kila mjumbe akikusanya na kuwasilisha majina 20 anapata Sh 50,000. Utaona basi kwa hali yetu ya umasikini, hii ni ajira kubwa ya kuishupalia.
Baada ya hapo, majina haya kutoka kila kituo hukusanywa pamoja na kupelekwa NEC ambako kazi yao kubwa ni ku-refer katika orodha ya wapiga kura katika vituo husika. Kazi ya NEC ni kuyaondoa majina ya wale wapiga kura wengine ambao hawamo katika orodha hizo zilizokusanywa na hao kumikumi wa CCM – yaani kubakiza wapiga kura wa CCM tu.
Majina ya wapiga kura wengine wote – ambao bila shaka watakuwa wa vyama vya upinzani -- ama hufutwa kabisa, ama huhamishwa kupelekwa vituo vingine ili wapiga kura husika wapate tabu kuyatafuta -- baada ya NEC kubandika hizo listi zao kwenye vituo wiki moja kabla ya uchaguzi.
Bila shaka kuna majina ya wapiga kura wachache wengine wa upinzani ambayo huachwa kama kudanganyisha tu.
Matokeo ya hujuma hii ni kwamba siku ya kupiga kura wafuasi wengi wa vyama vya upinzani hawayaoni majina yao katika vituo walikojiandikisha.
Na wale ambao waligundua kabla ya kupiga kura kwamba hayamo majina yao huwa wana muda mchache sana kurekebisha hali hiyo, hasa ukizingatia ile bureaucratic red tape ya NEC.
Nasema haya kwa sababu baada ya uchaguzi wa 2005, hapa Dar, mimi na rafiki zangu watatu tunaojuana hatukuyaona majina yetu katika kituo tulikojiandikisha – nasi wote siyo wafuasi wa CCM.
Wenzetu wawili waliyaona majina yao katika kituo kimoja huko katika kata ya Mchafukoge badala ya kituo chao walichojiandikishia. Mimi na mwenzangu mwingine hatukyaona majina yetu katika vituo vingine tulivyotembelea lakini bila shaka utakutwa yalipelekwa Manzese au Buguruni.
Lakini kuna hatari kubwa kwa CCM iwapo watatumia mbinu hii tena safari hii hasa kutokana na wafuasi wao wengi kukihama chama hicho na kuwa tayari kuwapigia kura wagombea wa upinzani, hasa baada ya zoezi lao la kura za maoni zilizojaa vurugu na uonezi.
CCM wanaweza kujikuta silaha yao inawageukia wao wenyewe…..
Aidha najaribu sana kutafakari hiyo hatua ya NEC kuyafuta majina zaidi ya milioni mbili kwa sababu waliyotoa ya kwamba wenyewe walikufa etc – as if hawakujiandikisha watu wengine waliotimiza umri wa miaka 18.
Inawezekana ni hao niliyosema hapo juu kwamba sasa wameondolewa kabisa katika orodha ya NEC?
Hii ni njia nzuri kwa kupambana na wizi wa kura!mimi nadhani kazi ni kwa vyama vya siasa kuhakikisha kabla ya uchaguzi vinapata idadi ya vituo vya wapiga kura vitakavyotumika na idadi ya watu kwa kila kituo ili kukitokea ongezeko la watu na vituo tume iueleze umma vimetoka wapi na orodha hii iwe wazi kwa watu wote tujue na iwe kabla ya uchaguzi
Alisema tabia ya mawakala kutoka nje ya chumba cha kuhesabia kura na kwenda kujisaidia, inatoa fursa kwa baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu kuiba kura za CUF.
Alisema itakuwa busara kwa mawakala wa chama hicho kufika vituoni na chupa za maji ili wanapojisikia kwenda haja ndogo, wajisaidie kwenye chupa hizo badala ya kutoka nje na kurudi jambo ambalo alisema kuwa linalochangia kuibiwa kwa kura hizo.
"Katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu nakuombeni mchukue chupa za maji; kila mtu ahakikishe anakuja na chupa yake, ili anaposhikwa ajisaidie hapo hapo kwa ajili ya kuzilinda kura zenu," alisema Maalim Seif.
"Kwenda kujisaidia nje kutasababisha kuibiwa kwa kura; lazima muwe na mbinu kama hizo."
Source: http://www.mwananchi.co.tz/habari/5-habari-za-siasa/4703-maalim-seif-ni-uchaguzi-wa-kulinda-kura
Kinyume na watu wengi wanavyofikiria ni vigumu sana kuiba kura; chama kikiwa na usimamizi wa kutosha ni vigumu kuiba au kuweka kura za uongo. Kura zinaweza kuibwa pale ambapo tu vyama havijawaweka wasimamizi kabisa... au wameweka wasimamizi wenye kutafuta fedha tu.
Wakishindwa kuiba kura watapora tu ushindi kama walivyofanya Kibaki na Mugabe.....halafu watamwapisha JK haraka haraka tu hata iwe barabarani