Elections 2010 Wizi wa Kura unafanyika hivi...

serikali ya CCM ya kidhalimu inaweza kila kitu yaani hata kukupigia kura! haya ndo makosa tuliyofanya kwa nchi isiyo na demokrasia kama yetu!
 
Ebu tujuze pls maana mimi ni mhanga

mamaa weeee.....sasa itakuwaje....mbona wahanga tupo wengi.....jamani chonde nyie wataalamu wa mambo haya mtuambie tufanyeje....na muda ndio huo unayoyoma
 
Thanks jethro... Usiishie kwenye tetesi, ukikamilisa urudi kusema
 
mamaa weeee.....sasa itakuwaje....mbona wahanga tupo wengi.....jamani chonde nyie wataalamu wa mambo haya mtuambie tufanyeje....na muda ndio huo unayoyoma

Hapo twisha liwa yaaani kha kama democrasia inalazimishwa namna hiyo kwa kuwazurumu wananchi haki zao kwa kutumia hizo mbinu kwani nchi hii inatatizo gana jamani naona watu wake wapo poa kabisa yaani kuiongoza hii nchi ni simple sana ati kama ukijipanga kabisa within 10yrs tu jamani tunatoka kabisa bila tatizo lolote, Mfano mzuri tu hapo Rwanda kagame ameweka strategic future plan kwa kuwapa watu kazi kwa malengo fulani ukishindwa kutimiza una jitoa mwenyewe na mkataba unaishia hapo ngojeni mwone ndani ya miaka 5 ijayo i mean 2015 Rwanda hatuwafikii kwa vyote

 
hiyo namba ni free ama ndo mjanja flani kajiajiri wakati wa uchaguzi kwa kutumia mwamvuli wa hao wanasheria
 
Naomba kuwatahadharisha wenye vyama vya upinzani kuwa kazi sio rahisi kama inavyoonekana,nimeshtuka leo kusikia kuwa CCM ina wafuasi ambao wanapoteza kabisa njia za kampeni na kuingiza vitisho ambavyo sio fair,hawa wanasema mtu yeyote ambaye maisha yake yako safi ni kwa sababu ya CCM,hivyo ni bora ukachagua kipi bora uendelee kula kama leo au ujaribishe usiyoyajua na kwa bahati watu walio kwenye kundi la kuhamasisha % kubwa ni wasomi wakubwa.
Hii ina maana kama mama,baba,yako anaishi kwenye nyumba ya shirika,aliuziwa nyumba na serikali,nyumba ni ya serikali,anafanya kazi serikalini etc basi acha kuipigia CCM uone kitakachofuatia ikitoka madarakani. Nikajiuliza maswali mengi baada ya kuona watu hawa wametoka kwenye huo mkutano wamevaa kofia na scarf na tshirt za CCM.
Nikajiuliza je ni kweli wamekosa la kusema mpaka wanawatisha wanachi kwa njia hii???
Kwa hiyo si kweli kuwa watakaoipigia CCM ni wasiosoma,wengi hawasemi lakini wasomi ndio wa kwanza kuipigia CCM na %kubwa wana card either ya CCM au 2,IPO KAZI,VYAMA VYA UPINZANI VIKAZE BOOT.
 
Wapinzani ambao mnahusika na usimamizi wa kura maeneo yenye vyuo vikuu, naomba muwe makini. Kuna tetesi kuwa cCM watapandikiza apiga kura wakitumia vitambulisho hewa na majina ya wanavyuo walioondoka maeneo hayo.
 
Nami pia nimeipata hiyo hiyo. Wapinzani kuweni macho hapo kwenye vyuo!!!!!
 
Wapinzani ambao mnahusika na usimamizi wa kura maeneo yenye vyuo vikuu, naomba muwe makini. Kuna tetesi kuwa cCM watapandikiza apiga kura wakitumia vitambulisho hewa na majina ya wanavyuo walioondoka maeneo hayo.

Nyie mtaibiwa sehemu zisizo na fujo si unajua maeneo gani ya kistaarabu?
 
Wana JF;

Nimepata taarifa kutoka chanzo changu cha uhakika ndani ya Taasisi Nyeti inayofuatilia pia mchakato mzima wa Uchaguzi Mkuu 2010 ili kuhakikisha kuwa haki inatendeka na kuwa hakutakuwa na uchakachuaji. Hata hivyo Taasisi hiyo ambayo ni huru bado inaonekana imeshindwa kushughulikia kwa uhakika uchakachuaji unaondelea katika zoezi zima la uchaguzi ambalo bado linaendelea kugubikwa na vitendo vya rushwa na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi.

Baada ya salamu za kawaida alinijulisha kuwa masikitiko makubwa kuwa Uchaguzi umepamba moto na kuwa mafisadi wamejiandaa kuiba kura "zetu" mpaka inakatisha tamaa.

Ili kupata uhakika zaidi nilitaka kujua wataibaje kura wakati NEC wamesema kuwa haiwezekani kura kuibiwa? Nilishangaa sana aliponijibu kwa kujiamini kuwa Niachane na NEC na kuniuliza nilitegemea NEC waseme nini? Akaniambia kuwa Slaa anatisha kwa "Wanachachama". alinihakikishia kuwa ikishindikana kabisa "watavuruga" uchaguzi kwa kuhakikisha kuwa vituo vingine vifaa havitafika.

Niliingiwa na wasiwasi kidogo na kumwuliza ni vipi hasa wataiba kura kwa maana nadharia hiyo mbona ni ngumu. Nilimwomba anieleze kwa uhakika. Akionyesha kujiamini na kuwa na uhakika na kile anachoongea aliniambia kuwa "Kwanza wananunua kadi za kupigia kura, pia kuna karatasi feki zimeandaliwa kwa ajili ya kuzidisha kura kwa CCM"

Habari ndo hiyo. Kama CHADEMA wanasoma hapa basi wajiandae kwa kulishughulikia hili.

Naomba kuwakilisha!
 
Long time not seen Mkuu Allien!

Natumaini staili "uchakachuaji" wa kura waliozoe CCM imepitwa na wakati na ndiyo maana kwa sasa wanahaha!
 



Wadau, hayo mambo ya kuiba kura CHADEMA wanayajua sana na kwa sasa wana uzoefu nayo wa miaka 10 au zaidi. Wamejifunza Tarime, Busanda, Ubungo na kwingineko. Napenda kuwatoa hofu kwamba mawakala wa CHADEMA wamekuwa wakipewa elimu ya jinsi ya kulinda kura kwa zaidi ya miezi sita iliyopita. Hii imefanyika kwa njia ya kuwagawia CD zilizorekodiwa maelekezo muhimu, semina elekezi na kadhalika.

Silaha kubwa ya Watanzania ni kupiga kura kwa wingi na bila kukatishwa tamaa na wasiwasi wa kuibiwa kura. Sheria ya Uchaguzi inaruhusu wapiga kura kukaa umbali wa mita mia moja toka katika kituo walichopigia kura wakisubiri matokeo ya kura hizo.

Tarehe 31 Octoba PIGA KURA, LINDA KURA YAKO!
 
wanajaribu kuwatia hofu wapiga kura tu safari hii hawana lolote, wanakufa huku wanajiona hao
 

Hapo ndo pakutilia mkazo na msisitizo
 
kama hiyo tuhuma itakuwa kweli basi itakuwa imeshakula kwa upande wa haki na demokrasia.
 
kwa walio wengi tunakumbuka habari hii iliyowekwa wiki tatu zilizopita.
1. poleni na harakati za kuikomboa nchi yetu!
Leo napenda kuwajulisha mikakati michafu ya kupora na kuzuia maamuzi ya umma yanayofanywa na ccm kwa uratibu wa usalama wa taifa. Baada ya kubaini dalili za kuanguka vibaya katika uchaguzi wa mwaka huu idara ya usalama wa taifa imeandaa mikakati ya kuiba kura ili kuzuia chadema msiingie ikulu. Mikakati hii inaeleweka vizuri kwa tume ya taifa ya uchaguzi ambayo inashirikiana bega kwa bega na idara ya usalama wa taifa kumtengenezea jk ushindi bandia wa 80%. Wana hakika watanzania watagundua wizi huo na watakataa matokeo ndiyo maana kwanza waliwatumia viongozi wa dini waliotembelea makao makuu ya chadema wawasihi chadema wakubali matokeo yatakapotangazwa na juzi wamelitumia jeshi kutisha wananchi watakaoamua kupinga matokeo ya kupikwa yanayoandaliwa na nec/usalama wa taifa. Majid kikula ambaye ni government security officer ndiye mratibu wa zoezi la kuiba kura, ni mtaalamu aliyebobea katika kazi za aina hii aliratibu vizuri zoezi kama hilo mwaka 2005. Pia mwaka 2007 alitumwa kenya kwenda kumsaidia kibaki kupora ushindi wa odinga.

Kikula anatumia muda wake mwingi hivi sasa ofisi za tume ya uchaguzi kwa ajili ya uratibu wa uvurugaji daftari la kudumu la wapiga kura akiifanya kazi hiyo kwa karibu na baadhi ya watendaji wa nec na maafisa kadhaa wa usalama wa taifa kutoka kurugenzi ya IT ya idara ya usalama (DITA) ambao wako ndani ya nec kwa zaidi ya miezi sita sasa, nitawapatia majina yao. Pia kuna vijana wataalamu wa IT waliochukuliwa kutoka maeneo mbalimbali wamepewa nyumba upanga mtaa wa undali shughuli kubwa wanayofanya ni kuandaa utaratibu wa ku-access remotely daftari la kudumu la wapiga kura. Hawa wanafanya kazi chini ya salva rweyemamu na mindi kasiga kutoka kurugenzi ya mawasiliano ikulu. Wapo vijana kadhaa leo nawapa majina ya wawili; maharage chande na edgar masatu wanafanya kazi kwa karibu na nzowa wa idara ya usalama ambaye ndiye aliyeratibu shambulio la kumwagiwa tindikali kubenea. Pia kuna kundi linalojumuisha wataalamu wa printing wa kiwanda cha uchapaji cha usalama wa taifa kilichopo MALINDI ambao hivi karibuni walikuwa mjini tanga kwa semina fupi ya jinsi ya kughushi kura kupitia fake ballot paper, timu hii inaongozwa na ndg SINYAU.

Kwa hiyo utaona kwamba imeandaliwa mikakati mingi kuufanikisha uovu huo ili mmoja ukikwama basi mwingine utatumika ila wameamua ni lazima jk ashinde kwa 80%. Ndani ya idara ya usalama wa taifa maafisa wengi wamechoshwa na uongozi mbovu wa ccm hivyo wanataka mabadiliko ya uongozi idara imechukua hatua kadhaa kuhakikisha maafisa wote wa idara wanampigia kura jk, wote wameagizwa kuwasilisha vitambulisho vyao vya kupigia kura ili vinakiliwe namba ili atakayepigia upinzani afukuzwe kazi baada ya uchaguzi. Fuatilieni kwa karibu haya niliyowaeleza nimeyapata kwa nafasi yangu ndani ya tiss. Huyu KIKULA mfuatilieni kwa karibu ni hatari. HAKIKISHENI DUNIA NA WATANZANIA WOTE WANAJUA MAPEMA HILA HIZI. Jambo la kujiuliza maafisa usalama wa taifa wanafanya nini ndani ya tume ya uchaguzi wakati huu.

Huu mpango umefikia wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…