Wote waliomtukana Shaffih Dauda kuhusu suala la Mo wamuombe radhi haraka sana

Pole yako ukitoa ligi ya mbigwa Afrika mgawanyo wa gate collection kwa mechi zote msimu mzima ligi kuu Tanzania bara simba kapewa 451,860,000/= yanga 415,620,000/=
 
Kwahiyo hata simba walivyomfunga as vita, al ahly na js soura hakuandika
 
Ila ni mikia mwenzenu na anafanya hivyo baada ya kumnyima kacheo fulani pale matopeni.mengine anaandika kweli kama la juzi ila mengine kwakweli anawaonea sana nyie mbumbumbu fc, Sisi wananchi anatuogopa maana amewahi kula makofi alipojaribu kuingilia nakusema vibaya bingwa wa muda wote Tz.

Siku moja mpeni hata makonzi tu ataacha ,anawaonea sana
 
Pole yako ukitoa ligi ya mbigwa Afrika mgawanyo wa gate collection kwa mechi zote msimu mzima ligi kuu Tanzania bara simba kapewa 451,860,000/= yanga 415,620,000/=
Wewe huelewagi ndio maana nakukosoaga kila pahala kuanzia kwenye matamthilia yako hadi kwenye uzi wq AFCON.

Simba sports msimu uliopita kwenye mashindano yote imekusanya Billion 5.
Mechi karibu zote zilizohusisha Simba ukiachilia alizocheza uhuru na timu za daraja la kati ndizo hazikuwa na mashabiki wengi zingine zote ziliingiza million 300+ .

Note. Hizi fedha zilikuwa zikinufaisha sana timu za ugenini kutokana sheria mpya za TFF.

Sasa nitajie timu iliyoingiza hata 2 billion msimu uliopita
 
Mpira bila uwekezaji hakuna kitu ni kama yanayowakuta Arsenal wanatafuta viporo. Simba kama wameridhika katika kushindana league ya ndani sawa tu wanaweza kumudu maana wote ni njaa tu ila kama malengo ni kutawala ndani na nje basi ndoto huwezi kufika huko team ikiendeshwa katika vibaraza vya kahawa. mpira ni biashara na biashara ni makubaliano sasa kama unaweka mkataba na mtu si unaweka terms ili mmoja asipotimiza katika makubaliano mkataba unavunjwa. Ukweli ni mchungu hizi team 2 kubwa zitakuja kufa kifo chakina Leopard siku mikoani wakiamka na kusupport team zao kuacha na ujinga wa kusupport haya ma team mawili.
 
Ipo siku yake tu,anakujazieni wachezaji wenye mishahara mikubwa kwanza ili akitoka mnyooke
Sasa si ndo vizuri mwacheni atujaze wachezaji wenye mishahara mikubwa ili akiondoka tunyooke....sasa nyinyi washabiki wa gongowazi mbona mnafurahia mnataka aondoke sahivi...c mpige kimya. Or hampendi tuje tunyooke
 
Mimi wala sina tatizo nawewe ila kama umesoma komenti yangu nimesa ukiondoa mapato ya club bigwa barani Afrika simba imekusanya milioni 450+. Pia mambo ya tamthilia achana nayo maana mm pengine ni mutu pekee naye fatilia mambo yote duniani kiasi Kwamba akuna sehemu yoyote unaweza nidanganya kuanzia siasa za ndani,nje, uchumi, michezo na burudani mpaka Utamaduni. Sehemu pekee utaniacha njia panda ni ulonzi full stop.
 
Naomba uweke pia imetumia kiasi gani usijekuta hela hizo zimeishatumika kugharamia timu pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…