Would you marry me?

Nilisahau jambo muhimu sana.I would marry you Mwali as long as we dont fight imperfection too much,being real is enough.
 
hii kitu ni too theoritical yan ukienda practically ndio hao kila siku wana malalamiko.
hapo ninakubaliana na ww ni bora mkawa hamtofautian saana hapo mwaweza cope yan.
 
kuna points nyingi nzuri sana ndani ya huu uzi na it seems people know a lot of stuff...but, surprisingly enough, the more watu wanavyozidi ku-analyse na kudadavua haya mambo ya mahusiano, ndoa n.k, the more elusive and unattainable they become na kufanya watu wazidi kuwa confused na kutopata fulfillment wanayoitarajia.... it may need something not less than divine intervention kuweka haya mambo sawa kiukweli
 
Hili suala kwa mtizamo wangu linaweza kuwa very complicated kama mtu akiamua hivyo na linaweza kuwa very simple kama ukiamua hivyo

Nasema hivyo kwa sababu, wakati mwingine tunakuwa too idealistic when it comes to issues za reality kwenye maisha. Mfano kwenye ndoa....huu usemi wa 'wife material' na 'girlfriend material' wenyewe uko flawed kwa sababu if anything, unamweka mwanamke katika nafasi ya mtu wa 'kupokea amri, maelekezo, mtiifu, asiye mbunifu, asiyeweza kuhoji, asiyependa/takiwa kwende kusocialise ' nk. Na girlfriend material vice versa

Nikimnukulu Mwali, "Wife material ni mpole, mtiifu, ana background nzuri, ni msomi kiasi, future oriented etc. Girlfriend material ana sura na umbo nzuri, ni mcheshi, anapenda kwenda out, ni mtundu kiasi."

Kitu cha kwanza ni kuondokana na hiyo dhana.

Kama walivyosema baadhi hapo juu, kwangu mimi mke pia ni girlfriend na ni "nyumba ndogo" , mhudumu wa bar, trafiki, etc in her own right. Inategemea na mazingira...wapi, wakati gani, kwa namna gani! Hivyo ni muhumu saaaana kupata mke/mume ambaye ni FLEXIBLE kulingana na mazingira ili aweze kucope na hali mbali mbali zinavyojitokeza.

Hivyo basi, Mwali mpwa wangu, be yourself. Kama unapenda kwenda club, na any other social activities za girlfriends, zifanye. Kama pia wapenda kuact kama 'wife material' then be...ILA tu usipretend kwa sababu hii ndo number one killer ya mahusiano yoyote yale. Ukiishi kama wewe, utampata ambaye atapenda maisha yako yalivyo, na wewe utayapenda.

Nikikunukulu tena,
Hapo Bold sio entirely true, tutake radhi, watu wengine kwetu beer tumezaliwa nazo an yet ni perfect husbands (sio kwamba najisifu hapana, ngoja ODM aone hapa)

Hapo Red, Hakuna haja kwa sababu the whole thing IMO is flawed. Hapo blue, uko sahihi ila niongezee tu kwamba ni hatari sana kuzungumzia "perfect spouses" watu mliokutana ukubwani...perfect hapo must be very relative. Kuwa spouses kuna sacrifieces na tolerance ya hali ya juu.
Hapo rangi ya magamba, thats the way it is supposed to be (normatively).

Baada ya kusema hayo, Mwali naomba chai sasa....koo limenikauka kidogo.:A S-coffee:
 
Baki kama ulivyo, akikuchagua hivyo hivyo poa kama hajataka his loss

Nakubaliana na G kwenye hili, hakuna haja ya kujibadili ulivyo....hakuna kitu kizuri na chenye amani kama kujikubali ulivyo na kuwa ulivyo....na nina hakika kuna mtu anatakupenda wewe ulivyo....nachokiona pia ni kuwa watu hubadilika kwenye baadhi ya characher huko mbeleni,sijui sasa mabadiliko hayo watayamudu vipi kama waliangalia tofauti za wife bf na hubby....Let love and commitment lead.

If i were boy n not you sisy, I would Marry you my Mwali....lolest!
 

Kaizer ukitulia nakukubali sana.... perfect adviser, perfect mume,perfect friend...lol
 
hii taasis ya ndoa mwaya ni pasua kichwa haswaa haina shukran.
dont take marriage too serious, make funny out of it and then enjoy.
NB: Usitegemee makubwa sana uko ndoan, expectation ndio zinazowaponza watu jua mumeo/ mkeo sio malaika lololte laweza kutokea.
cheerz.
will me you mwali n take u as u are.
 
Mmeisha ambiwa na mungu msiwe na uhusiano nje ya ndoa.....haya mambo ya gf/bf ni mambo yalio letwa na wendawazimu....yani mimi nikisikia mwanume au mwanamke anasema na gf/bf najua ni kichaa tu.

Mara nyingi sana hao walio anza utaratibu wa kuwa na ma gf /bf ndo ndoa zao hazidumu, mana walisha enda nje ya nidhamu na ukisha toka nje ya nidhamu....vigumu kurudi kwenye line....itabidi waendelee tu kuwa na gf/bf hata kama wameoa au wameolewa :biggrin:
 

We nawe unashangaza!!
Kwahiyo unataka watu wakutane na kuoana siku hiyo hiyo? Au we ukisikia Girlfriend/Boyfriend basi akili yako yote inakimbilia kwenye ngono?
 
We nawe unashangaza!!
Kwahiyo unataka watu wakutane na kuoana siku hiyo hiyo? Au we ukisikia Girlfriend/Boyfriend basi akili yako yote inakimbilia kwenye ngono?
Lizzy mimi sjasema uende kama kipofu ukaowe/kuolewa hata mungu anasema owa/olewa sehemu ulio penda....Lizzy mwanaume mpaa afike kwenye hatua ya kukupenda ujuwe kisha tazama hatua zako kwa mbali sana na wewe hujui....wanaume wengi wanatafuta excuse ya kuwadanganya watoto wa kike tu eti wanavuta time mpaa akujue vizuri.


Akujue vizuri kwa nmana ipi?

Afu na mwanamke lazima utazama reputation yako, unataoka na mwanaume kwa mda gani mpaa akujue tabia yako? Ok mmetoka afu badaye kakuwacha kwenye mataa nani atasema hujapendana na yule mwanaume au nani atakataa hata kama yule mwanaume atasema ka sex na wewe.

Afu badaye mnakuja sema wanaume washenzi....washenzi nyinyi wanawake manoa toka na mwanaume ambaye hakuhusu wala huna uhakika kama atakuwa mme wako siku za mbele.

Wkeni akili...mwanaume akipenda hata kusema nakupenda anaona anapoteza wakati tu....anaona bora akibie mbio mbio kwa wazazi wako akapose...kabla ya jamaa wengine hawajamuwahi...lakini hao wakusema ohh sweet ngoja tuvute time wewe unijue na mimi nikujue mwambie sawa...lakini kujunaa sio kutoka nje pamoja kila siku....wewe nichunguze kwa wanao nijua na mimi nikuchunguze kwa wanao kujua na haichukui time....mana kumjua mtu unaweza kumjua hata kwa siku moja ukapata details zake zote kwani duniani kuna siri....Kwenye nia hapakosi njia akitaka kuoa ataoa na atakuchunguza mpaa saa ngapi unalala na wewe hujui kwa week moja tu atakuwa na full details na wewe mwanamke utakuwa na full details za mwanaume anaye taka kukuoa.


Najua hapa kuna wanaume watakasirika kwa kuwa na wapa akili :biggrin:
 
Kama ni hivo sasa kwa nini wanawake wanadondokea wanaume wenye mambwembwe na wanaume wanadondokea wanawake watundu watungu katika uhusiano wa boyfriend girlfriend? Sio wote lakini
 
Baelezee sissy... na ndio maana mi nimeleta hili swali hapa. Ni kama you can read my mind yaani.
 
Pamoja na kua umesema ukweli fulani mi sijaongelea wale wanao olewa sababu ya presha ya miaka kupita au kijicho cha jamii. Naongelea wale wanao ingia katika mahusiano huku wakijua kabisa huyu hapa ni sawa kwa kua boyfriend au girlfriend, ila nitakapo taka kuoa au kuolewa nitatafuta mngine...
 
Afu badaye mnakuja sema wanaume washenzi....washenzi nyinyi wanawake manoa toka na mwanaume ambaye hakuhusu wala huna uhakika kama atakuwa mme wako siku za mbele.

Najua hapa kuna wanaume watakasirika kwa kuwa na wapa akili :biggrin:
Mimi mmoja nimekasirika kwa hiyo lugha uliyotumia kwenye red.
:focus:Labda nianze na kuelezea vile maisha yanapokuwa kabla na baada ya ndoa.
Wakati wa u-bf/u-gf:
- Kila mmoja anaishi kwao/kwake (hamko chini ya paa moja masaa 24). Katika kipindi hiki, kuonana yenu inakuwa ya nadra na kupanga. Kunakuwepo na maandalizi japo madogo kabla kuonana - nitoke vipi, niji-behave vipi, tuonane wapi (nisionekane). ME hata kama kachacha, siku hii atajipigapiga; KE atafanya aonekane asivyoonekana.Kila mmoja atataka aonekane mzuri, nje kimwonekano na ndani kitabia.
Mnapoishi pamoja, iwe kwenye ndoa au kukaa pamoja tu.
- Kwanza ile hali tu ya kuwepo pamoja tu 24hrs a day, 7days a week, all the time inabadilisha kila kitu, (hapa simaanishi kuwa hakuna anayeondoka alipo lakini katika masaa 24 ya siku angalau saa 6-8 mtakuwa pamoja). Hakuna tena kujiandaa uonekane vipi, kila mmoja anakuwa kama aivyo katika uhalisia wake, ambavyo mwenzake hakuwahi kumwona kabla ya kuishi pamoja. Zile caring, worrying, treating, listening, behaving...za wakati wa u-bf/-u-gf zinaanza kuyeyuka. Zile samahani zilizokuwa zinatolewa bure, mfano alipokuwa gf/bf unapiga simu imezimwa, hapatikani anazungumza dkk 30 saa moja badae unaambiwa nilikuwa mkutanoni, niliweka silence, iliisha chaji; ule uongo au kweli wa kuwa leo ninaenda kumwona shangazi, wiki ijayo nitakuwa mkutanoni... unaamini kila kitu bila ya maswali wala masharti; lakini mkiwa pamoja unaanza kuzidadisi, kuomba maelezo kamili, na pengine kutilia shaka.

Suluhisho
- Tuwe kama tulivyo wakati wa u-bf/u-gf. Usijaribu utake kuonekana vyengine na kujenga picha ambayo iko siku "itaungua" na kubaki "negative". Ikiwa atakukubali kama ulivyo leo na mkakubaliana iwe hivyo, atakayedai ziada anajitafutia presha za bure.

- Ndoa/kuishi pamoja ni ahadi na wajibu, timiza; ni haki, itoe; ni kuvumiliana, vumilia; ni kusamehe, samehe; ni kupenda na kuheshimiana, penda na heshimu ili nawe upendwe na kuheshimiwa.

- Ingawa wengine wanaweza kukataa, nahisi ule mvuto wa siku/miaka ya nyuma; zile nilizozitaja hapo juu: caring, worrying, treating, listening, behaving...zinaweza kufa kidogo kidogo kama hamkuzidumisha kwa maneno na vitendo; yale mapenzi moto moto yanaweza kufifia kidogo kidogo. Na sio kwa sababu hampendani wala hamtakani, lakini hamna wakati wa kutosha kama mlipokuwa mnaishi mbali mbali. Lakini kama alivyosema Lizzy, basi nobe ndani ya saa 24 unashindwa hata kumega saa moja ya kuwa na mpenzi wako ya kuishi mkajikumbusha na kutenda yale yaliyokuwa yanawapagaza mlipokuwa gf/bf?
 


Naweza nikasema kua kitu ambacho wanawake wengi tunakosea ni ile kuchagua kua kati ya a hot crazy chic na a decent lady.... Wanasahau ama wanashindwa tambua kua you can be both, yooote kutegemea na timing. Daima as a woman or lady strive to be something your man is proud of katika mazingira yoyote yale.

The secret in all this ni wewe mwanamke kutambua kua wewe ni mwanamke, kua proud kua wewe ni mwanamkea na play your role as a woman beside your man. Mwanaume atoke nje kwa tamaa zake, ama maybe tu imetokea bahati mbaya au maybe tu hamjablend, lakini sio sababu eti kukudefine wewe ni wife material hufai. You as a woman inabidi ukiwa nyumbani be a Great Wife and Mama, na ukiwa na your man mtaani mpaka wenzie waulize "Is she your gal friend/nyumba ndogo?" Nakubali na najua ni ngumu.... But it is possible.
 

Duu hii ni staili mpya ya kutafuta mchumba kila la heri mwali...sali sana mungu yu pamoja nawe,...
 
Nashindwa kuamini kua such an descriptive analysis iliishia hapo... twambie how do we overcome this then? tunafanyaje to keep the flame alive?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…