changaule
JF-Expert Member
- Jan 10, 2020
- 6,039
- 10,151
Baada ya kupangwa kwa droo ya robo fainali ya klabu bingwa Wydad dhidi ya Simba, kila mmoja aligeuka mtabiri wa mabaya kwa Simba kwa kuona kuwa watayaoga magoli mengi. Lakini ukiangalia reference wanazotumia kujiaminisha hilo ni zile za nyuma kabisa kwanzia mechi ya Rivers kurudi nyuma. Wameshindwa kuchukua kiwango cha Wydad kwasasa ili kufanya mlinganisho wa ubora wa timu.
Wydad kacheza vs As Vita na kuambulia goli moja hapo Morocco na pia vs Petro Luanda kaambulia goli moja pekee, ushindi wao mkubwa kwenye hatua ya makundi akiwa nyumbani ni vs Kabylie akiwa kwao Morocco na ulikuwa ushindi wa kubebwa tu.
Binafsi niliwapa asilimia kubwa ya Simba kufuzu hatua inayofuta lakini haikuwa bahati kwa Simba wamepoteza mechi mara mbili; ya kwanza ni kushindwa kushindwa kuzitumia zile nafasi za wazi kwa Mkapa na la pili ni kushindwa kutulia kwenye upigaji wa penati. Mimi niliona Wydad ndio walikuwa na wakati mgumu kifikra na niliona hadi wachezaji wa Wydad wakiwa wanalia hawakuamini kama ndio bye bye wakiwa kwenye ardhi yao lakini wachezaji wa Simba hawakuweza kutumia advantage hiyo.
Kuelekea mechi ya nusu fainali naona dalili ya hawa Wydad kudharirishwa na Mamelod. Finishing ya Wydad ni mbovu, viungo vyao hawawezi kutengeneza penetration pass za magoli, jana kuna wakati wachezaji wa Simba walikuwa wanafanya makosa ya wazi yaliyopaswa kuadhibiwa lakini walishindwa kutumia makosa hayo. Wydad kama watakuwa wanacheza hivyo kama kwenye group stage na robo fainali basi watatolewa na Mamelod.
View attachment 2603352
View attachment 2603354
Wydad kacheza vs As Vita na kuambulia goli moja hapo Morocco na pia vs Petro Luanda kaambulia goli moja pekee, ushindi wao mkubwa kwenye hatua ya makundi akiwa nyumbani ni vs Kabylie akiwa kwao Morocco na ulikuwa ushindi wa kubebwa tu.
Binafsi niliwapa asilimia kubwa ya Simba kufuzu hatua inayofuta lakini haikuwa bahati kwa Simba wamepoteza mechi mara mbili; ya kwanza ni kushindwa kushindwa kuzitumia zile nafasi za wazi kwa Mkapa na la pili ni kushindwa kutulia kwenye upigaji wa penati. Mimi niliona Wydad ndio walikuwa na wakati mgumu kifikra na niliona hadi wachezaji wa Wydad wakiwa wanalia hawakuamini kama ndio bye bye wakiwa kwenye ardhi yao lakini wachezaji wa Simba hawakuweza kutumia advantage hiyo.
Kuelekea mechi ya nusu fainali naona dalili ya hawa Wydad kudharirishwa na Mamelod. Finishing ya Wydad ni mbovu, viungo vyao hawawezi kutengeneza penetration pass za magoli, jana kuna wakati wachezaji wa Simba walikuwa wanafanya makosa ya wazi yaliyopaswa kuadhibiwa lakini walishindwa kutumia makosa hayo. Wydad kama watakuwa wanacheza hivyo kama kwenye group stage na robo fainali basi watatolewa na Mamelod.
View attachment 2603352
View attachment 2603354