Xavi Hernandez Vs Andres Iniesta

Xavi Hernandez Vs Andres Iniesta

Christopher Wallace

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2015
Posts
1,479
Reaction score
3,788
Tumalize utata, unamkubali nani hapo kati ya hao mafundi wawili mahiri kuwahi kutokea katika akademi ya La Masia?
2732242_heroa.jpg
 
Wote ni mafundi sana na ni marafiki sana walifika kipindi hawataki kulinganishwa !!
Combination yao yuko Messi,Xavi na Iniesta hawa hata ukimuambia mmoja tuzo fulani amuachie mwenzake hatasita hata kidogo!!
Kama unakumbuka Xavi hua anataniwa "Messi deserves to win it" kwa sababu kila anachoulizwa hao ndio walikuwa wanataka walete balaa la Messi aichezee Spain ilibakia kidogo..

!!
 
Inategemea sana na mchezo, lakini kwangu Xavi ni bora zaidi kwa kuwa alikua anafungua zaidi mchezo, alikuwa hakai sana na mpira na anafungua both sides so anafanya ukuta ufunguke zaidi tofauti na iniesta anatafuta weak point awe ana-penetrate na mpira mwenyewe.
Nafikiri ndo maana after xavi kusepa umeona barca wamepunguza sana pasi nyingi sasa hivi wanatumia uwezo wa mmoja mmoja kupenya ukuta wa mpinzani!
Timu sasa hv inajengwa kutokea kwa MSN tofauti na kipindi cha Xavi timu ilikuwa inajengwa tokea kwake
 
Iniesta nihatari kuliko xavi, xavi mtoa pasi ila iniesta anatoa pasi na anafunga.
Kwa hakika wote ni mafundi sana. Kinachomfanya Iniesta afunge zaidi ni eneo analocheza, Xavi alikuwa anaituliza timu vizuri sana kutoka na uwezo wake mkubwa wa kumiliki mpira na pasi kiasi kwamba mapungufu waliokuwa nayo kina Pique yakawa hayaonekani, kuondoka kwake kumechangia sana Barcelona kudhoofika. Xavi ni pengo lisilozibika kwa urahisi.
 
  • Thanks
Reactions: GUI
Kwa mimi Xavi ata wangekua watatu, hawanitishi kwakuwa akili ya xavi ni pass zaidi ila Iniesta huyu ni mtu hatari sana akiwa na mpira alafu anakuja golini kwako, maana anatizama pandezote na anatoa pasi, anauwezo wa kujitengenezea nafasi yeye mwenyewe na kufunga kwaujumla huwezi jua anatakakufanya nini.
 
wewe renzo daudi huyu zaviiiii alikuwa anapiga pasi kushinda timu pinzani hatari manchester united baada ya dakika 90 walikuwa wamepiga jumla ya pass 400 zaviii peke yake alipiga pass 800 wenyewe mtatoa majibu
Hahaaaaaa
 
Iniesta nihatari kuliko xavi, xavi mtoa pasi ila iniesta anatoa pasi na anafunga.
Kuna style flani alikuwa qnakimbia na Mpira kwenye chaki, aside hawa watu ni mafundi sana!!!
Barcelona waache ujinga watuletee wachezaji wamaana daahh ilikuwa raha sana kuiangalia barcelona!!!
 
Back
Top Bottom