Ya Morrison yalivyompofusha Fei Toto

GANA BANKS

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2020
Posts
608
Reaction score
872
Maoni ya mdau kuhusu sakata la Feisal na Yanga SC.

YA MORRISON YALIVYOMPOFUSHA FEI TOTO

Kulikuwa kuna upuuzi wa aina mbili katika kesi ya Feisal; kuamini mawakili wa Morrison wangeshinda kesi ya Feisal kama walivyoshinda kesi ya Morrison na upuuzi wa pili na kuamini Feisal alistahili kudai haki yake.

Kesi ya Morrison na Yanga ilikuwa ni kuangalia kama mkataba aliosaini na Yanga ulikuwa halali au sio halali baada ya mkataba wake wa awali kutamatika. Kesi ya Feisal na Yanga ilikuwa inafanishwa na ya Morrison wakati Feisal ana mkataba halali na Yanga tena mkataba wa miaka miwili. Huu ulikuwa ni upuuzi uliopewa uhalali na wachambuzi.

Upuuzi mwingine ni ule wa kudhani eti Feisal alikuwa sahihi kudai haki yake. Haki ipi? Alikuwa halipwi mshahara waliokubaliana? Alikuwa hapati nafasi ya kucheza? Aliposaini mkataba alisaini akiwa amelewa au alilazimishwa kusaini mkataba? Kama halikuwepo moja kati ya hayo basi mkataba wa Feisal ulikuwa ni halali.

Kuna hoja za eti Yanga walipaswa kumlipa zaidi Feisal baada ya kuona kiwango chake kimepanda. Hapa Kuna mambo mawili ya kujiuliza; kiwango cha Feisal Salumu kilipopanda hakukuwa na mchango wa Yanga katika kukuza kiwango hicho? Kwanini Yanga haifikiriwi namna ilivyowekeza kwa mchezaji huyo mpaka akafika hapo alipofika?

Yanga walimgharimia vitu vingi zikiwepo bonus na benchi bora la ufundi na kambi nzuri mpaka Feisal kuwa hivyo alivyo na ndio maana wachezaji waungawana hushukuru timu zao wakiwa katika ‘peak’ badala ya kufanya alichofanya Fei Toto.

Swali la pili, ni wapi katika mkataba wa Fei Toto kuna kipengele cha kuongezewa mshahara ikiwa kiwango chake kitapanda? Yanga wana uhalali wa kumtumia Feisal bila kuboresha mshahara wake mpaka mkataba utakapoisha na hakuna dhambi yeyote ile.

Yanga kutoboresha maslahi ya Feisal ili kumuongezea mkataba ni kwa hasara yao wenyewe kwa sababu mchezaji akimaliza mkataba ataondoka bure klabuni kwake lakini leo imekuwa kituko kwamba Yanga kutoboresha mkataba ni kosa. Sijui ni uchambuzi wa namna gani ulitumiwa na baadhi ya waeledi wa soka.

Sadio Mane hakuboreshewa mkataba wake pale Liverpool na Mane hakuondoka Anfield bali alitulia na kuitendea mema klabu yake mpaka mkataba ulipokwisha akagoma kusaini mkataba mpya na akaondoka zake kwenda Bayern Munich. Haikuwa dhambi.
 
Kama kusajili mchezaji mzuri na kuwa kiwango ni utumwa basi asajiliwe Shilole, Tausi Likokola na Juma Lokole muwakuze nao viwango. Heshimuni vipaji. Hakuna kiongozi wa yanga hata mmoja waliopo aliepata kushika mimba. Sasa mngemzaa mngesemaje.
 
Kama kusajili mchezaji mzuri na kuwa kiwango ni utumwa basi asajiliwe Shilole, Tausi Likokola na Juma Lokole muwakuze nao viwango. Heshimuni vipaji. Hakuna kiongozi wa yanga hata mmoja waliopo aliepata kushika mimba. Sasa mngemzaa mngesemaje.
Yani wewe Mmatumbi wa Mchambawima ndiwe unayeheshimu vipaji saaana vya Wachezaji ilihali Mchezaji mwenyewe hakushikiwa bunduki kulazimishwa kusaini mkataba wa kuichezea Yanga FC hadi May 2024?

Kumbe ile methali ya "Pili pili usiyoila inakuwashia nini inatakiwa ijengewe sanamu".
 
Jamaa katema sana madini aisee

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Lipeni pesa, mpira pesa kwanini kila siku ninyi tu.KAMBALE KATOKA BWAWANI KIGAMBONI JUZI.
 
Mdau ameongea point tupu. Nakala iwafikie mbumbumbu popote walipo.
 
Ni hoja mujarabu kwa wenye akili peke yake ndio wataelewa lakini kwa wale mbumbumbu watatoka kapa kama kawaida yao
 
Fei alijua bado Yanga kuna akili mbili tuu kumbe kwa sasa zipo 4 hivi...apambane nao kweli kweli la sivyo naona anaenda kupotea.
 
Fei alijua bado Yanga kuna akili mbili tuu kumbe kwa sasa zipo 4 hivi...apambane nao kweli kweli la sivyo naona anaenda kupotea.
Hawezi kupambana tena hapo aombe busara tu zitumike vinginevyo anakwenda kuumia.
 
Fei alijua bado Yanga kuna akili mbili tuu kumbe kwa sasa zipo 4 hivi...apambane nao kweli kweli la sivyo naona anaenda kupotea.
Kumbe wamefika wa 4 [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kule kwingine bado wote ni mbumbumbu
 
Kumbe wamefika wa 4 [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kule kwingine bado wote ni mbumbumbu
Mbumbu sio tusi mzee..umbuumbu huwa kwa muda yani hujui kitu fulani...ila kwa sasa ww unaona nani hajui kule Simba 😎 😆😆
 
Fei anahofia pindi mkataba utakapoisha, Je kiwango chake still kitaendelea kuonekana???

Mane hakua na wasiwasi, anaamini kiwango chake, akaamini mkataba utaisha na Kuna siku atapata mkataba mzuri zaid.

Pole sana bwana Fei.
 
Ninachoona ni watu walishapiga deal Kwa Feisal wakijifanya mawakala. Wanajifanya kushinikiza hukumu Kwa vijineno vya kuchombeza mara wanasiasa wanashinikiza hukumu mara blah blah.
 
KAMA KUSAJILI MCHEZAJI MZURI NA KUWA KIWANGO NI UTUMWA BASI ASAJILIWE SHILOLE, TAUSI LIKOKOLA NA JUMA LOKOLE MUWAKUZE NAO VIWANGO.HESHIMUNI VIPAJI.HAKUNA KIONGOZI WA YANGA HATA MMOJA WALIOPO ALIEPATA KUSHIKA MIMBA.sasa mngemzaa mngesemaje.
umepagawa na mrejesho wa TFF huna lolote,km kushika mimba ndo ishu angakaa kwao yeye kiungo mama yake beki baba yake mshambuliaji ingekuwa ize kuunja mkata kwa style ile
 
umepagawa na mrejesho wa TFF huna lolote,km kushika mimba ndo ishu angakaa kwao yeye kiungo mama yake beki baba yake mshambuliaji ingekuwa ize kuunja mkata kwa style ile
dem boy, Mwanadamu hafugiki ooh tumemkuza tumemkuza.Zaeni wa kwenu.
 
Binafsi, nikiwa kama shabiki wa Yanga, nasupport jamaa auzwe.

Hata wakishasettle ili swala, basi Yanga watangaze dau, then hao wanaomtaka, wamchukue.
 
Fei anahofia pindi mkataba utakapoisha, Je kiwango chake still kitaendelea kuonekana???

Mane hakua na wasiwasi, anaamini kiwango chake, akaamini mkataba utaisha na Kuna siku atapata mkataba mzuri zaid.

Pole sana bwana Fei.
Kiustaarabu angeweza kupeleka ombi kwenye management kwamba kuna timu imepeleka offer kwake then uongozi ungeona ni kwa namna gani unaweza kuboresha maslahi yake au hiyo timu ije ifanye mazungumzo na uongozi ili anunuliwe rasmi
 
Binafsi, nikiwa kama shabiki wa Yanga, nasupport jamaa auzwe.

Hata wakishasettle ili swala, basi Yanga watangaze dau, then hao wanaomtaka, wamchukue.
Sure
Hawezi kuwa sawa tenaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…