Tatizo watu hamjui hesabu. Ni kwamba ni kawaida kwa nchi masikini sana kuongoza kwa ukuaji wa uchumi. Mathalan ukiwa na sh.100 na mwingine akawa na sh. 1000 halafu yule mwenye sh. 100 akazalisha sh. 20 ina maana tayari amekuza kipato chake kwa 20%. Kwa upande mwingine yule mwenye sh 1000 ikiwa atazalisha sh. 100 atakuwa amekuza kipato chake kwa 10% tu. Hivyo basi ni kawaida kabisa nchi masikini sana kama tz kuwa miongoni mwa nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi. Jambo la msingi ni kujiuliza je, ukuaji huu wa uchumi unachangiaje kuondoa/kupunguza umasikini? Hapa tunazungumzia jinsi economic growth inavyoweza kuleta economic development na poverty eradication. Kwa hiyo sio jambo la kujivunia sana kwamba uchumi unakuwa ilihali rahisi wenu alishakiri kwamba hajui ni kwa nini tz ni masikini.