Yaelekea kuna mkanganyiko wa ufahamu baina ya wale wanaosema Tanzania ni nchi maskini na wale wanaosema ni nchi tajiri

Yaelekea kuna mkanganyiko wa ufahamu baina ya wale wanaosema Tanzania ni nchi maskini na wale wanaosema ni nchi tajiri

Status
Not open for further replies.

Sijali

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
2,672
Reaction score
1,814
Yaelekea kuna mkanganyiko wa ufahamu baina ya wale wanaosema Tanzania ni nchi maskini na wale wanaosema ni nchi tajiri. Wote hawakukosea. Makosa yapo katika kinachokusudiwa.

Miaka yote ya uongozi wa Mwalimu Nyerere alikuwa akisema Tanzania ni nchi maskini. Wakati mwingine alisema bara zima la Afrika ni maskini. Mwalimu alikuwa kwa kweli anajua maana ya utajiri.

Mtu huwezi kuwa tajiri hadi hapo utajiri uweze kuufasiri katika ubora wa maisha yako ya kila siku. Mfano mzuri ni ndugu zetu Wamasai ambao baadhi wana ng'ombe elfu kumi, lakini kutokana na kushindwa kufasiri utajiri huo kwenye maisha yao ya kila siku, watu hao ni maskini.

Sasa ninakuja katika hizi kauli za siku hizi kwamba Tanzania ni tajiri, hadi kuwapelekea baadhi ya watu kuanza kuwa na majivuno! Hii ni kweli, kama nchi, lakini Watanzania si tajiri. Maisha ya Watanzania ni duni mno hata kuliko ya Wasomali, Wasudan au WaComoro (moja ya nchi maskini sana), ukilinganisha uwezo wao wa kununua (purchasing power) wa walio wengi.

Ukitazama jinsi serikali inavyowachukulia raia wa Tanzania, utaona wazi kwamba kauli hii ya utajiri unaodaiwa wa Tanzania imewaingia kichwani, na wanaamini kuwa Watanzania wengi wanafaidi 'utajiri' huo.

La sivyo, unawezaje kuweka kodi ya laki tatu, milioni moja nk wakati ni kazi chache sana zinalipa mshahara huo? Sikuambii malipo ya matibabu, dawa nk.

Tozo na kodi za serikai haziendani kabisa na pato la raia.

Dhana hiyo hiyo potofu inawatesa wanaotembelea Tanzania. Nimewasikia watalii wakilalamika kuwa Tanzania "is expensive".
Ndiyo maana sishabikii hata hayo 'maendeleo' kwa vile si wengi watakaoweza kufaidi.

We wadhania tiketi ya SGR kutoka Dar hadi Morogoro tu itakuwa shs ngapi? Tuishaona nauli za ndege, mwendo kasi etc.

Yaelekea kuna mtu hajui hali halisi za Watanzania.
 
Unatuletea nadharia ya miaka ya 90 Sisi. Badirika mkuu, Hii nchi ni tajiri achana na watu. Poor allocation of resources ndio inafanya hiyo purchasing power kuwa ndogo.

Haki ya Mungu na kwamba kama tukizitumia resources tulizonazo in efficiency way kisha tukazi allocate in efficiency way, hiyo purchasing power kwanini isiongezeke.

Poor leadership poor leadership ya zamani ndio imefanya Watanzania kuwa maskini. Kiongozi wa zamani alibugia utajiri wetu wote tumboni mwake, sasa hiyo purchasing power inaongezekaje kwa mfano.
 
Duh, kuna watu bado wana Inferiority Complex of mind
Kama wewe
nadhani wewe ndio mwenye inferiority complex of mind na ndio sababu unakuja kulalamika humu. Kama wewe ni maskini wa mawazo kwanini usiwe maskini. Sie wengine ni matajiri. You are poor because you have scarcity for knowledge.
 
Nchi ni tajiri kwa maana ya raslimali lakini wananchi wake ni masikini kwa sababu ukosefu wa uongozi bora.Shida ya Afrika ni mfumo wa uongozi na sio raslimali.

Thus wakoloni wao walituletea maendeleo kwa raslimali hizihizi ambazo viongozi hawawezi.Tanzania ni ya pili baada ya congo kwa utajiri mali kidunia.Afrika ndilo bara la Kwanza kwa utajiri mali duniani.
 
Tanzania inatakiwa impate kiongozi Kama Gadaffi yaani kiongozi anaeguswa na umasikini wa watu, mzalendo,mwenye vision,anaesikiliza watu, anaefanya vipaumbele vya wananchi na sio vipaumbele vyake.
 
Unatuletea nadharia ya miaka ya 90 Sisi. Badirika mkuu, Hii nchi ni tajiri achana na watu. Poor allocation of resources ndio inafanya hiyo purchasing power kuwa ndogo....
Magufuli ndio huyu anakaza msuli watu wanakesha kumsimanga kila siku.

anyway sio ishu ninachompendea hajali kelele.
 
Kwenye points yako ni kweli tozo za kodi haziendani na kipato halisi cha mtza.Kukazania tu kutoza Kodi huku ukiua uzalishaji usitegemee kukusanya zaidi.Ukiua sekta binafsi, ukisomesha watu namba, ukizuia mzunguko wa pesa mtaani, uchumi na makatazo haviendani kukazania makatazo ya sheria KILA kitu uua uchumi,kodi komozi ni ngumu Sana kupata makusanyo.

Kodi inapokuwa komozi kubwa uchochea ukwepaji mkubwa wa kodi kwa maana walipa kodi wataungana na watunza sheria njia salama za ukwepaji Kodi.Kodi inapokuwa rafiki Hakuna atakaefikiria kukwepa Kodi.

Raslimali zilizopo hazitumiki kabisa yaani ni uwiano Mdogo Sana Kati matumizi ya raslimali zetu na nguvu Kazi iliyopo sababu kuu ni ukosefu wa maarifa ya uzalishaji.
 
Nchi tajiri Watendaji wanapiga mwananchi magumi kwasababu ya michango?
Mtawala kageuza nchi Kama shamba lake binafsi kwa msaada wa wapambe wanufaika wachache, ufanya vipaumbele vyake vimpavyo sifa hata Kama si tija kwa mlipa Kodi
 
Tza inatakiwa impate kiongozi Kama Gadaffi yaani kiongozi anaeguswa na umasikini wa watu, mzalendo,mwenye vision,anaesikiliza watu, anaefanya vipaumbele vya wananchi na sio vipaumbele vyake.
Yule alikua ni Dikteta kamili! Ishu ni pale mnapo tawaliwa na Dikteta ambaye hajakamilika! a.k.a Dikteta Uchwara! Aisee mtalia na kusaga meno.

Maana hao Madikteta Uchwara na ambao kimsingi wametamalaki katika Nchi nyingi za Kiafrika, hujiangalia zaidi wao wenyewe, marafiki zao, vimada wao, ndugu zao, watoto wao, vyama vyao,nk.

Wamejawa na uongo, unafiki, ukatili, ubinafsi, uroho wa madaraka, ulevi wa madaraka, u mungu mtu, ubabe wa kijinga, dharau, kejeli kwa wananchi wenzao, vitisho, nk.
 
Unatuletea nadharia ya miaka ya 90 Sisi. Badirika mkuu, Hii nchi ni tajiri achana na watu. Poor allocation of resources ndio inafanya hiyo purchasing power kuwa ndogo...
Utajiri uusemao ni lzm ureflect maisha ya watu,Kama watu wanakosa basic needs,wanakufa njaa wanakula mara 4 kwa wiki sababu hawana purchasing power, watoto wanakaa chini,vyoo unategemea msaada utasema vipi wwe ni nchi tajiri.Shida nchi hii bado haijapata kiongozi mwenye uchungu angalau waliotangulia.
 
nadhani wewe ndio mwenye inferiority complex of mind na ndio sababu unakuja kulalamika humu. Kama wewe ni maskini wa mawazo kwanini usiwe maskini. Sie wengine ni matajiri. You are poor because you have scarcity for knowledge.
Atuzungumzii utajiri wa mtu mmoja mmoja tunaangalia wa Jamii nzima.Kama wwe ni tajiri je umeshafanya jitahada gani kuhakikisha Jamii inayokuzunguka imeondokana na umasikini.Nani mwenye jukumu la kupeleka maarifa kwa masikini ili wazalishe?

Mfano wakoloni wao walitengeneza mifumo ambayo ilichochea uzalishaji awakutegemea kodi kuendesha nchi bali uzalishaji kodi iliwekwa tu Kama tools ya kuwaforce watu kufanya kazi.Wao walijenga maghala Kazi ya mkulima ilikuwa ni kulima na kupeleka ghalani unalipwa, walitengeneza mifumo ya ajira mfano estates, viwanda,nk automatically tu watu walipata ajira.

Bado shida kuu ni uongozi bora ndio chanzo cha umasikini wetu. Uchumi unajengewa kwa kuchochea uzalishaji na sio kukazania tu Kodi KILA kitu ni Kodi tu.Kodi isipoendana na uhalisia wa uzalishaji ni lzm nchi ifilisike.
 
Wanaosema hii nchi ni tajiri wako sahihi, maana wanapata huduma zote bure kwa gharama za serikali. Chochote watakacho kuanzia usafiri, malazi, elimu, afya nk kwao wanavipata kirahisi. Ila watanzania walio wengi wanaishi kimaskini sana.
 
magufuli ndio huyu anakaza msuli watu wanakesha kumsimanga kila siku.

anyway sio ishu ninachompendea hajali kelele.

Angekuwa hajali kelele watu wasingetekwa na kupigwa risasi, ama uchaguzi kunajisiwa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom