Yafahamu zaidi majina ya Nelson Mandela

Yafahamu zaidi majina ya Nelson Mandela

Peter Mwaihola

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2022
Posts
276
Reaction score
460
Aliyekuwa rais wa kwanza mweusi wa taifa huru la Afrika ya kusini alifahamika zaidi kwa majina mawili ya Nelson Mandela.

Hayati Mandela aliyezaliwa 1918 na kufariki 2013 alikuwa na majina mengine zaidi aliyoitwa katika Kipindi cha maisha yake.

Kila jina aliloitwa kilikuwa na maana yake lilipotumika.

1. Rolihlahla. Hili lilikuwa jina lake la kuzaliwa, lilikuwa jina la kabila ka Khosa lililokuwa na maana ya kuvunjavunja matawi ya miti. Jina hili alipewa na baba yake.

2. Nelson. Jina hili alipewa na mwalimu wake siku ya kwanza shuleni, Mwalimu Mdigane alimpa jina hilo ikiwa ni kawaida kwa kipindi hicho kuwabatiza majina ya kizungu watoto wa Kiafrika ili kuendana na utamaduni wa kizungu.

3. Madiba. Hili ni jina la ukoo ambao hayati Mandela alitoka, jina la ukoo lilikuwa na umuhimu mkubwa kuliko na baba mzazi katika utamaduni wa vizazi vya Afrika kusini. Madiba lilikuwa ni jina la mtawala wa kiasili "Thembu" ambaye alitawala eneo la Transkei katika karne ya 18.

4. Tata. hili lilimaanisha "Baba" kwa lugha ya kikhosa, Mandela aliitwa jina hilo ikiwa ni heshima kwa kile alichokifanya katika taifa lake, watu wote walimuita jina hili hata wale waliomzidi umri.

5. Khulu. Mandela aliitwa Khulu ikimaanisha Mkuu, pia walimuita "Tat'omkhulu" likimaanisha "Babu" kwenye lugha ya kikhosa.

6. Dalibhunga.
jina hili alipewa akiwa na umri wa miaka 16 alipotoka jandoni, lilikuwa na maana ya uongozi wa baraza au muongoza mjadala.

Follow Peter Peter Mwaihola

Photo_1676384990338.jpg
 
Aliyekuwa rais wa kwanza mweusi wa taifa huru la Afrika ya kusini alifahamika zaidi kwa majina mawili ya Nelson Mandela.

Hayati Mandela aliyezaliwa 1918 na kufariki 2013 alikuwa na majina mengine zaidi aliyoitwa katika Kipindi cha maisha yake.

Kila jina aliloitwa kilikuwa na maana yake lilipotumika.

1. Rolihlahla. Hili lilikuwa jina lake la kuzaliwa, lilikuwa jina la kabila ka Khosa lililokuwa na maana ya kuvunjavunja matawi ya miti. Jina hili alipewa na baba yake.

2. Nelson. Jina hili alipewa na mwalimu wake siku ya kwanza shuleni, Mwalimu Mdigane alimpa jina hilo ikiwa ni kawaida kwa kipindi hicho kuwabatiza majina ya kizungu watoto wa Kiafrika ili kuendana na utamaduni wa kizungu.

3. Madiba. Hili ni jina la ukoo ambao hayati Mandela alitoka, jina la ukoo lilikuwa na umuhimu mkubwa kuliko na baba mzazi katika utamaduni wa vizazi vya Afrika kusini. Madiba lilikuwa ni jina la mtawala wa kiasili "Thembu" ambaye alitawala eneo la Transkei katika karne ya 18.

4. Tata. hili lilimaanisha "Baba" kwa lugha ya kikhosa, Mandela aliitwa jina hilo ikiwa ni heshima kwa kile alichokifanya katika taifa lake, watu wote walimuita jina hili hata wale waliomzidi umri.

5. Khulu. Mandela aliitwa Khulu ikimaanisha Mkuu, pia walimuita "Tat'omkhulu" likimaanisha "Babu" kwenye lugha ya kikhosa.

6. Dalibhunga. jina hili alipewa akiwa na umri wa miaka 16 alipotoka jandoni, lilikuwa na maana ya uongozi wa baraza au muongoza mjadala.

Follow Peter Peter Mwaihola

View attachment 2517416
Halafu hakuwa na rekodi ya damu ya wananchi mikononi mwake kama hawa "mashujaa" wengine
 
ICON pekee Africa huyu
Icon ya Africa ni Mwl. Nyerere, hata hiyo Mandela mwenyewe alikuwa anamkubali sana kaka yake Nyerere na alijifunza mengi sana kwa gulu Nyerere.
Kilichompandisha Mandela ni ile kuwa against na Apartheid system ambayo dunia nzima ilijua jinsi waafrika wa south walivyokuwa wakibaguliwa na watu weupe Boaz.
 
Back
Top Bottom