Yahya Zayed achukuliwa na Ismailia ya Misri

Turnkey

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2013
Posts
7,359
Reaction score
5,837
MSHAMBULIAJI chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Yahya Zayed anayechezea klabu ya Azam FC ya Dar es Salaam ameomdoka jana mjini Dar es Salaam kwenda Misiri kujiunga na klabu ya Ismailia ya huko.
Zayed mwenye umri wa miaka 20 aliondoka kwa ndege ya shirika la Ethiopia moja kwa moja kwenda Cairo ambako imeelezwa akifika atasaini mkataba wa miaka mitatu.
Na hiyo ni baada ya Ismailia, moja ya klabu kongwe nchini Misri kumalizana na Azam FC juu ya mchezaji ambaye alikuwa amebakiza mkataba wa miaka miwili.
Akisaini mkataba huo, Zayed atakuwa mchezaji wa pili wa Tanzania katika Ligi Kuu ya Misri, baada ya kiungo Himid Mao anayechezea Petrojet ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa Azam FC.
 
Tatizo taarifa za wachezaji wa kibongo kwenda kucheza nje huwa zinaongezwa chumvi nyingi, miezi kadhaa iliyopita tuliambiwa habib kiyombo anaenda kujiunga mamelodi sundowns lakini mpaka leo yupo mwananyamala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…