Yalionikuta leo ni zaidi ya Yona alivyo mezwa na samaki

shin gun wook

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2017
Posts
995
Reaction score
1,514
Leo asubuhi niliamka vizuri kujiandaa kwenda ibada.wakati naendelea kujiandaa kuna binti akanitumia ujumbe kwamba anaitaji kushinda na Mimi siku ya leo .Mara papuu roho ikadunda ni kweli au ananitania maana nilishamjaribu kama Mara moja akazingua basi nikala hamsini zangu.nikamuendea hewani nikacomfirm yupo serious.shetani ana mbinu,
sikukumbuka tena ibada
.nikajiandaa kwenda tulipopanga.wakati natoka ghafla nyuki wakanivamia kumbe walikua kuna mti wanahamia sasa na harufu ile ya perfume sujui waliniona Mimi maua.walinivamia wengi .nikaona sasa wataniua washenzi hawa.nikajirusha kwenye dibwi la maji machafu ya mvua ,kila nikanyanyua kichwa wapo juu wananikwidaa sijui walitumwa.ikabidi nitoke mbio kukimbia nisipojua.mpaka sasa nimevimba uso jicho linaona kwa shida .Shetani kaniponza .Maturu mwili mzima.mpaka najiuliza hivi yona alivyomezwa na Samaki aliumia kama Mimi?yule binti badae kumtafuta kumwambia aniletee dawa za maumivu ,kaniandikia"nyoo si ungesema Una hela ya kutoka pamoja,ovyoo".maumivu Mara mbili.hawa mabinti hawa.ningekwenda ibada yote yasingenikuta.sasa nimejifungia ndani na ugulia maumivu.Jioni njema
 
Hahaaaa pole mkuu nikajua nawewe umemezwa na nyuki
 
Ningelikuwa ni wewe, ningeandaa sadaka ya shukrani kwa sababu hujui Mungu kakuepusha na nini. Nadhani ilikuwa siku yako ya kilio kwani ndo maana Mungu akakufinya japo kidogo tu ukome kutafuta vijisichana vya watu. Pole lakini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…