Yaliyojiri jana Kanumba day "Dar live" Tundaman, Snura, Bongo muvi wafunika

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
.

Msanii wa kundi la Tip Top Connection Khalid Ramadhan 'Tundaman' akiwapagawisha mashabiki katika Kanumba Day





Snura Mushi 'Mamaa Majanga' akifanya yake stejini usiku huu ndani ya Dar Live.





Mshereheshaji wa shughuli ya leo, Maimartha wa Jesse akiendesha mambo ndani ya Dar Live.





Mtanga akionyesha umahiri wake katika kusakata sebene.




Msanii Jacob Steven 'JB' akionyesha vitu vyake stejini.




Seth Bosco ambaye ni mdogo wake marehemu Kanumba akimkumbuka kaka yake kwa sebene.





DJ Max akiwa kazini.





Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba akizindua rasmi Kanumba Foundation usiku huu ndani ya Dar Live.
 

Attachments

  • k1.png
    161.2 KB · Views: 2,044
  • k2.png
    118.8 KB · Views: 2,022
  • k3.png
    310 KB · Views: 2,074
  • k4.png
    145 KB · Views: 2,018
  • k5.png
    139.9 KB · Views: 1,975
  • k6.png
    112.4 KB · Views: 1,959
  • k7.png
    151.4 KB · Views: 1,851
  • k8.png
    150.7 KB · Views: 1,837
Kanumba huko alipo nahisi hapumuii jamanii lol RIP THE GREAT
 
Mama yake nae kafirisi kila kitu cha mwanaee lol hana hata aibuu mamaee
 
haaa kumbukumbu ya namna hii kwa marehemu haifai eti wanacheza sebene. yani wanawaza kupiga ela tu kwa jina la marehemu utaskia ngwair day pia
 

Mi nilijua kuna Karume day, Nyerere day tu, kumbe kuna hadi Kanumba day??
 
Hii ndio nchi pekee hata mwehu akipewa itasonga tu sasa huu upuuzi gani ngoja zije bi Kidude day,Ngwair day,Sharo day nk alafu mwisho wa siku tutaambiwa tupumzike kwenye hizi siku.
 
kumbu kumbu ya kifo inakumbukwa kwa kukata viuno na kuandaa washereshaji...

kumbukumbu nzima imejaa furaha na mifuniko, nani kamzidi nani... mbona sioni hata wakisema ama kusoma nini wamefanya kumuenzi huyu mtu, mbona hawasemi nini wamemfanyia angalau kulinda heshima yake?

JB nae na akili zake anakata mauno tu, mipango hamna kichwani.. too lazy to think!!

hivi kama marehemu wangekuwa wanapewa ruhusa kwa kificho tu kuja kuangalia wanavyoenziwa, halafu wapewe mamlaka ya kuamua kitu, unadhani hawa wangeamuriwa nini na SK?
 
hha ha ha ha ha heaven yaonesha waboreka na mtu akicopy thread yote
 
marehem hafaidiki na hela wala hizo fund rising. Bali ananufaika kwa sala na dua zetu za kumuombea mungu amuepushe na adhabu.
Hayo wafanye kujinufaisha wao na kuongeza dhambi zao na siyo kufanya dhambi kwa mgongo wa marehemu
 
haaa kumbukumbu ya namna hii kwa marehemu haifai eti wanacheza sebene. yani wanawaza kupiga ela tu kwa jina la marehemu utaskia ngwair day pia
Hii inaitwa kamata fursa.
 
siwapendi bongo movie kiukweli coz akili zao kama kotama yaani hawajielewi wote eti KANUMBA DAY na bado hiyo siku waligeuza MIKASI DAY hii ni laana ni inashangaza mama kanumba anakubali huu ujinga baada ya kumuombea dua marehemu tunakata mauno stejini na wakitoka hapo wakina snura wanaenda kukata mauno kitandani!!!!!!
 
Kanumba nitamkumbuka kama kijana aliyejua nini anachokifanya na alikuwa anajifunza kitu kipya.Hakuogopwa kuchekwa kwenye kujifunza kitu na alikuwa na bidii kwenye kujifunza kitu.Kwenye suala lake la Kanumba foundation naomba mama yke asiwe msimamizi wa moja kwa moja maana mama ameonesha udhaifu mkubwa kwenye kusimamia mali alizoacha marehemu.
 
Watu hapo wamepiga zao wameondoka wanajifanya eti kumkumbuka kanumba
 
Lala unapostahili kanumba haya mengine ya sebene yaache tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…