Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Kesi ya kumng'atua Naibu Rais Rigathi Gachagua inayoendelea kwa sasa mbele ya Seneti imefuatia kupitishwa kwa hoja ya kumwondoa madarakani na Wabunge 281 ambao walikubaliana na madai yaliyowasilishwa na Mbunge wa Kibwezi Magharibi, Mwengi Mutuse.
Wakati wa kuhojiwa, kikosi cha mawakili wa Gachagua, kinachoongozwa na wakili Elisha Ongoya, iliipinga hoja iliyowasilishwa na Mutuse kwa nguvu. Katika hotuba yake ya ufunguzi, Ongoya alitaja madai hayo kama "ya uongo," "ya kipuuzi," na hata "ya aibu."
"Mambo yanazidi kuwa moto lakini tazama hali hiyo, tulia na usome. Jumla ya hisa katika Kampuni ya Vipingo Beach ni ngapi?" Ongoya alimuuliza Mutuse.
Aliangazia orodha ya kampuni 22 zilizotajwa na Mutuse, ambapo mbunge huyo alisema kwamba hawakuwa na matatizo na kampuni nyingi kati ya hizo.
Aidha, Ongoya alizungumzia madai ya Gachagua kujilimbikiza mali ya KSh bilioni 5.2 tangu aingie ofisini mwaka wa 2022.
Akibanwa Katika Mjadala wa Kumbandua DP Gachagua Mutuse alithibitisha kuwa alifikia hesabu hizo kupitia mahesabu yake.
Baada ya ukaguzi huo, Wakenya wengi wameonyesha kuvutiwa na jinsi Ongoya alivyoendesha kesi hiyo mahakamani.
=====================
KENYA: BUNGE LA SENETI KUPIGA KURA HATMA YA GACHAGUA
Bunge la Seneti linaendelea na mchakato unaohusisha tuhumba mbalimbali dhidi ya Naibu Rais Rigathi Gachagua ambapo kuna uwezekano wa kupiga kura leo Oktoba 17, 2024 ili kuridhia au kutoridhia kuondolewa kwenye nafasi yake ya Naibu Rais
Mchakato wa Wanasheria kubishana kwa hoja juu ya tuhuma zinazomkabili kiongozi huyo unaendelea Asubuhi na itakapofika jioni Wajumbe wa Bunge wanatarajiwa kuwa na mjadala kuhusu kinachoendelea kwa muda wa saa mbili kisha ratiba ikiruhusu wanawe kupiga kura usiku kuamua hatma ya Gachagua
Ikiwa theluthi mbili ya Wajumbe 67 wa Bunge hilo wakipiga kura ya kuridhia Gachagua kuondolewa madarakani, hilo litapitishwa na Rais William Ruto atakuwa katika nafasi ya kuwa na Naibu Rais mpya.
Gachagua (59) anakabiliwa na tuhuma 11 ambazo amekana kuhusika nazo, ikiwa hilo litatimia atakuwa Naibu Rais wa kwanza kung’olewa tangu kutambulishwa kwa mfumo huo katika Katiba Mwaka 2010
Senate to vote on DP Gachagua's impeachment
Kenya's upper house of parliament is set to vote Thursday on whether to remove Deputy President Rigathi Gachagua from office in an unprecedented political saga that has gripped the nation.
The Senate will give its verdict at the end of the second day of an impeachment trial against the embattled number two to President William Ruto.
It follows a historic vote last week in the lower house, the National Assembly, to impeach Gachagua on 11 charges including corruption, insubordination, undermining the government and practising ethnically divisive politics.
A trial in the Senate began Wednesday after the 59-year-old, also known as "Riggy G", failed in multiple court bids to halt the process.
He is expected to testify in his defence on Thursday.
Gachagua has denied all the charges -- and no criminal proceedings have been launched against him -- but he will automatically be removed from office if the Senate approves his impeachment.
If this happens, he would be the first deputy president to be ousted in this manner since impeachment was introduced in Kenya's revised 2010 constitution.
Gachagua, who has protested that he is being treated like a "spent cartridge", can however fight the impeachment in the courts once the parliamentary process is completed.
Source: Citizen Digital
PIA SOMA